Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Posted by kayombo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Posted by kayombo. Onyesha machapisho yote
Ijumaa, 29 Mei 2020
Alhamisi, 21 Mei 2020

SERIKALI INAHAKIKISHA WALENGWA WOTE WA CHANJO WANAFIKIWA KATIKA KIPINDI CHA CORONA
Alhamisi, Mei 21, 2020
-
Hakuna maoni
Na
Mwandishi Maalum – Pwani
20/05/2020
Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa
Taifa wa Chanjo imejipanga kuwafikia walengwa wote waliostahili kupata chanjo
na kuhakikisha kiwango kinabaki vilevile kama ilivyotarajiwa.
Hayo
yamesemwa leo na Ofisa Mradi kutoka Mpango huo Lotalis Gadau wakati wa
usimamizi elekezi wa kukagua utoaji huduma za chanjo katika Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na Engender Health kupitia
Merck Sharp& Dohme B.V (MSD).
Gadau
alisema kuwa katika kipindi hiki cha nchi kukabiliana na Ugonjwa wa Corona,
Wizara imejipanga kuhakikisha watoa huduma wa afya wanaendelea kutoa huduma za
chanjo kwa watoto wadogo pamoja na wasichana ambao walikua wapate chanjo ya
kujikinga na saratani ya mlango wa kizazi(HPV).
“Kama
Wizara tumejipanga vizuri kwa kuhakikisha chanjo zote zinakuwepo kwa wakati
kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kuhakikisha watoto wote waliokuwa
wanatarajia kupata chanjo wanapata,na watoa huduma wanachukua tahadhari zote za
kujikinga na ugonjwa huu”,
Alisema
walikuwa wakisikia wananchi wana wasiwasi kufika kwenye vituo vya kutolea
huduma,“tumepita kwenye vituo vya afya kwenye mkoa huu na tumeona hali ni zuri
kwani wazazi na mabinti wengi wanakuja kwenye vituo na tumewasisitiza kila
mmoja anayeenda awe balozi anaporudi nyumbani kuhakikisha wataambiana ili kila
anayestahili kupata chanjo anaenda kwenye kituo cha afya chochote cha jirani
aweze kupata chanjo”.
Vile
vile alisema kuhusu mabinti ambao walikua wapate chanjo ya kuzuia saratani ya malango wa kizazi tofauti na awali ambapo walikua wakifuatwa
mashuleni ila kutokana na janga la
Corona inasisitizwa wafike kwenye vituo
cha kutolea huduma za afya vya karibu
waweze kupata chanjo hiyo.
Upande wa watoto wadogo, Bi. Gadau amesema
hivi sasa umewekwa utaratibu kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka miwili
ambao wanastahili kupatiwa chanjo wao wanatakiwa kupata chanjo kama ilivyo
kawaida”Kwa kipindi hiki watoto ambao wamekamilisha ratiba ya chanjo na
wanafika kituoni kwa ajili ya uzito tu wao wanatakiwa waende kila baada ya
miezi mitatu hii ni kuepuka misongamano na tunasisitiza elimu ya afya ambayo
ilikua ikitolewa kwa muda mrefu au kusubiriana kwa sasa itatolewa kwa muda mfupi usiopungua dakika
tano lakini endapo mtoto atapata homa au tatizo lolote anatakiwa kupekekwa
kwenye kituo cha afya kwa ajili ya matitabu.
Naye
Mratibu Huduma za Chanjo kwa Mkoa wa Pwani Abbas Hincha amesema kuwa asilimia
90 ya walengwa wa chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa mabinti wenye umri
wa miaka 14 ambao hapo awali walikuwa wakipatiwa wakiwa shuleni ila kutokana na
janga hili wanashirikia na walimu wa shule zao kwani walikua wameandikishwa
hivyo wanawapatia namba za simu na kuwapigia wazazi na walezi ili kuwapeleka
kupatiwa chanjo hiyo.
Alisema
katika mkoa wake wamepanga mikakati mbalimbali ikiwemo ya kuwashirikisha watoa huduma ngazi ya jamii kuwatafuta
mabinti hao kwenye maeneo yao na kuwakumbusha kwenda kupata chanjo.
Alisema
muamko kwa chanjo kwa upande wa watoto wadogo unaendelea vizuri na kuna muitikio
mzuri hivyo wanaendela kutoa elimu jinsi ya kujikinga na Corona na kwenye vituo
ambavyo havina nafasi kubwa wanatoa huduma hizo nje ya kituo ili kuzingatia
umbali wa mita moja kati ya mtu na mtu
WAHIMIZWA KUJIPANGA, KUENDELEA KUTOA HUDUMA ZA MKOBA ZA CHANJO
Alhamisi, Mei 21, 2020
-
Hakuna maoni
Bi. Ipyana
Mwamwala Muuguzi Mkunga wa Kituo cha Afya Mtego wa Simba akimpima uzito mtoto
Niran Daudi (7) pembeni ni mama wa mtoto huyo, Bi. Joyce Mwantobe. Picha na
Englibert Kayombo
Bi. Elinivoniia Mchomvu Muunguzi Mkunga akisoma kitabu cha afya ya mtoto kabla ya kutoa
chanjo katika Zahanati ya Fulwe, Wilaya ya Morogoro VIjijini. Picha na
Englibert Kayombo
Ofisa Afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Lugata akitoa elimu kwa wananchi kuhusu ugonjwa wa Corona.kwa wananchi waliofika katika Kituo cha Afya Mtego wa Simba Wilaya ya Morogoro Vijijini kupata huduma za afya
Mwandishi
Maalum - Morogoro
Huduma ya chanjo za mkoba hasa
katika maeneo ya pembezoni (vijijini) zinapaswa kuendelea kutolewa kwa watoto
chini ya miaka mitano ili kuhakikisha wote wanafikiwa kwa wakati unaopaswa,
licha ya kuwapo kwa janga la Corona.
Pamoja
na kundi hilo, kundi jingine linalopaswa kufikiwa na kupatiwa chanjo ya ni
wasichana wenye umri wa miaka 14 ambao wanapaswa kupatiwa ile ya HPV inayokinga
dhidi ya maambukizi ya virusi hivyo vinavyosabisha ugonjwa wa saratani ya
kizazi.
Rai
hiyo imetolewa jana na Ofisa Miradi kutoka Mpango wa Taifa wa Chanjo wa Wizara
hiyo, Dk. Furaha Kyesi alipozungumza na uongozi wa Kituo cha Afya Mtego wa
Simba, kilichopo Wilaya ya Morogoro Vijijini, mkoani Morogoro wakati wa ziara
ya ukaguzi wa huduma za chanjo zinazotolewa kwenye vituo vya afya kipindi hiki
cha mapambano dhidi ya janga la Corona.
Timu
ya ufuatiliaji huduma za chanjo kutoka Mpango wa Taifa wa Chanjo (IVD) wa
Wizara hiyo, maofisa chanjo wa Mkoa wa Morogoro na wa Wilaya hiyo kwa
kushirikiana na Shirika la Engeder Health kupitia Merck Sharp & Dohme B.V
(MSD), wapo mkoani humo kukagua namna huduma za chanjo zinavyoendelea kutolewa
katika kipindi hiki cha janga la Corona.
“Kundi
hili la wasichana lazima tuhakikishe tunalifikia, kwa sababu hawa awali
msisitizo ulikuwa kuwapa chanjo kwa kuwafikia shuleni, lakini sasa shule
zimefungwa kutokana na janga la Corona, lakini tunahitaji kuwafikia.
“Watoto
chini ya miaka mitano nao lazima tuwafikie ili kwamba wakati tunapambana na
Corona tuhakikishe pia tunaendelea kuwapa chanjo dhidi ya magonjwa mengine kama
vile surua, polio, kuharisha na mengineyo, ili tusije tukapata mlipuko wa
magonjwa,” amesema.
Kyesi
ameshauri kwamba watoa huduma za afya waendelee kuzingatia mwongozo wa
kujikinga na kufikia maeneo ya pembezoni hasa huko vijijini kuwapa huduma.
Awali
akizungumza, Muuguzi Mkunga wa Kituo hicho, Ipyana Mwamwala alisema kila mwezi
hupokea watoto wapatao saba na kuwapa chanjo mbalimbali kulingana na umri wao.
Amesema
kituo hicho kimezungukwa na vijiji vinne ambavyo ni Sangasanga, New Land, Mkono
wa Mara, Mkambarani na Mtego wa Simba (chenyewe).
“Wakina
mama bado wana mwamko wa kuleta watoto kituoni lakini tunahitaji kwenda
outreach kwa ajili ya kuwafikia pia wale ambao hawaji kituoni, vijiji vipo
mbali na hapa,” amesema.
Ameongeza
“Tupo tayari kwenda, tunatambua, tumetangaziwa kuna ugonjwa wa COVID -19 nchini
ambao unatokana na maambukizi ya virusi vya Corona, hata hapa kituoni
tumechukua hatua na hata tukienda kule tutazingatia kanuni zote za kujikinga
sisi wenyewe na wale tunaokwenda kuwahudumia wasipate maambukizi.
Mganga
Mfawidhi wa Kituo hicho, Luambano Ally amesema kutokana na taarifa hiyo ya
tahadhari iliyotolewa na Wizara ya Afya, walilazimika kuchukua hatua za
kuimarisha kujikinga ikiwamo kuweka ndoo za maji katika maeneo ya kuingia ndani
ya kituo hicho.
“Kwenye
milango yote ya kuingia ndani ya kituo kuna ndoo ya maji safi tiririka na
sabuni lazima mtu anawe ndipo aingie huku ndani, lakini kama amejisahau kunawa
pale au anahitaji tena kunawa akiwa humu ndani, kuna ndoo nyingine tumeweka
ataweza kunawa pia.
“Hapa
kituoni tumewapa taarifa kwamba kila anayekuja kupata huduma lazima avae
barakoa, utaona hilo wanakijiji wanalitii na wamekuwa na mwamko, wanakuja
wakiwa wamevaa, wananawa mikono, wanapata huduma na kurudi zao nyumbani,”
amesema Ally.
MWISHO
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)













