Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 1 Novemba 2019

ELIMU YA TATHMINI YA UHAKIKI UBORA WA HUDUMA ZA AFYA YAZIDI KUTOLEWA











Na WAMJW-DSM


Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeendelea kutoa mafunzo kwa timu za Usimamizi wa uendeshaji wa huduma za afya katika Halmashauri (CHMTs) juu ya tathmini ya uhakiki wa ubora wa huduma za zinazotolewa katika eneo husika.

Mafunzo hayo yaliyofunguliwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Dkt. Yudas Ndugile siku ya Jumanne yameendelea kwa wiki moja lengo likiwa ni kuwaelimisha watoa huduma za afya kuzingatia misingi ya utoaji wa huduma bora za afya ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miundombinu.

Akiongelea mafunzo hayo Mratibu na mkufunzI kutoka Wizara ya Afya Dkt. Talhiya Yahya amesema  Lengo la kutoa nyota ni kuongeza chachu ya utoaji wa huduma za afya nchini ikiwa sambamba na uboreshaji wa miundombinu na watumishi wa afya kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa mahala pa kazi.

“Lengo la mafunzo haya ni kutoa elimu kwa CHMT kuhusu kutumia nyezo ya kielektroniki kufuatilia utekelezaji wa mipango ya uboreshaji wa vituo kutegemea na mapungufu yaliyopatikana katika vituo kipindi cha kufanya tathmini ya kutoa nyota kutokana na ubora wa kituo”. Amesema Dkt. Talhiya.

Dkt. amesema baada ya mafunzo  hayo anategemea kuona maboresho yakifanyika na tathmini ijayo ya kuhakiki ubora (Star Rating) vituo vingi vitakua na nyota tatu au zaidi.

Wakati huo huo, Wizara imetoa mafunzo kwa watumishi wa afya wa Hospitali mbalimbali za Jiji la Dar Es Salaam namna ya kufuata miongozo na taratibu za kukinga na kudhibiti maambukizi (IPC Standards).

Mafunzo hayo ya siku tano yamehitimishwa leo katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam tawi la Kijitonyama ambapo mratibu wa mafunzo hayo Dkt. Chrisogone German amesema lengo ni kuwajengea uwezo watumishi hao kufuata miongozo ya utoaji wa huduma katika maeneo yao ya kazi.

Dkt. Chrisogone amesema muongozo wa mpya wa kukinga na kudhibiti maambukizi (IPC Guideline) wa mwaka 2018 ambao umefuata vigezo vya Shirika la afya Duniani (WHO) utaanza kutekelezwa katika vituo vya kutolea huduma za afya katika mkoa wa Dar Es Salaam ikiwemo washiriki kujengewa uwezo wa utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.
Mafunzo hayo yamejumuisha washiriki kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila, Agha Khan, TMJ, Sali International, Hindu Mandal, BOCHI na Rabininsia.




0 on: "ELIMU YA TATHMINI YA UHAKIKI UBORA WA HUDUMA ZA AFYA YAZIDI KUTOLEWA"