Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 12 Februari 2018

TANZANIA INATUMIA DAWA ZILIZO SALAMA KWA UHAKIKA MKUBWA

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akiongea wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Mamlaka za Kudhibiti Chakula na Dawa Barani Afrika unaofanyika Jijini Dae Es Salaam na kuhudhuliwa nan chi zipatazo 17 za Afrika.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kuifungua mkutano huo.
Pichani Naibu Waziri Dkt.Ndugulile akiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) Bi.Agnes Kijo kwenye mkutano huo utakaofanyika kwa siku tano na kujadili mfumo wa pamoja wa kudhibiti ubora wa dawa barani Afrika.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akifuatilia mada (mwasilishaji hayupo pichani) katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi.Agnes Kijo akiongea kwenye ufunguzi wa mkutano wa  wa Mamlaka za Kudhibiti Chakula na Dawa Barani Afrik.
Msimamizi wa kitengo cha Afya katika Shirika la Maendeleo ya Afrika (NEPAD) yenye makao makuu yake nchini Afrika ya Kusini Bi.Margareth Ndomondo akiongea wakati wa uzinduzi huo.Shirika hilo katika afya linasaidia kupunguza magonjwa yanayoikabili nchi za Afrika.(Picha zote na Wizara ya Afya)

Na.WAMJW-DAR ES SALAAM
TANZANIA ni miongoni mwa nchi inayotumia dawa zilizo salama na ubora wa hali ya juu barani Afrika kutokana na udhibiti na umakini unaofanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini TFDA.
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mamlaka wa Udhibiti  na ubora wa dawa barani afrika unaofanyika jijini Dar es Salaam.
”Sisi kama Tanzania tunafanya vizuri sana katika udhibiti wa madawa yanayoingia,nataka niwathibitishie  kwamba Tanzania dawa zetu tunazozitumia ni salama na zipo salama kwa uhakika mkubwa” alisema Dkt. Ndugulile

Aidha ,Dkt. Ndugulile alisema kuwa ongezeko la matumizi ya dawa ambayo hayana kiwango na kutumika katika mfumo wa tiba umeleta changamoto katika kuongeza gharama za matibabu nchini na barani Afrika
Kwa mujibu wa Dkt. Ndugulile amesema changamoto hizo zinasababisha wagonjwa wengi kukaa hospitalini,kuongeza gharama, kuathiri matokeo ya mgonjwa na hatimaye vifo pamoja na kuleta usugu wa dawa kwa kutumia dawa zisizo na kiwango
Hata hivyo Dkt. Ndugulile alisema mkutano huo utajenga utaratibu na mfumo  wa pamoja wa kuona ni jinsi gani wanaweza kudhibiti matumizi ya madawa yasiyo na kiwango barani afrika.
 “Nataka niwathibitishie Watanzania kwamba tuna dawa za kutosha na dawa zote  zinazoingia zina ubora unaotakiwa,Taasisi yetu ya TFDA inatambulika Kimataifa, ina viwango vya Kimataifa na tumeboresha maabara zetu kuwa za kisasa na kutumika katika bara la afrika  katika udhibiti wa madawa”. Alisema Dkt. Ndugulile.
Naye kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA Bi.Agnes Kijo alisema mamalaka hiyo imejidhatiti katika masuala ya udhibiti wa dawa hivyo kupelekea mkutano huo kufanyika Tanzania
“Maabara yetu hivi sasa imewekewa vifaa vya kisasa ambapo mwaka huu wa fedha ilitengewa shilingi  bilioni tano nukta moja kwa ajili ya ununuzi wa vifaa kwa ajili ya maabara ya Dar es Salaam na  kanda ya ziwa ambapo itasaidia kufanyiwa uchunguzi wa dawa katika ukanda uliopo na hivyo kutoa majibu kwa wakati na mamlaka kufanya maamuzi sahihi” alisema Bi. Kijo.
Mkutano huo ambao una lengo la kubadilishana uzoefu wa  masuala mbalimbali yanayo uhusiana na udhibiti na ubora wa dawa ambapo kumekuwa na changamoto za matatizo ya madawa yasiyo na kiwango umekutanisha nchi zipatazo  17 na utafanyika kwa siku tano.

TUMEKOSOGEZA KARIBU


Wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto.

Inayo furaha kubwa kuwakaribisha wananchi wote ndani na nje ya nchi kutembelea katika mitandao yake ya kijamii ili kupata taarifa mbalimbali za kiafya. Aidha tunakaribisha maoni na ushauri mbalimbali kuhusu sekta ya afya. "Jenga taifa lenye afya bora kwa uchumi imara"
#AFYA_YANGU_MTAJI_WANGU

Jumatano, 7 Februari 2018

SERIKALI YAAZIMIA KUKUSANYA TAKWIMU ZA AFYA KIELEKTRONIKI NCHI NZIMA.





SERIKALI  imeazimia kukusanya na kutumia takwimu kwa njia ya kielektroniki nchi nzima ili kuweza kumudu na kutoa huduma za afya kwa ubora zaidi nchini.
Hayo yamezungumzwa na Katibu Mkuu Wizara ya afya Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa kutia Sahihi ya makubaliano ya kuanzisha mfumo wa ukusanyaji takwimu za afya utakaotekelezwa na Wizara ya afya,Wadau wa Maendeleo,Asasi za Kiraia na Shirika la Afya Duniani (WHO) uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
“Takwimu ni muhimu sana amabazo zitazomuwezesha mtoa huduma kujua mgonjwa historia yake ya ugonjwa  na matibabu aliyopewa awali,kuwapa Uwezo utumishi kujua tunahitaji rasilimali watu kwa kiasi gani  katika kituo cha Afya” alisema Dkt. Ulisubsya.

SERIKALI YAAZIMIA KUKUSANYA TAKWIMU ZA AFYA KIELEKTRONIKI NCHI NZIMA.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa taarifa mbele ya Wadau wa Sekta ya Afya wakati wa Kikao cha kusaini makubaliano ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu takwimu wa kielektroniki kilichofanyika mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam.

Wadau wa Sekta ya Afya wakifuatilia kwa makini  taarifa ya mgeni rasmi (Hayupo kwenye picha) ambae ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa Kikao cha kusaini makubaliano ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu takwimu wa kielektroniki.

Mwinyekiti wa DPG HEALTH Mhe. Norzin Grigoleit-Dagyab akitutubia mbele ya Wadau wa Sekta ya Afya na Watumishi wa Serikali wa Idara kuu ya Afya wakati wa Kikao cha kusaini makubaliano ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu takwimu wa kielektroniki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya na wa mwisho kulia ni Mwakilishi kutoka WHO Dkt. Matthieu Kamwa.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiwa na Wadau mbali mbali wa Sekta ya Afya katika Kikao cha kusaini makubaliano ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu wa kielektroniki kilichofanyika mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam.

Picha ya Pamoja ya Viongozi wa Sekta ya Afya wakiwa wameshika mikataba iliyosainiwa ya makubaliano ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu wa kielektroniki ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya.


Na WAMJW-DAR ES SALAAM.
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imeazimia kukusanya na kutumia takwimu kwa njia ya kielektroniki nchi nzima ili kuweza kumudu na kutoa huduma za afya kwa ubora zaidi nchini.
Hayo yamezungumzwa na Katibu Mkuu Wizara ya afya Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa kutia Sahihi ya makubaliano ya kuanzisha mfumo wa ukusanyaji takwimu za afya utakaotekelezwa na Wizara ya afya,Wadau wa Maendeleo,Asasi za Kiraia na Shirika la Afya Duniani (WHO) uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
“Takwimu ni muhimu sana amabazo zitazomuwezesha mtoa huduma kujua mgonjwa historia yake ya ugonjwa  na matibabu aliyopewa awali,kuwapa Uwezo utumishi kujua tunahitaji rasilimali watu kwa kiasi gani  katika kituo cha Afya” alisema Dkt. Ulisubsya.
Aidha, Dkt. Ulisubisya amesema kuwa kwa kuanzia zoezi hilo litaanza kwenye mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Manyara hatimaye kufikia nchi nzima mpaka kufika 2020 ili kuweza kuwa  na takwimu za afya.
Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mfumo wa kujaza takwimu kwenye makaratasi umepitwa na wakati kwani kadri makaratasi ya takwimu yanapokuwa mengi na makosa ya utoaji huduma unaweza kutokea  kwani mpaka uanze kutafuta takwimu zilizopita inachukua muda mrefu tofauti na kuhifadhi takwimu kielektroniki.
Mbali na hayo Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mpaka hivi sasa hali ya utoaji wa chanjo imefikia asilimia 97 na lengo letu ni kufikia asilimia 100 kupitia mfumo huu wa kukusanya takwimu kwa njia ya kielektroniki.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Matthieu Kamwa amesema kuwa wapo  tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya katika kutekeleza hilo ili kuweza kuboresha mifumo ya afya nchini.
“Unajua Takwimu ni utajiri hasa katika kutekeleza shughuli za kutoa huduma za afya kwa wananchi hivypo hatuna budi kuunga mkono juhudu za Serikali ya Tanzania katika kufanikisha hili jambo kwani litaturahisishia hata sisi katika kutoa miongozo ya afya” alisema Dkt. Kamwa.

Jumanne, 6 Februari 2018

TIBA MTANDAO KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI



Na WAMJWW. Dom
Serikali imejipanga kutumia tiba mtandao kuboresha huduma za afya nchini kwenye hospitali zote za ngazi ya taifa, rufaa na wilaya ili kuwawezesha wagonjwa waishio sehemu mbali mbali nchini kupata huduma za afya kwa wakati na kwa ufanisi.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati akifungua kongamano la ubunifu na utekelezaji wa huduma za tiba mtandao Tanzania lililofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa jengo la LAPF, Dodoma.

Dkt. Ulisubisya amesema kuwa lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha watendaji wakuu wa hospitali za taifa nchini, madaktari bingwa wa sekta ya Afya, wakuu wa taasisi zinazoshughulika na sekta ya Afya, Wizara ya TAMISEMI, Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano; taasisi nyingine za Serikali; sekta binafsi na wabia wa maendeleo ili kujadiliana na kuwa na uelewa wa pamoja wa kufanikisha utekelezaji wa huduma za tiba mtandao ili kuboresha huduma za afya nchini.

Amesema kuwa tiba mtandao itawezesha na kuongeza ufanisi katika kufanya uchunguzi, utoaji wa tiba na madawa kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza na yanayotokana na ajali za barabarani.
“Hadi hivi sasa ni asilimia 37 tu ya wagonjwa wa kifua kikuu ndio wanaotambulika na kupatiwa huduma na Wizara ya Afya katika hospitali mbalimbali nchini. Hivyo, tiba mtandao itawezesha upatikanaji wa wagonjwa na ufikishaji wa huduma kwao kwa wagonjwa wengine asilimia 63”, alifafanua Dkt. Ulisubisya.

Aliongeza kuwa tiba mtandao itapunguza gharama za wagonjwa na wanaowahudumia kusafiri kufuata madaktari. Aidha, amewataka wakuu hao wa taasisi kuwaruhusu wataalamu wao, wa Wizara ya TAMISEMI na wa Wizara ya Afya, kushiriki mafunzo ya tiba mtandao ili kuongeza ufanisi wao katika kuhudumia wagonjwa.

Amewataka wataalamu wa afya na wakuu wa taasisi zinazohusika na masuala ya afya kununua vifaa tiba vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) vyenye viwango na ubora unaohitajika ili kuwezesha tiba mtandao na manunuzi hayo yazingatie na kufuata ununuzi wa pamoja wa huduma na bidhaa za Serikali.
Vifaa vya kisasa vya TEHAMA vinavyohusika na tiba mtandao vitawawezesha wataalamu kufanya uchunguzi kwa mgonjwa, kupata majibu ya uhakika na kumpatia mgonjwa tiba inayostahili na ya uhakika. 
Aidha, amemuelekeza Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Eng. Ulanga, ambao ndio waanadaji na waratibu wa kongamano hilo, kushirikiana na TTCL kuhakikisha kuwa tiba mtandao inapatikana katika hospitali zote za rufaa na hospitali ambazo zina changamoto ya kijiografia ya kufikika kwa urahisi.

Ijumaa, 2 Februari 2018

DKT MPOKI ASEMA WATOA HUDUMA ZA USINGIZI WANAHITAJIKA ZAIDI NCHINI.

- Hakuna maoni




Watumishi wa wa afya wa kutoa huduma za usingizi wanahitajika zaidi nchini ili kuweza kutoa huduma hiyo kwa wingi na ukaribu zaidi mara zinapohitajika kwa wagonjwa wanaohitaji upasuaji kwa usalama katika hospitali zetu

TUMEKOSOGEZA KARIBU


Wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto.
Inayo furaha kubwa kuwakaribisha wananchi wote ndani na nje ya nchi kutembelea katika mitandao yake ya kijamii ili kupata taarifa mbalimbali za kiafya. Aidha tunakaribisha maoni na ushauri mbalimbali kuhusu sekta ya afya. "Jenga taifa lenye afya bora kwa uchumi imara"

#AFYA_YANGU_MTAJI_WANGU

Jumatano, 31 Januari 2018

TANGAZO LA KUITWA KAZINI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,
WAZEE NA WATOTO
 
 
 
 
TANGAZO LA KUITWA KAZINI
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto -Idara Kuu Afya anawajulisha wafuatao kuripoti kazini Makao Makuu ya Wizara Mjini Dodoma ndani ya siku 14 wakiwa na vyeti halisi vya  elimu ya Sekondari, Taaluma,usajili wa Baraza/Bodi ya kitaaluma,cheti cha kuzaliwa pamoja na nakala mbili za picha ndogo (passport)
Imetolewa na :

Katibu Mkuu-Afya
31/1/2018




ORODHA YA MAJINA YA WOAMBAJI WANAOTAKIWA KURIPOTI WIZARA YA AFYA MEANDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO KUKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA  






NA JINA CHEO KITUO CHA KAZI







1 LILIAN DIDAS LYAKURWA KATIBU WA AFYA II KATIBU MKUU AFYA







2 NKWIMBA NYALALI AFISA MUUGUZI MSAIDIZI II KATIBU MKUU AFYA







3 MARY MATHIAS OTTARU AFISA AFYA MAZINGIRA II KATIBU MKUU AFYA







4 JACOB R. TARIMO MUUGUZI  KATIBU MKUU AFYA







5 SOPHIA ISSA LUCAS MHUDUMU WA AFYA KATIBU MKUU AFYA







6 HAPPY ALEX YOHANES MHUDUMU WA AFYA KATIBU MKUU AFYA







7 MARTHA ADRIANO MHUDUMU WA AFYA KATIBU MKUU AFYA







8 JENIPHER JOSEPH GHULIKU MTEKNOLOJIA MSAIDIZI MAABARA KATIBU MKUU AFYA







9 SURAIYA A. DULE MHUDUMU WA AFYA KATIBU MKUU AFYA







10 NEEMA MWASENGA MHUDUMU WA AFYA KATIBU MKUU AFYA







11 SCHOLASTICA OFAMAN MHUDUMU WA AFYA KATIBU MKUU AFYA







12 BLANDINA VICTOR SHUMA AFISA MUUGUZI MSAIDIZI II KATIBU MKUU AFYA

WATOA HUDUMA ZA USINGIZI WANAHITAJIKA ZAIDI NCHINI.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya, akihutubia mapema leo wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi, tukio lililofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Dkt. Otilia Gowelle, akinyoosha mkono kama ishara ya kujitambulisha, wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi.
 
Mkurugenzi wa Mafunzo ya Shahada za mwanzo MUHAS ambae pia alimwakilisha Mkuu wa Chuo Prof. Mainem Moshi akiwasilisha taarifa fupi ya Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi.

Mlezi wa Wanafunzi kutoka Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS Dtk. Edith Tarimo akiwasilisha Taarifa mbele ya mgeni rasmi ambae ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya.

Tukio la ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi, katika ukumbi wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya, wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi, tukio lililofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS jijini Dar es salaam.


Na WAMJWW-DSM.
Watumishi wa wa afya wa kutoa huduma za usingizi wanahitajika zaidi nchini ili kuweza kutoa huduma hiyo kwa wingi na ukaribu zaidi mara zinapohitajika kwa wagonjwa wanaohitaji upasuaji kwa usalama katika hospitali zetu .
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Idara kuu ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa kufundishia watu watakaotoka na Shahada ya Huduma ya Usingizi itakayotolewa na Chuo Cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS leo jijini Dar es salaam.
“Nawaagiza wenzetu wa MUHAS wahakikishe  kasi ya kuandaa mtaala wa kufundishia iongezwe na  uletwe haraka ili kuweza kupata wataalamu wa kutoa huduma za usingizi ili wakafanye kjazi kwenye Hospitali za Rufaa za Mkoa” alisema Dkt. Ulisubisya.
Aidha Dkt. Ulisubisya amesema kuwa kabla ya mtaala huu kupitishwa hapo nyuma wagonjwa awalikuwa wanapata huduma za usingizi pindi wanapohitaji kufanyiwa upasuaji kutoka kwa wataalamu waliopata mafunzo kwa mwaka mmoja au waliojifunza kwenye sehemu zao za kazi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mafunzo wa Shahada za Mwanzo MUHAS Prof. Mainem Moshi amesema kuwa tayari wameshapeleka mtaala wa wahandishi wa vifaa tiba kwani wanahitajika takribani wahandisi  elfu 8 nchini.
Aidha Prof. Mainem amesema kuwa kusimamishwa kwa mtaala wa kufundishia shahada ya udhamiri kwa kozi za ukunga kumepeleka vifo 556 katika kina mama laki moja kwa wamama wanaojifungua hivyo Serikali ipo haja ya kurudisha huu mtaala.