Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 31 Januari 2018

WATOA HUDUMA ZA USINGIZI WANAHITAJIKA ZAIDI NCHINI.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya, akihutubia mapema leo wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi, tukio lililofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Dkt. Otilia Gowelle, akinyoosha mkono kama ishara ya kujitambulisha, wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi.
 
Mkurugenzi wa Mafunzo ya Shahada za mwanzo MUHAS ambae pia alimwakilisha Mkuu wa Chuo Prof. Mainem Moshi akiwasilisha taarifa fupi ya Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi.

Mlezi wa Wanafunzi kutoka Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS Dtk. Edith Tarimo akiwasilisha Taarifa mbele ya mgeni rasmi ambae ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya.

Tukio la ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi, katika ukumbi wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya, wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa Kufundishia watu watakaotoa Huduma ya Usingizi, tukio lililofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS jijini Dar es salaam.


Na WAMJWW-DSM.
Watumishi wa wa afya wa kutoa huduma za usingizi wanahitajika zaidi nchini ili kuweza kutoa huduma hiyo kwa wingi na ukaribu zaidi mara zinapohitajika kwa wagonjwa wanaohitaji upasuaji kwa usalama katika hospitali zetu .
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Idara kuu ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa ufunguzi wa Mtaala wa kufundishia watu watakaotoka na Shahada ya Huduma ya Usingizi itakayotolewa na Chuo Cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS leo jijini Dar es salaam.
“Nawaagiza wenzetu wa MUHAS wahakikishe  kasi ya kuandaa mtaala wa kufundishia iongezwe na  uletwe haraka ili kuweza kupata wataalamu wa kutoa huduma za usingizi ili wakafanye kjazi kwenye Hospitali za Rufaa za Mkoa” alisema Dkt. Ulisubisya.
Aidha Dkt. Ulisubisya amesema kuwa kabla ya mtaala huu kupitishwa hapo nyuma wagonjwa awalikuwa wanapata huduma za usingizi pindi wanapohitaji kufanyiwa upasuaji kutoka kwa wataalamu waliopata mafunzo kwa mwaka mmoja au waliojifunza kwenye sehemu zao za kazi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mafunzo wa Shahada za Mwanzo MUHAS Prof. Mainem Moshi amesema kuwa tayari wameshapeleka mtaala wa wahandishi wa vifaa tiba kwani wanahitajika takribani wahandisi  elfu 8 nchini.
Aidha Prof. Mainem amesema kuwa kusimamishwa kwa mtaala wa kufundishia shahada ya udhamiri kwa kozi za ukunga kumepeleka vifo 556 katika kina mama laki moja kwa wamama wanaojifungua hivyo Serikali ipo haja ya kurudisha huu mtaala.

0 on: "WATOA HUDUMA ZA USINGIZI WANAHITAJIKA ZAIDI NCHINI."