Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 13 Desemba 2019

TAASISI BINAFSI ZAOMBWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA YA AFYA KATIKA KUBORESHA HUDUMA NCHINI



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya vitanda vya wodi ya watoto wanaohitaji uangalizi maalumu (PICU) ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, vitanda hivyo vimetolewa na Benki ya NMB.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB Bw. Juma Kimoli, Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa Wizara ya Afya Bi. Deodatha Makani (Mwisho) wakiwa katika hafla ya upokeaji wa Vitanda vitano vya chumba cha watoto wagonjwa mahututi (PICU) katika Hospitali ya Muhimbili vilivyotolewa na NMB.


 Mwakilishi wa Benki ya NMB Bw. Juma Kimoli akikabidhi rasmi vitanda hivyo kwa Waziri Ummy Mwalimu.
Mwakilishi wa NMB Bw. Juma Kimoli (kushoto) akiwa na Waziri Ummy Mwalimu, Kaimu mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi Bi. Zuhura Mawona wakimuangalia mmoja wa watoto aliyelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu Muhimbili.

Waziri Ummy Mwalimu akiongea na baadhi ya wazazi walioleta watoto kwa ajili ya matibabu katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili kitengo cha watoto.

Waziri Ummy Mwalimu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Madaktari na Wauguzi wa wodi ya watoto wenye kuhitaji uangalizi maalumu (PICU), pamoja na wawakilishi wa Benki ya NMB.

Na Emmanuel Malegi-DSM

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ameziomba sekta binafsi ikiwamo benki ya NMB kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za Sekta ya Afya nchini.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati akipokea msaada wa vitanda vitano kutoka Benki ya NMB vyenye thamani ya shilingi Milioni 35 kwa ajili ya wodi ya watoto wanaohitaji huduma ya uangalizi maalumu (ICU) katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na vitanda 10 pamoja na magodoro 10 kwa Hospitali ya Muhimbili-Mloganzila vyenye thamani ya shilingi milioni 10. 

Amesema sekta binafsi zina wajibu mkubwa katika kuchangia shughuli za maendeleo ikiwamo huduma za afya kama ilivyofanya Benki ya NMB.

“Nawapongeza NMB kwa jitihada zao kwani msaada wa vitanda vya ICU ni msaada mkubwa kwa watoto na pia benki hii inafanya vizuri kurejesha fedha zake kwa jamii ikiwemo na kutoa gawio Serikalini”. Amesema Waziri Ummy.

Pia, Waziri Ummy amesema kutokana na juhudi za Serikali ya awamu ya tano, Muhimbili inaendelea kutoa huduma za kibingwa za hali ya juu zikiwemo huduma ya kupandikiza figo pamoja na huduma ya kupandikiza vifaa vya usikivu kwa watoto wenye matatizo ya kusikia.

Naye mwakilishi wa Benki ya NMB, Bw. Juma Kimoli ameipongeza Muhimbili na serikali ya awamu ya tano kwa kuboresha huduma za afya huku akisisitiza kuwa NMB imeweka utaratibu wa kuisaidia sekta ya afya kwa kutenga fedha kwa ajili ya kutoa misaada mbalimbali kwa jamii.

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi katika Hospitali ya Muhimbili, Bi. Zuhura Mawona ameishukuru NMB kwa msaada huo kwa kuwa umekuja wakati ambapo Hospitali hiyo kwa kushirikiana na wahisani imejenga wodi za uangalizi maalumu kwa watoto wenye umri kati ya siku 1 hadi siku 28 (NICU) na wenye umri wa siku 29 hadi miaka 14 (PICU), hivyo kuwa na uhitaji wa vitendea kazi mbalimbali ikiwemo vitanda.

 “Vitanda hivi vya kisasa vinatumia umeme na vinaweza kutumika kwa kupandishwa juu na kushushwa  kulingana na uhitaji,  hivyo vinasaidia mgonjwa kulazwa katika mlalo unaofaa na pia kupunguza maumivu ya mgongo kwa wauguzi na madaktari wakati wa kutoa huduma”. Amesema Bi. Zuhura.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa vitanda hivyo pia vimesaidia wauguzi kutoa huduma kwa urahisi na ufanisi zaidi ikiwamo kumwezesha mgonjwa kupumua (Intubation) kwa urahisi.

Kwa niaba ya Hospitali ya Muhimbili, Bi. Zuhura ameishukuru NMB kwa kutoa msaada huu na pia ameiomba kuongeza vitanda vingine kwani mahitaji ya vitanda ni makubwa kwa watoto wanaohitaji uangalizi maalumu.

0 on: "TAASISI BINAFSI ZAOMBWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA YA AFYA KATIKA KUBORESHA HUDUMA NCHINI"