Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 18 Januari 2018

SERIKALI YAJA NA MUONGOZO ILI KUPAMBANA NA USUGU WA VIMELEA VYA DAWA.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wadau mbalimbali wa sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa matibabu na orodha ya dawa zote muhimu leo jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi Muongozo wa Matibabu na Orodha ya dawa muhimu wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam, wa kwanza kushoto ni Mganga Mkuu wa Serikali prof. Mohammed Bakari Kambi na kushoto ni Mwakilishi wa WHO.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wa pili kushoto akionyesha Muongozo wa Matibabu na orodha ya dawa zote muhimu wakati wa uzinduzi wa Muongozo huo leo jijini Dar es salaam, wa kwanza kuhoto ni Mganga Mkuu wa Serikali prof. Mohammed Bakari Kambi ,wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Kinga na Ubora Wizara ya Afya Dkt. Mohammed Mohammed na anayefuata ni mwakilishi wa WHO.



Pix 4,5 &6
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto mwenye kilemba akiwakabidhi baadhi ya wawakilishi wa Taasisi mbalimbali za Afya nchini Muongozo wa Matibabu na orodha ya dawa wakati wa uzinduzi wa Muongozo huo leo jijini Dar es salaam.
NA WAMJW-DAR ES SALAAM

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeandaa Muongozo wa matibabu nchini na orodha ya dawa zote muhimu ili kuepukana na tatizo la usugu wa vimelea vya dawa. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa matibabu na orodha ya dawa zote muhimu uliofanyika leo jijini Dar es salaam. 

"Ni muhimu kila kituo cha afya kuwa na dawa za kutosha, vifaa na vifaa tiba lakini ni lazima tuzingatie muongozo wa matibabu na orodha ya dawa kulingana na ugonjwa fulani ili kuepuka tatizo hili" alisema Waziri  Ummy 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Muongozo huo umezingatia vigezo vyote vya kuweka dawa ambazo zilikuwa hazipo katika ngazi ya  zahanati na  vituo vya afya ambazo zimepata uthibitisho kutoka Shirika la Afya la Dunia (WHO). 

Aidha Waziri Ummy amewapiga marufuku Bohari Kuu ya dawa ya Taifa MSD na Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa (NHIF) kuagiza na kuandika dawa zilizo nje ya muongozo uliozinduliwa leo ili kuondoa matumizi ya dawa yasiyo sahihi. 

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa kila kituo cha afya ni lazima kiongozwe na Tabibu na sio vinginevyo ili kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana katika kituo cha afya husika. 

Kwa mujibu wa Waziri Ummy amesema kuwa itafika kipindi vituo vya afya ambavyo havikizi vigezo vitafungiwa ili kuepuka usababishwaji wa vifo visivyo vya lazima kwa watanzania. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi amesema kuwa muongozo wa kutibu magonjwa mbambali 
umezingatia Orodha ya dawa ambazo zitakuwa zinatumika nchini kwetu kama dawa muhimu za kutibu magonjwa hayo. 

0 on: "SERIKALI YAJA NA MUONGOZO ILI KUPAMBANA NA USUGU WA VIMELEA VYA DAWA. "