Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 20 Septemba 2019

SASA NI ZAMU YA DAR - MAFUNZO YA KUDHIBITI MAGONJWA KATIKA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA


Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora Wizara ya Afya Dkt. Joseph Hokororo akitoa mafunzo mbele ya Watumishi wa Sekta ya Afya wakati wa Semina ya mafunzo juu ya  kujikinga dhidi ya Maambukizi kwa kufuata miongozo yakutoa huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).


Bi. Laura Marandu, Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora Wizara ya Afya akitoa mafunzo ya jinsi yakumkinga kichanga dhidi ya maambukizi mapya kwa kufuata miongozo ya IP.

Mtaalamu wa Maabara Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikikishi MUHAS Bw. Akili Mawazo Mwakabhana akisisitiza jambo mbele ya Watumishi wa Sekta ya Afya Jijini Dar es salaam, wakati wa Semina ya mafunzo yakujikinga dhidi magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).
 
Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Chrisogone Justine akijibu hoja wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata miongozo ya IPC wakati wa utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).
 

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya wakiwa katika  Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).



Baadhi ya wawezeshaji wa Semina ya mafunzo juu ya namna yakujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline) wasahisha mitihani ya kupima uelewa iliyofanywa na Watumishi wa Sekta ya Afya ngazi ya Mkoa (RHMTs) na ngazi ya Halmashauri(CHMTs).


Picha ya Pamoja ikiongozwa na Wataalamu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto sambamba na Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya baada ya kumaliza Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), Jijini Dar es salaam.







SASA NI ZAMU YA DAR -  MAFUNZO YA KUDHIBITI MAGONJWA KATIKA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA.

Na WAMJW - DSM

Watu zaidi ya milioni.1.4 duniani wanaugua magonjwa yanayosababishwa na kupata maambukizi mapya wakati wa kupata huduma.

Hayo yameelezwa na Afisa kutoka kitengo  cha Uhakiki Ubora Wizara ya Afya Dkt. Joseph Hokololo wakati wa mafunzo njia ya kujikinga dhidi ya Magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa, katika maeneo ya utoaji huduma yaendelea Jijini Dar es salaam, ikiwa ni moja kati ya mikoa iliyo katika hatari ya kupata magonjwa ya  mlipuko ikiwemo ugonjwa wa Ebola kutokana na muingiliano wa watu kutoka nchi mbali mbali 

Dkt.Hokololo alisema kuwa maambukizi hayo hutokana na watoa huduma za afya afya kutofuata taratibu za namna ya kutoa huduma.

Katika mafunzo hayo ambayo yametolewa na Kitengo cha Uhakiki Ubora, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa timu za uendeshaji huduma za Afya ngazi ya Mkoa (RHMT) na za Halmashauri (CHMTs) za Mkoa wa Dar es salaam

"Timu za uendeshaji huduma za Afya mnatakiwa kusimamia miongozo ya kukinga na kudhibiti maambukizi (Magonjwa) wakati mnatoa huduma za Afya kwa Wagonjwa ili kudhibiti maambukizi mapya"Alisisitiza Dkt.Hokololo

Aliendelea kusema kuwa Asilimia 15 ya Wagonjwa hupata maambukizi ya magonjwa mapya pindi waendapo kupata huduma za Afya katika Vituo vya kutolea Huduma za Afya, kutokana na kutofuatwa kwa miongozo ya kutoa huduma za Afya (IPC Guideline, SOP).

Aidha, Dkt. Hokororo amesema kuwa Tanzania ipo kwenye hatari ya kupata wagonjwa wa Ebola kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu na ukaribu na Nchi ya Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo ambako Mlipuko unaendelea.

Aliendelea kusisitiza kuwa, Serikali ya Tanzania tayari imekwisha kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha utayari wa kukabiliana na tishio la Ugonjwa huo ili kuhakikisha hauingii nchini, ikiwemo kuelimisha jamii njia za kujikinga na Ugonjwa ili kuzuia usiingie nchini, na kutoa Elimu kwa Watoa huduma za Afya juu ya kumuhudumia mtu mwenye dalili za Ebola endapo atatokea.

Kwa upande mwingine, Afisa kutoka Kitengo cha uhakika ubora Wizara ya Afya Bi. Laura Edward Marandu amesema kuwa kufuata miongozo ya utoaji huduma katika vituo vya kutolea huduma za Afya kusaidia kupunguza vifo vya vichanga pindi vinapozaliwa kwa kuvikinga dhidi ya maambukizi ya magonjwa yanayohusiana na sehemu za kutolea huduma za Afya (Health care associated infections)

Naye Mtaalamu wa Maabara kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS Bw. Akili Mawazo Mwakabhana amesema kuwa kutofuata miongozo ya IPC ni moja ya chanzo kikubwa cha ongezeko la maambukizi ya magonjwa yanayopatikana katika vituo vya kutolea huduma (nosalcomial diseases)

Mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Medipeace, yanatarajia kuendelea katika mikoa yote iliyo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Ebola ili kuhakikisha ugonjwa huo hauingii nchini.

MWISHO.

Jumatatu, 16 Septemba 2019

HAKUNA UGONJWA WA EBOLA TANZANIA



Serikali imesema hakuna ugonjwa wa Ebola nchini Tanzania na  kuwataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini kutoka nchi  za jirani ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (Congo DRC)
Hatua hiyo inakuja baada ya taarifa kuzagaa katika mitandao ya kijamii zikidai kuwa ugonjwa huo umeingia nchini na baadhi ya watu wameanza kufariki kwa Ebola.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu aliyekuwa akitoa taarifa rasmi ya Serikali kuhusu ugonjwa huo leo (Septemba 14, 2019) jijini Dar es Salaam amesema mpaka sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola. 

"Wizara inawasihi wananchi, kutokuwa na hofu kwani mpaka sasa hivi hakuna mgonjwa yeyote ambaye amethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola nchini Tanzania,” amesema Mwalimu.
Hata hivyo, amewataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na kudhibiti  ugonjwa huo ambao umeripotiwa katika nchi jirani usiingie nchini. 

"Ikumbukwe kuwa ugonjwa wa Ebola umethibitika kuwepo nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo ilitolewa taarifa kwa mara ya kwanza Agosti 2018 na hadi kufikia Septemba 12, 2019,  kuna jumla ya wagonjwa 3,099 ambao wamethibitishwa kuwa na ugonjwa huo,” amesisitiza Mwalimu.

Amesema  wizara yake  inapenda kuwahakikishia Watanzania kuwa tangu ugonjwa huo uliporipotiwa katika nchi jirani imeweka mikakati na kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa ili usiingie nchini kwa kufanya masuala mbalimbali ikiwemo kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huo kupitia katika wataalam wa afya katika mikoa, wilaya na maeneo ya mipakani.

Pia wizara imeimarisha uchunguzi wa wageni wanaoingia nchini kupitia mipakani na kununua vifaa mbalimbali ikiwemo kipima joto, ambavyo wasafiri kutoka nchi mbalimbali wanaohisiwa kuwa na ugonjwa huo wamekuwa wakipimwa kabla ya kuingia nchini.

Aidha, Serikali imenunua na kusambaza seti takriban 2,700 za mavazi kinga kwenye mikoa yote iliyo katika hatari ya kukumbwa na tishio la Ebola ambayo mikoa hii ni Kigoma, Kagera, Mwanza, Rukwa na Katavi, kwa sababu inapakana na DRC.


Dalili kuu za ugonjwa wa Ebola ni homa kali, kuumwa na kichwa, kutapika, kuharisha, viungo vya mwili kuuma, kutokwa na vipele mwilini na kutokwa na damu katika matundu ya mwili.

Alhamisi, 12 Septemba 2019

WIZARA YA AFYA YAPATA BILIONI 26.6 KUTOKA SERIKALI YA UJERUMANI


Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula pamoja na Mwakilishi kutoka Serikali ya Ujerumani Mrs. Vera Rosendahl wakijadiliana mambo kabla ya kusaini mkataba.
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la giz Dkt. Mike Falke akisaini mkataba wa makubaliano na serikali ya tanzania kupitia wizara ya afya katika kuimarisha afya ya msingi nchini, kushoto ni katibu mkuu wa wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula.

Katibu Mkuu Idara kuu Afya Dkt. Zainabu Chaula akisaini mkataba huo wa shilingi bilioni 26.6 kutoka Serikali ya Ujerumani,halfa hiyo ilifanyika kwenye ukumbi wa wizara uliopo mji wa serikali Mtumba.

Viongozi hao wakibadilishana mikataba hiyo mara baada ya kusaini.

Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula na baadhi ya viongozi wa  giz na serikali ya Ujerumani mara baada ya kusainiana mkataba
Na. Catherine Sungura- Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesaini mkataba wa makubaliano wa miaka mitatu na serikali ya Ujerumani kwa ajili ya kuimarisha afya ya msingi nchini.

Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainabu Chaula alisema kuwa wizara yake imesaini mkataba huo na serikali ya Ujerumani katika kuboresha sekta ya afya katika maeneo manne ambapo sekta hiyo itapata kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 26.6.

Dkt. Chaula amesema kwamba kwa mwaka huu wameweka makubaliano ili fedha hizo zitolewe kwa wakati mmoja na kuweza kutumia mfumo wa Force Akaunti kama walivyoweza kutumia kwenye ujenzi wa Vituo vya afya na Hospitali za Wilaya na Mikoa katika kuboresha sekta ya afya nchini.

“Tumeanza mahusiano tangu mwaka 1961, kuanzia  mwaka 2003 huu ni mkataba wa tano na mkataba wao ni wa miaka mitatu mitatu ambapo umejikita katika kuimarisha afya ya msingi katika halmshauri zetu katika vituo vya afya pamoja na zahanati”.

Dkt. Chaula alitaja maeneo yatakayonufaika na mkataba huo ni uhimarishaji wa taarifa, afya ya mama na mtoto, uzazi wa mpango, bima ya afya kwa akina mama wajawazito pamoja na utawala bora jinsi ya kutumia fedha hizi kulingana na kanuni na taratibu za nchi.

“Huu ni muendelezo wa mkataba wa miradi mingi ambayo tumeifanya katika kuboresha sekta ya afya, kama mnavyokumbuka hadi sasa hivi tumeshafanyia ukarabati wa vituo vingi vya afya ambapo tuna vituo 470 ambavyo vimeshafanyiwa ukarabati  tangu mwaka 2017 katika ngazi za zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya.

Aidha, Dkt. Chaula alisema Serikali iliwekeza shilingi bilioni mia moja na milioni mia tano katika hospitali za halmashauri.

“Zamani hawa wenzetu walikua wakitumia wakandarasi wao na pesa wanakaa nazo hivyo tumekaa nao na kukubaliana kama fedha hizi watazitoa kwa wakati mmoja ili tuweze kuzisimamia kama tulivyofanya kwenye vituo tulivyoanza ili kuweza kutekeleza kwa umakini na kupata matokeo makubwa katika kipindi hiki” . Amesema Dkt. Chaula.

Kwa upande wa hali ya uzazi, mama na mtoto Katibu Mkuu huyo alisema hivi sasa inakaribia asilimia 80 ya akina mama wajawazito wanajifungulia kwenye vituo vya afya tofauti na zamani ambapo kulikuwa na changamoto kubwa kwani wengi walikua wanajifungulia majumbani kwa asilimia 39 na kufuatia na asilimia 59 hii ni kutokana na kuboreshwa kwa  vituo vya afya pamoja  na mikakati mbali mbali ya kuhakikisha akina mama wote wanajifungulia kwenye vituo vya afya.
Mwisho

FUATILIENI MTOTO ALIYEKATWA MKONO MWANANYAMALA: DKT. NDUGULILE


Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokua akiongea wakati wa uzinduzi wa bodi ya maabara binafsi za afya kwenye ukumbi wa hoteli ya Veta jijini Dodoma.



Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Vivian Wonanji akiongea na washiriki waliohudhuria uzinduzi wa bodi hiyo


Msajili wa baraza la maabara binafsi za afya Dominic Fwiling'afu akiongea wakati wa uzinduzi.huo.
Kaimu Mwenyekiti wa bodi hiyo Prof. Said Abood akitoa neno la shukrani mara baada ya uzinduzi wa bodi ya maabara binafsi za afya ambapo aliahidi kufanya ukaguzi wa kuzibaini maabara ambazo hazijasajiliwa nchini.


Aliyekuwa mjumbe wa bodi iliyoisha muda wake Dkt. Charles Massambu akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile
Kaimu Msajili wa bodi ya Maabara binafsi Dickson Majige akipokea cheti cha shukrani wakati wa uzinduzi huo.


Baadhi ya wasajili wa mabaraza ya kitaaluma yaliyo chini ya wizara ya afya wakimsikiliza Naibu Waziri(hayupo pichani) wakati wa uzinduzi huo.

Picha ya pamoja mgeni rasmi na wajumbe wa bodi iliyomaliza muda wake.

Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile akiwa kwenye picha ya pamoja na bodi mpya ya nane ya baraza la maabara binafsi za afya.
Na. Catherine Sungura –Dodoma

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee wa Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amemuagiza Msajili wa  Baraza la Madaktari la Tanganyika kushirikiana na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania kufuatilia mtoto aliyekatwa mkono baada ya kuhamishiwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutoka hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala.

Dkt. Ndugulile ametoa maagizo hayo wakati akizindua bodi ya nane ya maabara binafsi za afya kwenye ukumbi wa Veta jijini hapa.
“Nilitegemea baraza la madaktari muwe mmeanza uchunguzi, kwahiyo nakupa maagizo kesi hiyo muanze kufuatilia na kama itathibitika ni uzembe waliohusika wachukuliwe hatua, ndani ya wiki mbili mtuletee majibu ili mimi na Mhe. Waziri tujue tunachukua hatua gani.

Dkt. Ndugulile amesema kwenye mabaraza bado kuna changamoto ya baadhi ya mashauri kuchukuliwa hatua hivyo kama mabaraza ya kitaakluma ni vyema kuangalia ufanisi wa majukumu yao na kuchukulia hatua pale taaluma inapokosewa na waliokosea wachukuliwe hatua.

Dkt. Ndugulile ameitaka bodi hiyo kusimamia usajili wa maabara zote nchini kwani hivi sasa imetokea uanzishwaji wa maabara kiholela zinazotoa huduma kwa wananchi bila ya kusajiliwa hivyo kufanya ukaguzi ili kubaini maabara hizo na kuzichukulia hatua.

“Naomba sheria ifuate mkondo wake ili kubaini wale wote walioanzisha huduma za maabara bila kufuata sheria na taratibu za usajili, tushirikiane kuhakikisha kuwa hakuna taasisi au mtu atakayefungua au kutoa huduma za maabara bila kusajiliwa”. Amesisitiza Dkt. Ndugulile.

Aidha, Naibu Waziri huyo amesema baraza hilo ni chombo muhimu na ndio moyo wa sekta ya afya kwani maabara inatoa muelekeo wa mgonjwa kwa kuthibitisha tatizo, hivyo inahitajika maboresho katika utoaji huduma za maabara. 

“Sasa hivi huduma hizi zimekua ni biashara kwani asiliamia 70 ya homa wala sio Malaria ni virusi watu wanakunywa dawa sana pasipo kuzingatia misingi kwani maabara hizi zinatumika kama sehemu ya matibabu na hata upasuaji, mtu anaenda maabara anakaa dakika kumi na tano anaambiwa ana UTI wakati mwingine anaambiwa ana malaria plasi plasi hii maana yake ni nini hili linahitaji ufuatiliaji”. Alisema Dkt. Ndugulile.

Hata hivyo aliitaka bodi hiyo mpya  kusimamia ubora wa huduma za maabara  ili kuinufaisha jamii na kuhakikisha huduma za afya katika jamii zinaboreshwa kukidhi viwango vitavyotarajiwa na hivyo kuboresha afya na maisha ya watanzania.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la maabara binafsi Prof. Said Abood  aliahidi kutekeleza maagizo yote waliyopewa na Naibu waziri ikiwemo ya kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kubaini maabara bubu na  ambazo hazijasajiliwa pamoja na kuhakikisha maabara zinatoa huduma zinazostahili ili kuweza kumsaidia daktari kumpatia mwananchi huduma stahili.

-Mwisho-

Jumatano, 11 Septemba 2019

DKT. NDUGULILE ATAKA MABORESHO YA MIFUMO YA TAKWIMU



Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa kongamano linalohusisha wadau mbalimbali wa masuala ya UKIMWI linaloendelea Jijini Arusha.


Makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Juma Nkamia akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano la wadau mbalimbali wa masuala ya tafiti za ugonjwa wa UKIMWI linaloendelea Jijini Arusha.


Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia moja ya bidhaa zinazotengenezwa na kikundi cha watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI wakati alipotembelea mabanda mbalimbali kabla hajafungua kongamano la wadau wa Masuala ya UKIMWI linaloendelea Jijini Arusha.



Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia moja ya bidhaa zinazotengenezwa na kikundi cha wajasiriamali waliokua wanatumia madawa ya kulevya kabla ya ufunguzi wa kongamano la wadau mbalimbali wanaojihusisha na takwimu za ugonjwa wa UKIMWI linaloendelea jijini Arusha.


Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mbalimbali wanaohudhuria kongamano la wadau wanaohusika na masuala ya tafiti za ugonjwa wa UKIMWI linaloendelea jijini Arusha.

Baadhi ya wajumbe wanaohudhuria kongamano la wadau mbalimbali wanaojihusisha na takwimu za ugonjwa wa UKIMWI linaloendelea jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile (wa tatu kulia) akijadiliana jambo na makamu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na maendeleo ya Jamii Mhe. Juma Nkami (wa kwanza kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa NIMR prof. Yunus Mgaya na wengineo baada ya kumaliza ufunguzi wa kongamano la wadau mbalimbali wanaojihusisha na masuala ya tafiti za UKIMWI nchini linaloendelea jijini Arusha.


Na WAJMW-ARUSHA

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ametaka maboresho ya mifumo ya takwimu za tafiti mbalimbali zinazofanyika nchini.

Dkt. Ndugulile amesema hayo wakati akizindua kongamano linalohusisha wadau mbalimbali wa masuala ya UKIMWI ambao wanawasilisha tafiti na takwimu mbalimbali ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi nchini.

“Tunahitaji tuboreshe mifumo yetu ya takwimu ili tuwe na uwiano wa takwimu ambazo zinawasilishwa katika mkutano huu, hapa nimeona takwimu mbalimbali zimewasilishwa, ninaomba takwimu hizo ziwe za wote kwa sababu tuna wadau wengi wanaoshiriki katika mapambano haya dhidi ya Ugonjwa wa UKIMWI hivyo maelekezo yangu kuwe na mfumo mmoja wa takwimu ambao kila mmoja atakua anachangia takwimu zake na mfumo huo uwe wa mwisho utakaotoa takwimu za wote”. Amesema Dkt. Ndugulile.

Hata hivyo Dkt. Ndugulile amehamashisha makongamano kama hayo yafanyike mara kwa mara ili kuwawezesha wanazuoni, watunga sera na walengwa kukaa pamoja ili kujadiliana mambo mbalimbali ambayo yanahusuana na afua ambazo zinatekelezwa hapa nchini.

Kongamano hilo limeshirikisha taasisi za Serikali ambazo ni NIMR na TACAIDS pamoja na wadau mbalimbali wanaofanya tafiti kuhusiana na ugonjwa wa UKIMWI ambao wamekutana ili kuwasilisha takwimu za tafiti mbalimbali ambazo wanazifanyia kazi katika maeneo yao.