Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 27 Januari 2018

WAKURUGENZI WA HALMASHAURI WATAKIWA KUSIMAMIA FEDHA ZA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA AFYA

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto akiangalia kazi inavyoendelea katika hospitali hiyo.

Waziri ummy Mwalimu akiangalia ramani ya kituo hicho cha afya ambacho kimejengwa kwa ushirikiano wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Shirika la SEDA Foundation, kulia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Subi na kushoto ni mmoja wa Viongozi wa Shirika hilo.

Waziri Ummy Mwalimu akiangalia duka la dawa lililopo kwenye hospitali ya Mkoa ya Sekoture ambapo upatikanani wa dawa kwa Mkoa wa Mwanza ni asilimia 80.

Jengo la Maabara lililojengwa kwenye kituo hicho cha afya katika mpango wa Serikali wa kuboresha huduma za dharura za uzazi kwenye vituo vya afya nchini.(Picha zote na Wizara ya Afya)

Waziri Ummy Mwalimu akiangalia Ramani ya Ujenzi wa jengo la ghorofa nne la Uzazi linalojengwa hospitali ya Mkoa ya Sekoture jijini Mwanza. 

Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akikagua huduma za afya kwenye kituo cha afya cha kamanga kilichopo Wilaya ya Sengerema.Waziri ummy yupo Mkoani Mwanza katika ziara ya kikazi ya kujionea hali ya utoaji huduma za afya mkoani hapo.

Waziri Ummy Mwalimu na Naibu Waziri Dkt.Angela Mabula wakikagua ujenzi wa jengo la dharura la uzazi kwenye kituo cha afya cha Karume kilichopo kata ya Igombe Wialayani Ilemela,akiyevaa koti la bluu ni Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt.Florian Tinuga.

Mawaziri hao wakijadili jambo wakati wa ukaguzi wa jengo la upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni linalojengwa kwenye kituo cha afya cha Karume ,Wilayani Ilemela.


Na.WAMJW,Mwanza
Wakurugenzi wa Halmashauri nchini wametakiwa kusimamia Fedha za kuboresha huduma za dharura zinazotolewa na Serikali zitumike ipasavyo na si kwa matumizi mengine.
 
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu jijini hapa wakati akiwa kwenye ziara ya kukagua shughuli za utoaji huduma za afya pamoja na ujenzi wa huduma za dharura za Uzazi kwenye kituo cha afya cha Karume kilichopo kata ya Igombe Wilayani Ilemela.
 
Waziri Ummy alimpongeza Mkurugenzi wa Ilemela kwa matumizi mazuri ya fedha hizo ambapo alijionea kazi nzuri inayoendelea katika kituo hicho ambapo wametumia wajenzi wa kawaida na ujenzi huo unaenda vizuri na kwa kiwango kinachoridhisha.
 
Aidha,alisema Fedha za kuboresha miundombinu ya huduma za uzazi wa dharura zitumike kama haya angalau kujengwe chumba cha upasuaji,maabara ya damu na tunamataka wodi ya wazazi na nyumba moja ya mtumishi kuliko kujenga masuala mengine
 
“kama fedha zitabaki unaweza kufikiri kujenga vitu vingine,kuliko kqenda kutumika kwa masuala mengine kama baadhi ya sehemu nyingine wanavyofanya, kama fedha zimebaki nipo tayari kukuruhusu kujenga kitu kingine Mkurugenzi,hongera sana Mkurugenzi na viongozi wengine”.
 
Hata hivyo alisema Tanzania ni moja ya nchi yenye vifo vingi vya akina mama wajawazito na watoto”leo hii toka saa sita usiku tuanze siku hadi saa sita usiku wanawake 30 wa kitanzania wanafariki kwa sababu tu ya kutimiza wajibu wao wa kuleta kiumbe duniani”
 
“Kwahiyo Mhe.Rais alichokifanya  kwa kushirikiana na wadau tunaboresha huduma za uzazi zikiwepo za upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni,hivyo tumefurahi kuona hapa zile shilingi milioni mia tano zimetumika ipasavyo,binafsi nimedhirika  na kazi iliyofanywa hapa karume hivyo naahidi kuleta fedha kwa ajili ya   kuboresha miundombinu ya kituo cha afya Buzurugwa”alisema Mh. Ummy.
Wakati huo huo nae naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi na Mbunge wa Jimbo la Ilemele Dkt.Angela Mabula alisema wao kama viongozi watahakikisha fedha zote zitakazoenda kwa ajili ya afya itatumika ipasavyo na wataisimamia ili kuweza kuboresha miundombinu ya sekta ya afya
 
Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela amewataka wananchi wa    Igombe kuendeleza mshikamano wanaouonyesha ili kuendelea kufanya makubwa zaaidi kwa kujiletea maendeleo”mchakato wa maendeleo chini ya Jemedari wetu rais Magufunli ndo kwanza umeanza”.

0 on: "WAKURUGENZI WA HALMASHAURI WATAKIWA KUSIMAMIA FEDHA ZA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA AFYA"