Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 15 Januari 2018

BAADHI YA MADAKTARI BINGWA KUTOKA MUHIMBILI WANATAKIWA KUHAMIA HOSPITALI YA TEMEKE KUONGEZA NGUVU.


Pix 1 & 2
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiwajulia hali baadhi ya wagonjwa wakati alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke ili kuona hali ya utoaji hudfuma kwa wagonjwa katika hospitali hiyo leo jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katikati akiongea na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke awapo pichani alipotembelea hospitali hiyo  ili kuona hali ya utoaji huduma kwa wagonjwa katika hospitali hiyo leo jijini Dar es salaam, wa kwanza kulia ni Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Mohammed Mohammed na wa kwanza kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Amani Malima

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katikati akipata maelezo kutoka kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke  Dkt. Amani Malima kushoto wakati alipotembelea Hospitali hiyo ili kuona hali ya utoaji huduma kwa wagonjwa katika hospitali hiyo leo jijini Dar es salaam.


Pix 5 & 6
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu mwenye kilemba cheupe akiongea na baadhi ya wananchi wanaosubiri kupata huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke wakati alipotembelea Hospitali hiyo ili kuona hali ya utoaji huduma kwa wagonjwa hospitalini hapo leo jijini Dar es salaam.

NA WAMJW-DAR ES SALAAM

BAADHI ya Madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili wanatakiwa kuhamia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke ili kuongeza rasilimali watu kwa ajili ya kumudu hali ya ongezeko la wanaotaka huduma bora za afya hospitalini hapo. 

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.  Ummy Mwalimu alipotembelea Hospitali hiyo ili kuangalis hali ya utoaji wa huduma za afya kwa wananchi hospitalini hapo. 

"Kubwa nliloligundua hapa ni kuna mlundikano wa idadi kubwa ya wanaohitaji huduma hivyo wale madaktari tunaowatoa Muhimbili hasa madaktari bingwa baadhi tutawahamishia hapa ili kusaidiana na madaktari wa Temeke katika kutoa huduma bora kwa watu wengi zaidi" alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Serikali ipo mbioni kutafuta rasilimali fedha kwa ajili ya kujenga jengo la ghorofa nne ambalo litachangia katika kuondoa tatizo la mlundikano wa wagonjwa hospitalini hapo mapema mwaka huu.

Mbali na hayo Waziri Ummy ametoa rai kwa wananchi wore kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kupata huduma za matibabu kwa wakati sahihi na kwa bei nafuu hasa kwa watoto wadogo wenye kadi inayoitwa Afya toto Kadi kwa bei ya shilingi 50, 400 tu. 

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke Dkt. Amani Malima amesema kuwa wapo mbioni kuagiza vifaa na vifaa tiba pamoja na kuomba kuongezwa watumishi  kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wengi zaidi kama ilivyoelekezwa na Mhe.  Waziri Ummy. 

"Tunakabiliwa na upungufu wa watumishi na ndo mana kuna mlundikano wengi wa wanaohitaji huduma lakini tunamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kuja na kuona changamoto zetu na kutuhaidi mazuri zaidi katika jitihada za kutoa hufuma bora za afya kwa wananchi" alisema Dkt. Malima. 


0 on: "BAADHI YA MADAKTARI BINGWA KUTOKA MUHIMBILI WANATAKIWA KUHAMIA HOSPITALI YA TEMEKE KUONGEZA NGUVU. "