Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 17 Mei 2019

SERIKALI YAIMARISHA UPATIKANAJI WA VIPIMO VYA UGONJWA WA DENGUE





Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Mohammad Bakari Kambi akizungumza jambo kuhusu ugonjwa dengue na waandishi wa habari (hawapo pichani).

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Dkt. Yudas Ndungile akizungumza jambo na waandishi wa habari (hawapo pichani).




Picha ya pamoja Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohhamad Bakari Kambi (meza kuu) akizungumza na waandishi wa habari.


Na WAMJW - DSM


Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeendelea kuimarisha upatikanaji wa vipimo vya ugonjwa wa Degue kwa kununua vipimo 30,000 kwa ajili ya kupima ugonjwa huo.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Mohhamad Bakari Kambi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mapema leo katika ofizi ndogo za Wizara Jijini Dar Es Salaam.

Prof. Kambi amesema kuwa vipimo hivyo tayari vimeshanunuliwa na vitaingia nchini hivi karibuni na kusambazwa kwenye vituo vya umma JIjini Dar Es Salaam pamoja na mikoa mingine yenye athari za ugonjwa huo.

Amesema kuwa ugonjwa wa dengue hauna chanjo wala tiba ya moja kwa moja na kuwataka wananchi kuacha kutoa taarifa za upotoshaji kuhusu tiba za ugonjwa huo.

“Niwakumbushe tena wananchi kinga ni bora kuliko tiba, jikinge na ugonwja huu wewe mwenyewe, kaya na familia yako pamoja na jamii kwa ujumla” amesema Prof. Kambi.

Mganga Mkuu amesema kuwa mpaka sasa vituo vinavyopima ugonjwa wa homa ya Dengue katika Mkoa wa Dar es Salaam ni Muhimbili, Maabara kuu Muhimbili, Amana, Temeke, Mwananyamala, Sinza, Vijibweni, Mnazi mmoja, Lugalo, Mbagala, FFU Ukonga. Katika mkoa wa Tanga; vituo vya Bombo na Horohoro, vituo vingine ni Tumbi Mkuranga, Utete Rufiji na Mafia, Morogoro na Manyara Aidha natambua vipo pia vituo binafsi vinavyotoa huduma za upimaji. Katika mikoa mingine ufuatiliaji unaendelea na hatujapa wagonjwa wenye dalili za Homa ya Dengue.

Aidha Prof. Kambi amesema kuwa Wizara inatambua juhudi zinazofanywa na Mkoa wa Dar Es Salaam na kuwapongeza kwa kazi kubwa wanayofanya ya udhibitiwa ugonjwa huo kupitia zoezi la kunyunyizia dawa viuadudu (Biolarvicides) kwa ajili ya kuangamiza mazalia ya mbu sambamba na elimu ya kujikinga dhidi ya ugonjwa huo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Dkt. Yudas Ndungile Amesema kuwa idadi kubwa ya wagonjwa wanaojitokeza katika vituo vya afya kupata vipimo ni kutokana na wananchi kupata uelewa wa ugonjwa huo baada ya kupatiwa elimu dhidi ya ugonjwa huo.

“Tumepita kwenye maeneo ya kata zenu kufanya ueleimishaji wa namna ya kujikinga na kutambua dalili za ugonjwa huu” amesema Dkt. Ndungile na kuendelea kusema kuwa vyombo vya habari vimetoa mchango mkubwa katika kuelimisha wananchi dhidi ya ugonjwa wa dengue.

Aidha Dkt. Ndungile amesema kuwa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya wameweza kuandaa vituo vya upimaji wa homa ya dengue ambapo huduma za upimaji zinatolewa bure.

Mwisho

0 on: "SERIKALI YAIMARISHA UPATIKANAJI WA VIPIMO VYA UGONJWA WA DENGUE"