Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 24 Aprili 2019

WAZIRI UMMY ALIPONGEZA JIJI LA DODOMA KWA JITIHADA ZA KUTOKOMEZA MALARIA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamoi, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akimuangalia mtoto aliyeletwa kliniki ya kituo cha Afya cha Makole kilichopo Jijini Dodoma kwa ajili ya kupata chanjo wakati alipotembelea kituo hicho kwa ajili ya kugawa vyandarua vyenye dawa.

Waziri Ummy Mwalimu akimpongeza baba aliyeleta mtoto kliniki kwa ajili ya kupata chanjo wakati alipofika katika kituo cha afya cha Makole Jijini Dodoma kwa ajili ya zoezi la kutoa vyandarua vyenye dawa kwa akinamama wajawazito na watoto walio chini ya mwaka mmoja.

Waziri Ummy Mwalimu akimpongeza baba aliyeleta mtoto kliniki kwa ajili ya kupata chanjo wakati alipofika katika kituo cha afya cha Makole Jijini Dodoma kwa ajili ya zoezi la kutoa vyandarua vyenye dawa kwa akinamama wajawazito na watoto walio chini ya mwaka mmoja.



Picha mbalimbali zikimuonesha Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akigawa vyandarua vyenye dawa kwa akinamama wajawazito, wakina baba na wakina mama walioleta watoto kliniki na katika kituo cha afya cha Makole Jijini Dodoma.

Waziri Ummy akiwa na baadhi ya akinamama waliopewa vyandarua baada ya kufika kliniki katika kituo cha afya cha Makole Jijini Dodoma wakati Waziri alipofika na kugawa vyandarua hivyo.


Na WAMJW-Dodoma

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amelipongeza Jiji la Dodoma kwa jitihada kubwa zilizofanyika kwa ajili ya kutokomeza ugonjwa wa Malaria.

Waziri Ummy ametoa pongezi hizo wakati alipokua anagawa vyandarua vyenye dawa kwa akinamama wajawazito na wenye watoto wadogo katika Kituo cha Afya cha Makole Jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema Jiji la Dodoma limetokomeza Malaria kutoka Asilimia 1 mpaka asilimia 0.6 ikiwa mafanikio makubwa, ambapo amesema katika kipindi cha miaka mitatu nchi nzima ugonjwa wa Malaria umeweza kupungua kutoka asilimia 14 mwaka 2015 mpaka asilimia 7 mwaka 2018.

“Toka Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli iingie madarakani tumeweza kutekeleza mikakati mbalimbali ya kutokomeza Malaria nchini, katika kipindi kifupi cha miaka mitatu tumeweza kupunguza Malaria zaidi ya asilimia 50 kutoka asilimia 14 mwaka mwaka 2015 mpaka asilimia 7 mwaka 2018”. Amesema Waziri Ummy.

Pamoja na hayo, Waziri Ummy amewataka wananchi kwa ujumla kutimiza wajibu wao ili kutokomeza Malaria kama kauli mbiu ya mwaka huu inavyosema “Ziro Malaria inaanza na mimi”, hivyo amewataka wakina mama wajawazito kuhudhuria kliniki kwa ajili ya uchunguzi wa afya zao na kufanyiwa vipimo vyote kikiwemo kipimo cha Malaria.

Waziri Ummy amebainisha kuwa Tanzania bado haijafanya vizuri katika takwimu za akina mama wajawazito kuhudhuria kliniki ambapo katika akinamama wajawazito 100 ni akinamama 29 ndiyo wanaohudhuria kiliniki mara nne katika kipindi cha ujauzito.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mratibu wa Malaria wa mkoa, Dkt. Francis Bujiku amesema mafanikio ya kutokomeza Malaria katika jiji la Dodoma yamekuja baada ya utekelezaji wa afua mbalimbali za Malaria ikiwa ni pamoja na kuhakikisha tiba sahihi za Malaria zinatolewa katika vituo vyote vya afya, elimu ya kujikinga na ugonjwa huo, pamoja na mkoa kufanikiwa kuangamiza viluilui wa mbu kwa kunyunyizia dawa kwenye mazalia yao.

Dkt. Bujiku amesema mwaka 2015 mkoa uliendesha zoezi la ugawaji vyandarua vyenye dawa kwenye ngazi ya kaya, takribani vyandarua milioni moja na laki tano viligawiwa kwa wananchi, vile vile akina mama wajawazito waliofika kliniki kwenye hudhurio la kwanza la ujauzito na watoto chini ya mwaka mmoja waliofika kupata chanjo ya surua walipewa vyandarua hivyo.

MWISHO



0 on: "WAZIRI UMMY ALIPONGEZA JIJI LA DODOMA KWA JITIHADA ZA KUTOKOMEZA MALARIA"