Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 1 Desemba 2019

MAAMBUKIZI YA VVU YASHUKA NCHINI

Logo ya Siku ya UKIMWI.

Hadi sasa Watanzania milioni.1.4 wanaoishi na VVU ambapo kiwango cha maambukizi kikiwa ni asilimia 4.7 ikilinganishwa na asilimia 7.0 ya mwaka 2014.

Hayo yamesemwa leo na Mgeni rasmi wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya UKIMWI duniani  na Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemevu Mhe. Jenista Mhagama jijini Mwanza.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.
Waziri Mhagama amesema kuwa maambukizi mapya na vifo  vitokanavyo na UKIMWI pia vimepungua.
 "Tumeweza kupata mafanikio haya kufuatia kuboreshwa kwa huduma.za ART na afua za kinga kama vile utahiri wa kitabibu wa wanaume na kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto"Alisema Waziri Mhagama.

Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenister.

Aidha, amesema kiwango  cha watu wanaoishi na VVU walioko kwenye mpango wa ARV kimeongezeka kutoka asilimia 22 mwaka 2009 hadi kufikia asilimia 57 ya mwaka 2017.

Naye Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema mpaka kufikia mwezi Septemba 2019 takribani watu 1,252,205 kati ya wananchi 1,600,000 wanaokadiriwa kuishi na VVU nchini walikuwa wamepima na kufahamu hali zao za maambukizi ya VVU. 
"Hii ni sawa na asilimia 78.3 ya lengo la 90 ya kwanza.
Miongoni mwao wanaume walikuwa 413,985 sawa na asilimia 33, na wanawake walikuwa 838,220 sawa na asilimia 77".

Mhe. Jenister akiwa na Mhe. Ummy Mwalimu.
Kwa upande wa vijana Waziri Ummy amesema kuwa Vijana balehe (umri wa miaka 10 – 19) walikuwa 57,167 sawa na asilimia 4.6, na vijana (umri wa miaka 15 – 24) walikuwa 96,006 sawa na asilimia 7.7.

Aidha, amesema kati ya waliopima na kutambua afya zao watu 1,221,799 sawa na asilimia 97.6 wanatumia ARV. 

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella.

 Hata hivyo alisema Lengo la 90 ya pili ambalo ni asilimia ya kuwa watu waliopimwa na kugundulika kuwa wana maambukizi ya VVU wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU (yaani ARV’s), tayari tumefikia takriban asilimia 98 wanatumia zawa za kupunguza makali ya VVU yaani ARV.

"Lengo la 90 ya tatu, ambalo ni kuhakikisha kuwa asilimia 90 ya wanaotumia ARV’s wamefanikiwa kupunguza wingi wa VVU mwilini Waziri huyo alisema wamefanya vizuri sana,"ni kuwa tumekuwa tukifuatilia kwa karibu hali za watu wanaotumia dawa za kupunguza makali ya VVU".Alisema 

Mhe. Jenister Mhagama akiwa na Mhe. Ummy Mwalimu, wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa TACAIDS Leonard Maboko.

Waziri Ummy alitaja mafanikio mengine ya kujikinga dhidi ya maambukizi ni tohara kwa wanaume ambapo kuanzia mwaka 2009 hadi Agosti 2019 jumla ya wanaume 4,456,511 wamefanyiwa tohara kupitia njia za mkoba na huduma katika vituo vya huduma.

Takwimu zinaonesha kwamba watu 953,973 sawa na asilimia 89 ya watu 1,072,650 waliopimwa wingi wa VVU wamefanikiwa kupunguza wingi wa VVU mwilini jambo ambalo ni muhimu katika kinga dhidi ya UKIMWI.Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "Jamii ni chachu ya mabadiliko,tuungane kupunguza maambukizi mapya ya VVU"

Wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Rock City Mall leo, kushuhudia Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani, mgeni rasmi akiwa Waziri Jenister Mhagama, aliyemwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Kassim Majaliwa.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenister Mhagama, aliyemwakilisha Mgeni rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Mhe. Kassim Majaliwa.


#TunaboreshaAfya.
#WAMJW









0 on: "MAAMBUKIZI YA VVU YASHUKA NCHINI"