Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 18 Februari 2020

WAGANGA WA TIBA ASILI/MBADALA FUATENI SHERIA-DKT. CHAULA


Dkt. Zainab Chaula, Katibu Mkuu Wizara ya AAfya akiongea na waandishi wa habari 

Na.Catherine Sungura, Chato

Waganja  wa Tiba asili na tiba mbadala wote  nchini, wametakiwa kufanya kazi zao kwa kufuata Sheria, kanuni, taratibu zilizowekwa na Serikali .

Hayo yamesemwa juzi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto-Idara kuu afya Dkt. Zainab Chaula alipozungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuzindua kongamano la wajasiriamali lililoandaliwa na Chama cha Wanataaluma Waadventista Tanzania (ATAPE).

Dkt. Chaula alisema hadi sasa Tanzania  hakuna mgonjwa Corona wala dawa iliyothibitishwa kuwa na uwezo wa kutibu ugonjwa huo hapa nchini.

“Tanzania hakuna mgonjwa wa Corona wala dawa iliyothibitishwa kuwa na  uwezo wa kutibu ugonjwa huo, kwa yule ambaye ametangaza kwamba ana dawa, Serikali imechukua hatua".

Aidha, aliwataka waganga wa tiba asili/mbadala wote  wazingatie kufanya kazi zao kwa mujibu wa matakwa ya Serikali, "wizara kupitia kitengo cha tiba asili na tiba mbadala pamoja na msajili wa baraza hilo wametoa sheria na taratibu za kujisajili,lazima wajisajili, lakini wakifanya kazi bila kufuata ile misingi, bila kutii mamlaka iliyopo madarakani, hatutasita kumchukulia hatua yeyote atakayekiuka,” alisisitiza.

Dkt. Chaula aliwahimiza wananchi kuendelea kufuata kanuni za afya na maelekezo yanayotolewa na wataalamu ili kujikinga dhidi ya magonjwa ya mlipuko ambayo yanaendelea kuripotiwa katika maeneo mengine duniani kama vile Ebola na Corona.

Aliwahimiza wazazi kuwakatia watoto  wadogo na wale wanafunzi waliopo sekondari na vyuoni bima ya afya ili waweze kupata huduma za matibabu popote nchini wanapokuwa wagonjwa.

"Nawaona wanafunzi wa sekondari hapa ni vyema mzazi akakata bima ile ya elfu hamsini na mia nne(50,400) ili iweze kuwasaidia kupata matibabu mahali popote na kuwapunguzia mzigo wazazi pindi mtoto anapougua".

Jumatatu, 17 Februari 2020

WATAALAM WA AFYA WATAKIWA KUHUWISHA LESENI ZAO

 Msajili wa Baraza la Famasi Elizabeth Shekhalage akikagua moja ya stoo ya dawa kwenye hospitali

Mfamasia kutoka kitengo cha huduma za dawa, wizara ya afya Daniel Pyuza akikagua moja ya stoo kwenye ziara ya katibu mkuu wa wizara hiyo.



WATAALAM WA AFYA WATAKIWA KUHUWISHA LESENI ZAO

Na. Catherine Sungura-Kasulu

Wataalam wa kada mbalimbali za afya nchini wametakiwa kuhuwisha leseni zao  kila mwaka.

Hayo yamesemwa na msajili wa baraza la wafamasia kutoka wiza ya afya Elizabeth Shekhalage wakati akiongea na watumishi wa hospitali ya halmashauri ya mji kasulu kwenye ziara ya katibu mkuu wa wizara ya afya

Msajili amesema kuwa kwa mujibu wa sheria ya mabaraza ya kitaaluma,kila anayestahili kuwa na leseni ni wajibu wake kuzingatia takwa hilo na hivyo kutimiza kwa mustakabari wa taaluma zao

"Kila mwaka mnatakiwa kutoka kwenye gazeti la serikali,hakikisheni wote mna leseni ili mtimize takwa la kisheria".Alisisitiza Shekhalage.

Kwa upande mwingine  Shekhalage aliwataka watumishi wa afya wenye maduka ya dawa,wawe na maduka ya mfano kwa kusajiliwa  kwani hakuna kifungu kinacho wazuia wasiwe nayo.

Aidha, aliwataka watumishi hao kutoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi holela  ya dawa ambayo husababisha usugu wa vimelea  vya dawa kwa binadamu.

“Matumizi yasiyo sahihi ikiwemo kutumia dawa bila.kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na wataalam au kutotunza dawa vizuri  husababisha  athari  nyingi kwa binadamu ikiwemo kuongezeka kwa ugonjwa ama madhara yasiyo ya lazima kwa wagonjwa".Alisisitiza

Hata hivyo aliwataka wananchi  kuacha kununua dawa bila kwenda kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kupara vipimo na kupata ushauri kutoka kwa wataalam.

-Mwisho-

Jumapili, 16 Februari 2020

WATUMISHI WA AFYA WAASWA KUTOSHIRIKI KWENYE UHALIFU WA KUHARIBU USHAHIDI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisema jambo na watumishi wa afya (hawapo pichani) wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro.

Watumishi wa afya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro wakiwa kwenye kikao na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (hayupo pichani) alipofanya ziara katika Hospitali hiyo.


Na Englibert Kayombo, WAMJW – Moshi Kilimanjaro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaasa watumishi wa afya kutoshiriki kwenye makosa ya uhalifu kwa kuharibu ushahidi wa makosa ya jinai pindi wanapofanya uchunguzi wa kitaalam.

Dkt. Ndugulile ametoa kauli hiyo alipokuwa ziarani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi) akizungumza na watumishi wa afya hospitalini hapo.

“Katika kosa ambalo hatutamsamehe mtumishi wa afya ni kushiriki katika uhalifu wa kuharibu ushahidi, hatutamvumilia mtu ambaye atashiriki kwenye makosa hayo” alisema Dkt. Ndugulile.

Alisema kuwa kesi za ukatili wa kijinsia mara nyingi huwa ni kesi za jinai huku wataalam wa afya wakipewa dhamana ya kuthibitisha ukweli wa matukio hayo na kuwataka kufuata miiko na maadili ya taaluma ya afya.

“Mtu amepata shambulio, daktari unasema kwamba huyu mtu hajashambuliwa, tumeshawahi kufanya hiyo na endapo tukithibitisha pasipo na shaka kwamba wewe mtaalam wetu umeenda kinyume na miiko na maadili ya kazi yako lazima tutakuchukulia hatua” alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Mwisho

Jumamosi, 15 Februari 2020

DKT. NDUGULILE APIGA MARUFUKU MAOMBI YA DAWA KWA NJIA YA KARATASI


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo kwa wataalam (hawapo pichani) katika kikao alichofanya nao mara baada ya ukaguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi)

Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Kilimanjaro (Mawenzi) Dkt. Jummane Karia akisema jambo wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile na wataalam katika Hospitali hiyo


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia) akikagua nyaraka ya dawa iliyoandikwa kwa karatasi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ambapo amepiga marufuku na kuwataka kujaza maombi ya dawa kupitia fomu maalum.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiakikagua nyaraka ambayo imeandikwa kwa usahihi kwenye fomu maalum ya maombi ya dawa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi)


Na Englibert Kayombo, WAMJW – Moshi, Kilimanjaro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amepiga marufuku kwa watumishi wa afya katika vituo vya kutolea huduma za afya kutumia karatasi kama njia ya kuidhinisha maombi ya dawa.
Dkt. Ndugulile ametoa marufuku hiyo maara baada ya kubaini mianya ya upotevu wa dawa za Serikali katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini alipokuwa ziarani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi)
“Ni marufuku kuanzia sasa kutumia karatasi za daftari kuomba dawa kutoka idara moja kwenda nyingine, tuandae fomu maalum za maombi” Amesema Dkt. Ndugulile
Ameagiza kuwa dawa zote zinazopatikana katika vituo vya kutolea huduma ziwekwe kwenye fomu za maombi (reiquizitaion form) huku zikionyesha jina la  aliyeomba pamoja na kusaini kuthibitisha maombi yake ya dawa.
Amesepa pia mtu au idara ya famasi inayopoke maombi hsyo anatakiwa  kuhakikisha maombi hayo na kusaini fomu hiyo.
“Ni marufuku kwa mtu wa famasi kujiongezea dawa kwa maneno ya mdomo au kuambiana, na atakayepokea dawa hizo pia anatakiwa aandike jina lake na kusaini.
Hatua hiyo inakuja mara baada kubaini mianya ya upotevu wa dawa za Serikali ambapo Dkt. Ndugulile amesema “Serikali imewekeza nguvu kubwa sana katika upande wa dawa, lakini pia nyie wataalam ambao mnasimamia mnatakiwa kuhakikisha mnaweka kumbukumbu zenu sahihi ili kudhibiti mianya ya upotevu wa dawa”
“Hapa nnapata mashaka kuwa kuna uptevu wa dawa za Serikali tujirekebishe na kuhakikisha tunatunza vzuri kumbukumbu zetu” Amesema Dk. Ndugulile na kuwataka kuhakikisha wanaweka mifumo ya TEHAMA katika kusimamia maombi ya dawa. 
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi) Dkt. Jumanne Karia amesema wamepokea maelekezo hayo na kuahidi kuyatekeleza mara moja.
“Tunashuruku kwa maelekezo yako, tutaendelea kuunga mkono Wizara ya Afya na tutatekeleza maelekezo uliyoagiza” Amesema Dkt. Karia.

Ijumaa, 14 Februari 2020

MAAFISA AFYA WATAKIWA KUIMARISHA UKAGUZI KWENYE MIPAKA

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto-Idara Kuu Afya Dkt. Zainab Chaula akiwa kwenye jengo la mpaka wa nchi ya Uganda ikiwa ni ziara yake ya kikazi ya kuangalia utayari wa kukabiliana na magonjwa ya milipuko.

 Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula akiongea na watumishi wa idara mbalimbali wa mpaka wa mtukula nje ya jengo la kituo cha pamoja nchini Tanzania.





Dkt. Chaula akiangalia ofisi ya maofisa afya wa mpaka wa mtukula nchini Tanzania na kujionea jinsi wanavyotoa huduma ikiwemo ya kudhibiti magonjwa ya milipuko na utoaji wa chanjo ya homa ya manjano(Yellow Fever).


MAAFISA AFYA WATAKIWA KUIMARISHA UKAGUZI KWENYE MIPAKA

Na. Catherine Sungura-Kagera

Maofisa afya wanaofanya kazi kwenye mipaka nchini  wametakiwa kuongeza umakini  wa  kufanya ukaguzi katika mipaka.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto-Idara kuu Afya Dkt. Zainab Chaula wakati alipotembelea mpaka wa Mutukula nchina Tanzania na Uganda ikiwa ni moja ya ziara yake ya kuangalia utayari wa kukabiliana na magonjwa ya milipuko ambayo inafanywa na wizara ya afya kwa kushirikiana na TAMISEMI.

"Umakini mkubwa unatakiwa katika kufanya ukaguzi kwa wasafiri wanaopita kwenye.mpaka huu ingawa kuna mwiingiliano mkubwa baina ya nchi hizi mbili ili kuweza kuzuia magonjwa ya mlipuka kama Ebola usiingie nchini.

"Kujilinda ni jambo moja na kuzuia ni jambo lingine,nimetembelea mpaka huu, nimejionea na maofisa wetu wa Tanzania wa afya, forodha, uhamiaji wamenieleza changamoto iliyopo hapa ni mwingiliano mkubwa, watu wanatoka upande mmoja kwenda mwingine kwa wingi, wanashirikiana kwenye shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi,hivyo lazima muangalie tunatoka vipi kwenye hili.

Hata hivyo Dkt. Chaula aliwapongeza watumishi wote wa idara zote kwa ushirikiano na kwa kazi kubwa waliyoifanya  katika kudhibiti magonjwa ya milipuko hayajaingia  nchini.

"Lakini pamoja na hayo, bado inahitajika muwe imara zaidi, ndiyo maana tumeleta vifaa tiba  vya kisasa vya ukaguzi wa joto la afya ya mwili, nawasihi msimamie hili kwa umakini zaidi," alisema.

Aidha, Dk. Chaula alisisitiza maofisa afya hao kuongeza elimu.ya afya kwa umma kwa wananchi wote wanaopita mpakani hapo ili kuwajengea uelewa  jinsi ya kujikinga na dalili  za magonjwa hayo

"Wataalamu wa afya wa Mkoa na viongozi wote pamoja hakikisheni elimu ya afya kwa umma  inafika hadi kule vijijini, watu wetu waelewe jinsi ya kujikinga," alisema Dk. Chaula.

MWISHO

“TANZANIA NI SALAMA HAKUNA UGONJWA WA CORONA” - DKT. NDUGULILE

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, jisnai, Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Waandishi wa Habari (Hawapo kwenye picha) wakati wa ziara yake Jijini Arusha,



“TANZANIA NI SALAMA HAKUNA UGONJWA WA CORONA” -  DKT. NDUGULILE

Na Englibert Kayombo, WAMJW, Arusha.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewahakikisha Watanzania kuwa nchi bado iko salama na hakuna mgonwjwa yeyote mwenye ugonjwa wa Virusi vya Corona.

Dkt. Ndugulile ametoa kauli hiyo akiwa Jijini arusha katika Ziara zake za kikazi ambapo waandishi wa habari walimuuliza juu ya tetesi za uwepo wa ugonjwa huo nchini, pamoja na kutaka kufahamu ukweli wa taarifa za mtu anayedai kuwa na dawa za ugonjwa huo.

“Niseme tuu kuwa Tanzania mpaka sasa hivi bado tuko salama na hakuna mgonjwa yeyoteambaye ameripotiwa na amethibitika kuwa na ugonjwa” amesema Dkt Ndugulile.

Amesema kuwa Serikali imekuwa ikifuatilia taarifa mbalimbali za washukiwa na watu wote ambao tunawahisi kuwa na ugonjwa huo na tumeweza kuwapima na kubaini kuwa hawana ugonjwa.

“Sambamba na hilo tumeendelea kuchukua tahadhari mbalimbali na mimi niko katika Mkoa huu wa Arusha na nitaenda Kilimanjaro kwenda kuangalia utayari” amesmea Dkt. Ndugulile na kuendelea kusema “ Nimepita hapa leo nimeongea na uongozi na nimeridhika na maandalizi ambayo tunayo hapa katika Mkoa huu wa Arusha katika kudhibiti ugonjwa huo” Ameeleza Dkt. Ndugulile.

Akijibu kuhusu mtu ambaye anasema kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa huo ambaye anajulikana kwa jina la Mosses Mollel maarufu kwa jina la “Nabii namba saba” aliyetoa taarifa za kuwa na dawa yenye uwezo wa kutibu virusi vya corona, Dkt Ndugulile amesema kuwa anazo taarifa za mtu huyo ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari akijitangaza kuwa anayodawa ya kutibu ugonjwa huo na kumtaka athibitishe kauli yake.

“Kimsingi nimeiona hiyo taarifa ya huyo mtu  anayejiita Nabii Saba kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa wa Corona ,ila hapa kwetu Tanzania hatuna maambukizi yoyote ya ugonjwa huyo ,tunachotaka huyo mtu  atuthibitishie uwezo wake wa kutibu huo ugonjwa wa Corona” Amesema Ndugulile

Ameongeza kuwa iwapo atashindwa kuthibitisha atachukuliwa hatua Kali za kisheria.
Amesema hadi sasa Serikali imetuma wataalamu wake kwenda kumsaka na kumhoji kama anavyo vibali Vya kutoa huduma ya Tiba na kujitangaza kuwa anatoa Huduma ya kutibu ugonjwa huo  hatari ambao hadi sasa mataifa bado yanahaha kusaka  Tiba ya ugonjwa huo.

Nabii Namba Saba ambaye ni mkazi wa Ngaramtoni Wilayani Arumeru,Mkoani Arusha amekuwa akijitangaza kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa huo wa virusi vya corona na kuweka mawasiliano yake  kwenye mitandao .

Dkt. Ndugulile amesema kuwa mtu yeyote anayetoa tiba asili na mbadala kwanza ni lazima asajiliwe na mamlaka husika ambayo ni Wizara ya Afya, pili lazima dawa zake ziwe zimesajiliwa na Wizara ya Afya na kusisitiza kuwa nabii huyo pia anapaswa kuthibitisha amesajiliwa wapi na lini.

“Tuepuke kutoa kauli ambazo zinakwenda kuchanganya jamii, na endapo tutabaini mtu huyu hana sifa ambazo anasema kuwa nazo tutamchukulia hatua za kisheria” Amesema Dkt. Ndugulile.