Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 9 Septemba 2019

BILION 30 ZATOLEWA KILA MWAKA KWAAJILI YA HUDUMA ZA CHANJO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikabidhi funguo ya gari kwa Mganga Mkuu wa Dar es Salaam Dkt. Yudas Ndungile Katika shughuli ya ugawaji wa magari kwa Halmashauri 61 nchini, shughuli iliofanyika katika ofisi za mpango wa chanjo taifa Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwasha gari ishara ya uzinduzi wa magari hayo yaliyotolewa na Serikali kwa Halmashauri 61 ili kurahisisha shughuli za chanjo nchini.
 

Baadhi ya magari ya yatayosaidia shughuli za chanjo yaliyoyolewa na Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa halmashauri 61 nchini, shughuli imefanyika katika ofisi za mpango wa chanjo wa taifa Jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikagua moja kati ya majokofu ya kuhifadhia chanjo, ameambatana na Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya Dkt Leonard Subi (wakatikati) na Meneja wa mpango wa taifa wa Chanjo Dafrosa Lyimo (wakwanza kushoto) wakati wa kukabidhi magari ya chanjo kwa Halmashauri 61 nchini.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati  wa mkutano na Waandishi wa habari wakati wa kukabidhi  magari ya  chanjo kwa Halmashauri 61 ili kurahisisha shugchanjo nchini.


Baadhi ya Waandishi wa Habari na baadhi ya Waganga Wakuu wa Wilaya waliojitokeza katika shughuli ya ugawaji wa magari ya chanjo kwa Halmashauri 61 nchini uliofanywa leo na Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu




BILION 30 ZATOLEWA KILA MWAKA KWAAJILI YA HUDUMA ZA CHANJO

Na WAMJW-DSM

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto yatoa kiasi cha shilingi Bilion 30 kila mwaka kwaajili ya huduma za Chanjo ili kuwakinga wananchi dhidi ya magonjwa mbali mbali.

Hayo yamesemwa na waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo wakati akikabidhi magari 71 ya chanjo kwaajili ya Halmashauri 61, na magari 10 kwaajili ya Mpango wa chanjo nchini ikiwa ni sehemu ya kuimarisha huduma za chanjo kwa Wananchi.

Waziri Ummy amesema kuwa, Serikali imetoa magari hayo ili kurahisisha shughuli za chanjo katika maeneo mbali mbali hivyo, ameagiza magari hayo yakafanye kazi kulingana na madhumuni yaliyokusudiwa.

Waziri Ummy aliendelea kusema, Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa Halmashauri zote zilizobaki zinapata magari ya chanjo ili kurahisisha utendaji kazi katika maeneo yote nchini.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy amesema kuwa, Serikali imetoa na kusambaza majokofu zaidi ya 1300 yanayotumia umeme wa sola katika Halmashauri zote nchini, jambo lililosaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa majokofu hayo.

 “Nafurahi kwamba tumeweza kugawa majokofu Zaidi ya 1300 yanayotumia umeme wa sola, lakini uzuri wa majokofu hayo ambayo tumeyasambaza mwaka huu, yanatumia umeme wa sola, hivyo kupunguza gharama za uendeshaji majokofu ambayo kwa mwezi yaligharimu kiasi cha shilingi Elfu 50 kwaajili ya mtungi wa gesi” Alisema Waziri Ummy.

Mbali na hayo, Waziri Ummy ametoa wito kwa wazazi na walezi wote nchini kuhakikisha wanawapeleka Watoto katika vituo vya kutolea huduma za Afya kupata chanjo ili kuwakinga dhidi ya magonjwa ya surau na lubena.

“Tumeona mafanikio mazuri katika kuwekeza kwenye chanjo, ikiwemo kupunguza vifo vya Watoto wenye umri chini ya miaka mitano, kwa mfano mwaka 2005 tulikuwa na vifo 112 katika kila vizazi hai 1000, laini sasahivi takwimu rasmi zinaonesha vifo 67” Alisema Waziri Ummy

Hata hivyo, Waziri Ummy amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya wote nchini kuhakikisha wanawafikia Watoto wote nchini walio na umri wa chini ya miaka mitano, kuwapa huduma za chanjo ili kuwakinga dhidi ya magonjwa.

“Katika kila Watoto 100 ambao wanatakiwa kufikiwa kupatiwa chanjo, tumewafikia Watoto 98, kimataifa ni Zambia na Rwanda ndio waliotuzidi, lakini lengo letu ni kuwafikia hata hao Watoto wawili waliobaki” Alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy Amesisitiza Serikali itaendelea kuwekeza katika masuala ya chanjo kwani zipo shahidi ya kisayansi ambazo zinaeleza kwa kuwekeza kila dola moja huokoa kiasi cha dola 16.
“Kila mwaka serikali inatupa angalau sh. bilioni 30 kwa kuwekeza katika chanjo tumeweza kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka mitano kutoka vifo 112 katika kila vizazi hai 1000 hadi kufikia vifo 67 kwa kila vizazi hai 1000 hivi sasa,” amesema.

Amesema Tanzania kupitia jitihada ilizofanya sasa hivi katika kila watoto 100 ambao wanatakiwa kupatiwa chanjo, watoto 98 wanafikiwa. “Ni watoto wawili ambao tunawakosa...Barani Afrika, Tanzania ni nchi ya tatu, tumezidiwa na Rwanda ambayo imewafikia zaidi ya asilimia 99 na Zambia tupo nao sawa kwa asilimia 98,” amesema.

Ameongeza “Lengo letu japo tupo namba tatu kwanini tunawakosa hawa wawili katika 100 ambao wanatakiwa kupata huduma za chanjo.

Kwa upande wake Meneja Mpango wa Taifa wa Chanjo, Dk. Dafrosa Lyimo amesema ni jukumu la Serikali kuhakikisha chanjo zipo na zinapatikana kwa wakati.

“Hadi sasa hatuna upungufu wa chanjo, hatua hii (kukabidhi magari) ni muhimu sana, katika utunzaji wa chanjo tunahakikisha kuna utunzaji kuanzia ngazi ya Taifa na tunahakikisha zinasafirishwa katika mnyororo baridi na zinatunzwa vizuri,” alisema.

Mwisho

0 on: "BILION 30 ZATOLEWA KILA MWAKA KWAAJILI YA HUDUMA ZA CHANJO "