Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 5 Juni 2020

EWURA NA MOUNT MERU ZATOA MSAADA KWA AJILI YA UDHIBITI WA CORONA NCHINI





Na Emmanuel Malegi-Dodoma

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa leo amepokea msaada wa hundi ya kiasi cha Tsh. Milioni 100 kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA)uliokabidhiwa na Kaimu Mkurugenzi Bw. Godfrey Chibulunje akiwa na Meneja Mawasiliano na uhusiano wa mamlaka hiyo Bw. Titus Kaguo.

Aidha, Waziri Ummy amepokea msaada wa ndoo 480 sawa na Lita 9600 za vitakasa mikono (Hand Sanitizer) zenye thamani ya Tsh. Milioni 11 zilizotolewa na kampuni ya Mafuta ya Mount Meru ambazo zitatumika katika kudhibiti ugonjwa wa Corona nchini. Vitakasa mikono hivyo vimekabidhiwa na Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Bw. Prabhat Yadau.

Katika makabidhiano hayo yaliyofanyika katika ofisi ya Waziri Mkuu Mlimwa jijini Dodoma, Waziri Ummy kwa niaba ya Waziri Mkuu ameshukuru kupata misaada hiyo ambayo itasaidia katika kudhibiti ugonjwa wa Corona nchini na pia amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari licha ya maambukizi ya ugonjwa huo kupungua nchini.

0 on: "EWURA NA MOUNT MERU ZATOA MSAADA KWA AJILI YA UDHIBITI WA CORONA NCHINI"