Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 3 Januari 2018

MAGONJWA YASIYO YAKUAMBUKIZA YACHANGIA ASILIMIA 27 YA VIFO VYOTE NCHINI

Kaimu Mkurugenzi magonjwa yasiyo yakuambukiza Dkt. Sarah Maongezi akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo katika picha) katika kikao kilichofanyika mapema leo katika ukumbi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road kikihusu tuzo ya Elimu kwa jamii waliopata kutoka Shirikisho la kimataifa la magonjwa yasiyo yakuambukiza mwishoni mwa mwaka katika mkutano wa kimataifa uliofanyika katika falme zakiarabu.

Kaimu Mkurugenzi magonjwa yasiyo yakuambukiza Dkt. Sarah Maongezi akipokea tuzo ya Elimu kwa jamii kutoka kwa Mwenyekiti wa TANCDA Dkt. Tatizo Waane mapema leo katika ukumbi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road, Wapili kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TANCDA Andrew Swai.

Kaimu Mkurugenzi magonjwa yasiyo yakuambukiza Dkt. Sarah Maongezi akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo katika picha) katika kikao kilichofanyika mapema leo katika ukumbi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road kikihusu tuzo ya Elimu kwa jamii waliopata kutoka Shirikisho la kimataifa la magonjwa yasiyo yakuambukiza mwishoni mwa mwaka katika mkutano wa kimataifa uliofanyika katika falme zakiarabu, pembeni yake ni Mwenyekiti wa TANCDA Dkt. Tatizo Waane.


Na WAMJWW, Dsm

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yasema kuwa magonjwa yasiyo yakuambukiza yanachangia kiasi kikubwa katika vifo vyote vinavyotokea hapa nchini.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa magonjwa yasiyokuwa yakuambukiza Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Sarah Maongezi wakati akipokea tuzo kutoka kwa TANCDA waliopata mwishoni mwa mwaka huu kutoka katika Shirikisho la Kimataifa la Magonjwa yasiyo yakuambukiza.

“Muongeze juhudi katika kupambana na magonjwa hayo ambayo yanachangia asilimia27 ya vifo vyote hapa Tanzania” Alisema Dkt Maongezi.

Dkt Maongezi aliendelea kusema kwamba Serikali imedhamiria kwa nia kabisa katika kupambana na magonjwa haya kwa kuamua kushirikiana na Asasi mbali mbali nchini ili kutimiza azma hiyo ya kupambana na magonjwa haya.

“Serikali pekee yetu hatuwezi na ndio maana tukashirikiana na Asasi kama TANCDA  inayojumuisha vyama vingine kama vile, Taasisi ya Saratani, Taasisi ya Magonjwa ya Moyo, Taasisi ya Mfumo wa Hewa na Taasisi ya Kisukari ambazo kwa ujumla zimejenga ushirikiano katika kupambana na magonjwa haya” Aliongeza Dkt. Maongezi.

Aidha Dkt. Maongezi amewahasa TANCDA kuongeza juhudi na kasi zaidi katika kupambana na magonjwa haya ili kuisaidia jamii kubwa ya Watanzania inayoangamia kutokana na kukosa elimu juu ya magonjwa hayo.

Dkt. Maongezi amewashukuru Waandishi wa Habari wote kwa mchango mkubwa wanaoendelea kuutoa katika kuisaidia jamii ya Tanzania hususani katika kupambana na Magonjwa yasiyo yakuambukiza kwa kuandika Makala za magazetini na vipindi vya Redioni na Tv, na kuwahasa kuendelea kufanya kazi hivyo ya kuelimisha jamii kwa juhudi.

Nae Makamu Mwenyekiti wa TANCDA Pro Andrew Swai ametoa wito kwa Asasi hizo kufanya tafiti zaidi katika maeneo mbali mbali bila kusahau vijijini, ili kuweza kufahamu idadi kamili ya watu waliohathirika na maradhi hayo na kurahisisha kufikisha ujumbe katika maeneo hayo.

“TANCDA inatakiwa kujitanua ili waweze kuwafikia watu wote, pia ule ujumbe unaopelekwa uweze kuwafanya watu ili aweze kubadilika”. Alisema Prof. Andrew Swai.

0 on: "MAGONJWA YASIYO YAKUAMBUKIZA YACHANGIA ASILIMIA 27 YA VIFO VYOTE NCHINI"