Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 18 Desemba 2019

WARATIBU WA MTUHA WATAKIWA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA TAKWIMU SAHIHI

Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Saitore Laizer akiongea na waratibu wa  mfumo wa taarifa,na ufuatiliaji wa huduma za afya kutoka mikoa na halmashauri nchini.

Kaimu mkurugenzi msaidizi ufuatiliaji na tathimini kutoka wizara ya afya Tumainiel Macha  akiongea kwenye kikao kazi hicho.

Mwenyekiti wa waratibu hao Dkt. Ally Msoke akitoa neno la shukrani wakati wa ifunguzi wa mkutano huo.

 Waratibu hao wakimsikiliza mgeni rasmi(hayupo pichani)  wakati wa ufunguzi wa kikao kazi hicho.kinachofanyika chuo cha mipango Dodoma.

Picha ya pamoja ya watumishi kutoka wizara ya afya na OR-TAMISEMI na mgeni rasmi.


WARATIBU WA MTUHA WATAKIWA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA TAKWIMU SAHIHI

Na. Catherine Sungura, Dodoma

Waratibu wa Mfumo wa Taarifa za Utoaji wa Huduma za Afya (MTUHA) nchi wametakiwa kuimarisha upatikanaji wa takwimu sahihi za sekta ya afya  katika maeneo yao ya kazi.

Rai hiyo imetolewa leo na Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali ambaye pia ni mkurugenzi wa mafunzo na rasiliamali watu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Saitore Laizer wakati akifungua  kikao kazi cha waratibu MTUHA wa mikoa na halmashauri Tanzania kinachofanyika jijina hapa.

Dkt. Saitore amesema kuwa Wizara imeboresha mfumo wa takwimu kulingana na mahitaji  ya sasa na zinaingizwa na kuchanganuliwa kwa kutumia program maalum ya kompyuta katika ngazi ya wilaya ijulikanayo  kama ‘District health information software-DHIS 2’, hivyo ana imani  watasimamia na kuratibu kwa umakini.

“Matarajio ya wizara ni kuwa takwimu  zinazopatikana kutoka katika program hii zitakuwa sahihi  na mtatengeneza  orodha ya kielekroniki ya vituo vya kutolea huduma  za afya  ili kusaidia  katika mipango na kutoa maamuzi katika Sekta ya Afya”.

Vile vile Dkt. Saitore aliwataka waratibu hao kuweka mipango kabambe ili kuhakikisha mrejesho wa zoezi la uhakiki  wa ubora wa takwimu za afya  uliofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali pamoja  na kutoa mafunzo ya mrejesho katika meza maalum zitakazoandaliwa ili kutoa msaada wa watumishi ambao wanahitaji kujifunza,kupata ufafanuzi au kuuliza na kupata majibu ya masuala ya MTUHA yanayowasumbua  katika maeneo ya kazi .

Hata hivyo aliwataka waratibu hao kuhakikisha  halmashauri zinatenga fedha kwa ajili ya  MTUHA katika mpango kabambe wa  halmashauri(CCHP) na timu za  za afya za mikoa na halmashauri na Wadau wa Maendeleo wanashiriki kikamilifu katika kuimarisha  upatikanaji wa takwimu sahihi za Sekta ya Afya.

Mfumo wa taarifa za utoaji wa huduma za afya nchini umesaidia kuwezesha sekta ya afya kupata takwimu sahihi na kwa wakati zinazowezesha kufanya maamuzi sahihi katika kupanga na kutekeleza malengo yake ili hatimaye kufikisha huduma bora kwa wananchi kutoka asilimia 43 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 85 mwaka 2019.

0 on: " WARATIBU WA MTUHA WATAKIWA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA TAKWIMU SAHIHI"