Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 16 Januari 2018

TANGAZO LA UFADHILI-MARUDIO

 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
Tanzania Emblem RGB                             

         




TANGAZO LA UFADHILI-MARUDIO

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anawatangazia wanafunzi wote walioko vyuoni na wale wote waliopata udahili wa masomo ya Uzamili katika fani za Afya kwa mwaka wa masomo 2017/2018, kuwa muda wa kuwasilisha maombi umeongezwa hadi tarehe 19/01/2018. Ufadhili huu ni kwa ajili ya kulipiwa ada pamoja na posho ya utafiti pindi mwanafunzi anapokuwa kwenye kipindi cha kufanya utafiti kama sehemu ya mafunzo yake. Kwa wanafunzi waliokwisha wasilisha maombi yao, hawatakiwi kuomba upya.

Vigezo vilivyowekwa ni kama ilivyoainishwa kwenye Tangazo la awali ambavyo ni :

1.    Raia wa Tanzania.
2.    Awe amedahiliwa chuoni kuanza masomo kwa mwaka wa kwanza 2017/2018
3.    Watumishi wa Afya wanaofanya kazi katika vituo vilivyo wilayani/mikoani ambao baada ya mafunzo, aidha wanaweza kupangiwa vituo vya kazi (hospitali za mikoa) au kurudi na kuendelea kufanya kazi katika vituo vyao vya awali ambao utaalamu wao utakuwa unahitajika na awe ameruhusiwa na mwajiri wake kwenda masomoni.
4.    Nyanja za Tiba ambazo ni za msingi katika utoaji wa huduma za rufaa katika hospitali za Rufaa za mikoa kama Anaesthisiology, Surgery, Neurosurgery, Obstetric and Gynaecology, Orthopaedic Surgery, Emergency Medicine, Paediatric, Internal Medicine, Critical Care in Nursing na Midwifery and Womens Health
5.    Nyanja za ubingwa (Specialities na Super-specialities) katika hospitali za kitaifa (magonjwa ya moyo, figo, saratani n.k.) ili kujenga uwezo wa ndani ya nchi katika jitihada za kupunguza wagonjwa wa rufaa wanaotibiwa nje ya nchi.
6.    Awe na barua ya ruhusa ya masomo kutoka kwa mwajiri wake (ambatanisha)
7.    Awe tayari kuingia mkataba wa kuitumikia Serikali kwa muda usiopungua miaka 5 baada ya kuhitimu mafunzo.
8.    Mtumishi asiwe na ufadhili mwingine.

Aidha, kwa kuwa wanafunzi wamesharipoti vyuoni, barua za maombi zipitishwe kwa Wakuu wa Vyuo kuthibitisha kuwa mwanafunzi yuko chuoni, na kwa wale ambao bado wapitishe barua kwa Mwajiri wao. Tangazo hili linahusu watumishi wa mwaka wa kwanza wa masomo 2017/2018 tu. Mwisho wa kupokea maombi haya ni tarehe  19/01/2018. Waombaji wote watume maombi hayo kwa anuani ifuatayo ;


Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Chuo Kikuu Dodoma,
Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Maendeleo ya Jamii
Jengo Namba 11,
S.L.P 743
40478, DODOMA


Imetolewa na;

Katibu Mkuu - Afya

16/01/2018


1 on: "TANGAZO LA UFADHILI-MARUDIO"
  1. Mnachelewa sana kutoa majina ya walipata ufadhili wa masomo,kwahiyo inakuwa kero huku mavioni,mjitahidi wizara mtoe kwa wakati,ili mtu ajijue amepata ama laa

    JibuFuta