Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 24 Januari 2018

MH. UMMY MWALIMU AONGOZA KIKAO CHA MWAKA CHA WADAU WA SEKTA YA AFYA.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akielezea jambo katika kikao cha mwaka cha Wadau wa Sekta ya Afya nchini mapema leo jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Faustine Ndugulile akijibu hoja wakati wa kikao hicho cha Wadau wa Sekta ya Afya, kilichofanyika mapema leo jiini Dar Es Salaam.

Kiongozi wa shirika la Maendeleo ya Afya Milma Kettunem(wa mwisho) akiwasilisha mchango wake katika kikao cha Wadau wa Sekta ya Afya. Wa kwanza ni Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu, na katikati ni Barozi wa Ujerumani nchini Tanzania Dkt. Detlef Waechter.

Wadau wa Sekta ya Afya wakifuatilia kwa makini taarifa kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu(hayupo kwenye picha) katika Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Afya wenye lengo la kubainisha vipaumbele vya 2017/2018 katika Sekta ya Afya.


Na WAMJWW. DSM
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (MB) leo ameongoza kikao cha mwaka cha Wadau wa Sekta ya Afya nchini, huku lengo likiwa kujadili na kubainisha vipaumbele vya mwaka 2018/2019 katika sekta ya Afya.

Akifungua Mkutano huo Mh. Ummy Mwalimu(MB) alisema kuwa katika kuelekea Tanzania ya Viwanda ni lazima taifa lielewe kwamba kuna umuhimu wa kuimarisha Sekta ya Afya nchini katika ngazi ya utoaji huduma na miundombinu kwa jamii ili kuwezesha uwepo wa jamii yenye afya njema itakayoweza kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.
“Ni Vigumu kutekeleza Sera ya Viwanda kama hatutaimarisha Sekta ya Afya nchini”, alisema Mh. Ummy Mwalimu.

Katika kikao hicho ambacho kilihudhuriwa na Wadau mbali mbali wa Maendeleo, Mashirika yasiyo ya kiserikali, Mashirika ya kidini na Sekta Binafsi huku  kikitawaliwa na masuala ya kuimarisha Afya ya mama na watoto wachanga, rasilimali watu katika Afya, miundombinu ya Huduma za Afya, rasilimali fedha katika Sekta ya Afya, Muendelezo wa Huduma, Utawala na uwajibikaji na Afya ya vijana hasa wasichana.
 
Akiongea kwa niaba ya Wadau wa Maendeleo, Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Dkt. Detlef Waechter ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa nia ya dhati katika kuimarisha na kukuza Sekta ya Afya nchini na kuahidi kuendeleza ushirikiano ikiwemo kutoa rasilimali fedha na utawala ili kufanikisha utoaji wa huduma bora za Afya katika jamii.
 
Kwa upande wa Mashirika yasiyo ya kiserikali wameiomba Serikali kuharakisha mpango wa Bima ya Afya kwa wote jambo litalosaidia kupunguza gharama za matibabu kwa kiasi kikubwa kwa wananchi wa kipato cha chini.

0 on: " MH. UMMY MWALIMU AONGOZA KIKAO CHA MWAKA CHA WADAU WA SEKTA YA AFYA."