Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 12 Juni 2020

WITO WATOLEWA WANANCHI KUENDELEA KIJIKINGA NA CORONA ILI PIA KUJIKINGA NA MAGONJWA MENGINE.




 
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (kushoto) akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma kupata huduma ambapo amezungumza nao kuendelae kujilinda na ugonjwa wa corona kwa mbinu zinatotolewa na Wizara ya Afya ikiwemo tiba asili ya kujifukiza. 


 
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi (kulia) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika wakielekea kwenye kituo kilichotengwa kuhudumia wagonjwa wa corona  ambacho hakina mgonjwa yeyote.

 

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi akizunguma na watumishi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa alipotembelea hospitlai hiyo, Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika.




WITO WATOLEWA WANANCHI KUENDELEA KIJIKINGA NA CORONA ILI PIA KUJIKINGA NA MAGONJWA MENGINE.

Na WAMJW-DOM

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi ametoa wito kwa wananchi kuendelea kujikinga dhidi ya ugonjwa wa corona na kudhibiti magonjwa mengineyo ya kuambukiza.

Prof. Makubi ametoa wito huo leo alipofanya ziara ya kuona hali ya utoaji huduma katika Hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo Jijini Dodoma.

“Katika kudhibiti ugonjwa wa corona wananchi walipokea kwa mikono miwili mbinu za kuepuka kuambukizwa ugonjwa wa corona ikiwemo unawaji mikono kwa maji yanayotirika na sabuni, uvaaji wa barakoa, kuepuka mikusanyiko na misongamano pamoja na mbinu za tiba asilia/tiba mbadala ili kutibu ugonjwa wa corona”. Amesema Prof. Makubi

Pamoja na kupungua kwa ugonjwa wa corona nchini, Prof. Makubi amesema kuwa bado Watanzania tunatakiwa kuendelea kuchukua tahadhari za kinga ili hatimae tuweze kutokomeza kabisa ugonjwa wa corona au pale ambapo bado utaendelea kuwepo tuweze kuishi nao bila madhara makubwa.

Prof Makubi amesema kuwa Serikali inawapongeza wananchi kwa kuipokea na kutumia njia zote zilizotelewa kukabiliana na ugonjwa wa corona pamoja na magonjwa mengine ya kuambukiza na kuwataka wananchi kuendelea na mbinu walizoelimishwa kujikinga na magonjwa ya kuambukiza.

“Mwamko tulio nao sasa hivi wananchi juu ya mbinu hizi tusiziache, tukiendelea nazo zitatusaidia kujikinga na magonjwa mengine” amesisitiza Prof. Makubi.

Hatukuwa na utamaduni wa kunawa mikono mara kwa mara, lakini tuelewe pia usafi wa mikono unatusaidia pia kupunguza hatari ya kupata magonjwa mengine yanayotokana na uchafu yakiwemo magonjwa ya kuhara, au hata kipindupindu.
Prof. Abel Makubi amesema kuwa kufanya mazoezi ya mwili na kula lishe bora yanasaidia pia kujenga afya ya mwili uimara na pia kujikinga na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama shinikizo la damu, kisukari na moyo.
Ni vema wanachi wakaendelea na utamaduni huu huku wakiendelea kupata lishe bora aili kujenga kinga zao dhidi ya mgonjwa mengine” Amesisitiza Prof. Makubi
Kuhusu mbinu ya tibaasili, Prof. Makubi amewapongeza wananchi kwa kuipokea na kuikubali mbinu hiyo katika kusaidia kutibu ugonjwa wa corona na kutumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzana Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuelekeza bajeti ya tiba asili/mbadala na tafiti za dawa asilia iweze kuongezwa ili kuwawezesha wataalam wanaotengeneza dawa hizo zinazosaidia kutibu magonjwa mbalimbali na kupambana na maambukizi ya virusi vya corona nchini.

Aidha Prof Makubi amewaagiza wataalam wa afya hasa Wakurugenzi, Waganga wa Mikoa, Wilaya, Maafisa wa afya ngazi za jamii, viongozi wa mashule, vyuo, michezo, na mamlaka za mitaa kuendelea kutoa elimu ya kupambana ugonjwa wa corona na kuendelea kuhamasisha mbinu za kuthibiti CORONA ambazo  zikiendelezwa zitapunguza uwezekano wa kuibuka magonjwa mengine hivyo kuokoa afya za wanachi na fedha nyingi ambazo zingetumika  kutibu wagonjwa.

Mwisho.

0 on: "WITO WATOLEWA WANANCHI KUENDELEA KIJIKINGA NA CORONA ILI PIA KUJIKINGA NA MAGONJWA MENGINE."