Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 20 Desemba 2019

HOSPITALI YA KANDA YA RUFAA MBEYA (MZRH) YAANZISHA KIWANDA CHA UZALISHAJI MAJI TIBA (DRIP)

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji akiongea na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Wizara ya Afya na Taasisi zake (hawapo pichani) wakati walipotembelea Hospitali hiyo ili kuona mafanikio katika kipindi cha miaka minne ya Rais Magufuli madarakani.

Baadhi ya chupa za maji ya tiba zinazotengenezwa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya.

Mtaalamu akionesha jinsi maji ya tiba yanavyotengenezwa

Mashine ya kutengeneza maji ya tiba



Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya imetaja mafanikio iliyopata katika kipindi cha miaka minne ya Rais Dkt. John  Pombe Magufuli akiwa madarakani ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa kiwanda chenye uwezo wa kuzalisha maji tiba lita 3,840  kwa mwezi.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Dkt. Godlove Mbwanji alipokuwa akizungumza na Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Wizara ya Afya na Taasisi zake walioambatana na waandishi mbalimbali wa habari katika kutekeleza kampeni ya “Tumeboresha Sekta Ya Afya” katika mikoa ya nyanda za juu kusini.

Dkt. Mbwanji amesema Hospitali hiyo imetekeleza kwa vitendo sera ya Viwanda ya Awamu ya Tano pamoja maagizo ya Rais Dkt. John Magufuli kwa kuanzisha kiwanda cha uzalishaji wa maji tiba “Drip”.

Amesema kiwanda hicho kilianzishwa Februari 2019 kwa gharama ya TSh. Milioni 120  kwa mapato ya ndani na kinazalisha dripu hizo zenye lita za ujazo 250 na 500 zimeanza kutumika kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wenye uhitaji.

“Hali hii imesaidia kuondokana na adha ya kununua au kuagiza dripu nje ya nchi na kiwanda kina uwezo wa kutengeneza maji tiba lita 3840  kwa mwezi huku uhitaji wa hospitali ni lita 5232 na hivyo kukidhi kwa asilimia 73 ya uhitaji wa maji tiba kwa ajili ya hospitali”. Amesema Dkt. Mbwanji.

Mkurugenzi huyo amesema wamefanikiwa kupunguza gharama za manunuzi ya maji tiba nje nchi, wana uhakika na upatikanaji wake, wametoa mafunzo ya utaalam wa utengenezaji wa maji tiba na kuongeza ajira kwa wataalamu wa kutengeneza bidhaa hiyo.

Aidha Dkt. Mbwanji amesema wanatarajia kuanza kutengeneza dawa ya macho na masikio kwenye kiwanda hicho mwaka 2020.

Hospitali hiyo inahudumia mikoa saba ya Nyanda za juu kusini  ambayo ni Iringa, Njombe, Ruvuma, Katavi Rukwa, Songwe na Mbeya na  imeendelea kuboresha huduma zake mbalimbali ili kutoa huduma bora za afya kwa wananchi.

Mafanikio mengine yaliyotajwa ni pamoja na kuwa na ongezeko la upatikanaji wa dawa kutoka asilimia 70 hadi 95,  ongezeko la madaktari bingwa kutoka 36 hadi 53, huduma za kibingwa za masikio, koo, pua.

Pia amesema kuanzishwa kwa chuo cha Udaktari cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tawi la Mbeya kumetoa fursa kwa madaktari kuanza kufanya tafiti mbalimbali, kuanzishwa kwa huduma ya mkalimani wa lugha ya alama, uwezo wa kulaza wagonjwa kutoka vitanda 477 hadi 553 baada ya kukamilika jengo la watoto.

Dkt. Mbwanji amesema Serikali ilitoa TSh. Bilioni 3 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Radiolojia ambalo baada ya kukamilika limefanikisha utoaji wa huduma za mionzi na kuanzisha huduma mpya za  CT Scan, mashine za kidigitali za X ray, Fluoroscopy, Mammography na Ultrasound.

MWISHO

0 on: "HOSPITALI YA KANDA YA RUFAA MBEYA (MZRH) YAANZISHA KIWANDA CHA UZALISHAJI MAJI TIBA (DRIP)"