Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 18 Januari 2018

WAZIRI UMMY ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA KUHAMISHA WAGONJWA MNH


Pix 1&2
Baadhi ya vitanda vilivyohamishwa wagonjwa katika wodi mbalimbali kwenye jingo la Mwaisela Hospitalini Muhimbili kwenda Hospitali ya Tiba na Taaluma Mloganzila kufuatia utekelezaji wa agizo la Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto la kuhamisha wagojwa katika jingo hilo hivi karibuni.



Pix 3 & 5
Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitembelea baadhi ya wodi zilizohamishwa wagonjwa kwenye jingo la Mwaisela kufuatia agizo alilolitoa la kuhamisha wagonjwa kwenye jingo hilo kuhamia Mloganzila wakati alipotembelea Hospitali ya Taifa muhimbili kuangalia utekelezaji wa agizo lake.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wa pili kulia akimjulia hali mtoto Maria (17) mkazi wa Mtwara aliyetangazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa ana uvimbe mkubwa wakati alipokwenda kumtembelea kwenye Taasisi ya Mifupa MOI jijini Dar es salaam.


NA WAMJW DAR ES SALAAM

WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameridhishwa na utekelezaji wa agizo la kuhamisha wagonjwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili kwenda Hospitali ya Tiba na Taaluma Mloganzila.

Hayo ameyasema wakati alipotembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kuangalia hali ya utoaji wa huduma pamoja na utekelezaji wa agizo hilo alilolitoa wakati alipotembelea Hospitali ya Tiba na taaluma Mloganzila mapema mwezi huu.

“Niliwaagiza MNH kuhamisha wagonjwa waliopo kwenye jingo la Mwaisela kuaznia wodi namaba 3,4,5,6,7 na 8 isipokuwa wagonjwa mahututi na wenye kesi maalumu ila nawapongeza wametekeleza agizo hilo mara moja” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amewapongeza MNH kwa  kuwahamisha madaktari bingwa 15  15 na wauguzi zaidi ya 30 kwenda katika Hospitali ya Mloganzila ili kuongeza nguvu ya kutoa huduma sawa na inayotolewa Muhimbili.

Mbali na hilo Waziri Ummy amesema kuwa zoezi hilo limetoa nafasi ya kuwahamisha baadhi ya wagonjwa wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) hususani watoto angalau vitanda 50 kupeleka kwenye jingo la Mwaisela hospitali ya MNH.

“JKCI ni moja wapo ya Taasisi zinazotoa matibabu ya upasuaji hasa ya moyo na ina upungufu wa majengo  hivyo kutokana na uhamishwaji wa wagonjwa jengo la Mwaisela tunawapa nafasi ya kupeleka vitanda 50 kwa ajili ya wagonjwa wao waliofanyiwa upasuaji hususan watoto” aliongeza Waziri ummy.

Sambamba na hilo Waziri Ummy alipata muda wa kwenda kumtembelea Mgonjwa alikuwa analalamika kwenye baadhi ya vyombo vya habari ajulikanaye kwa jina la Maria (17) mkazi wa Masasi Mkoani Lindi kuwa ana uvimbe mkubwa na akalizimika kuletwa katika Hospitali ya Taifa yMuhimbili.

“ Niliposikia habari ya Binti huyo kwenye baadhi ya vyombo vya habari niliomba namba za wahusika na kuwaelekeza waende Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na hivi sasa anapata matibabu kwenye taasisi ya Mifupa (MOI) na wanaendelea na juhudi za kumtibia ili kumrudsha katika hali yake ya zamani” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy alitoa rai kwa Watanzania kuwa wanatakiwa kuzingatia maelekezo kutoka kwa madaktari bingwa na kuacha imani potofu kwa kwenda kwa waganga wa kishirikina kwa kuamini mgonjwa atakuwa amerogwa ili kuepuka tatizo kuwa kubwa zaidi.

“Kwa mujibu wa madaktari wamesema kuwa Maria alihudhuria hospitali hapo mara mbili na hakurudi tena kama ilitakiwa afanye na badala yake akajikita zaidi kwenye tiba asili mpaka imesababisha tatizo kuwa kubwa zaidi hivyo watanzania tunatakiwa kuwaamini zaidi madaktari na kufuata maelekezo” alisema Waziri Ummy.


0 on: "WAZIRI UMMY ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA KUHAMISHA WAGONJWA MNH"