Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 20 Desemba 2019

MUUGUZI ANAYETUHUMIWA KUBAKA MJAMZITO ASIMAMISHWA KAZI.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, akielekeza jambo mbele ya Wananchi waliojitokeza katika viwanja vya shule ya msingi Majalila Wilaya ya Mpanda, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma katika Mkoa wa Katavi.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda (Tanganyika) Bi Lilian Matinga akiwasalimu Wananchi, katika viwanja vya shule ya msingi Majalila Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Wananchi waliojitokeza katika viwanja vya shule ya msingi Majalila Wilaya ya Mpanda (Tanganyika) kumsikiliza Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Mkoa wa Katavi.


MUUGUZI ANAYETUHUMIWA KUBAKA MJAMZITO ASIMAMISHWA KAZI.

Na Rayson Mwaisemba WAMJW- Katavi

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo ameliagiza Baraza la Uuguzi na Ukunga kumsimamisha kazi muuguzi anayetuhumiwa kumbaka mama mjamzito katika kituo cha Afya Mamba kilichopo Kijiji cha Mamba Mkoani Katavi ili kupisha uchunguzi.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati akiongea na Wananchi katika viwanja vya shule ya msingi Majalila Wilaya ya Mpanda, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya na uboreshaji wa miundombinu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi.

"Naliagiza baraza la wauguzi na ukunga kusimamisha leseni ya muuguzi huyu wakati uchunguzi unafanyika  ".Amesema Waziri Ummy

Aidha,amewataka watumishi  wote wa afya nchini kufanya kazi kwa kuzingatia maadili, weledi na viapo vya kazi zao

“Na yeyote atakayefanya kazi kinyume na maadili,weledi na kiapo chake tutamchukulia hatua za nidhamu ikowemo kuwafutia leseni zao na kuwapeleka katika vyombo vya dola"Amesisitiza Waziri Ummy.

#TunaboreshaAfya

0 on: "MUUGUZI ANAYETUHUMIWA KUBAKA MJAMZITO ASIMAMISHWA KAZI."