Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 23 Januari 2018

SERIKALI YAENDELEA KUJIZATITI KATIKA KUPAMBANA NA MAGOJWA YASIYO YAKUAMBUKIZA.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) akisikiliza kwa umakini changamoto kutoka kwa mgonjwa, pindi alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake a kukagua Ubora wa huduma za Afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) akisalimiana na mgonjwa pindi alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, wa kwanza ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt. Yahya Msuya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) akikagua Bin Kadi katika Stoo ya Dawa pindi alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake a kukagua Ubora wa huduma za Afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile (wa katikati) akiendelea na ziara yake ya kukagua Ubora wa huduma za Afya, pindi alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mbeya. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Jinsia kutoka Wizara Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, wazee na watoto Idara ya Maendeleo ya Jamii Dkt. Julius Mbilinyi, Kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo.



Na WAMJWW. MBEYA

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yaendelea kujizatiti katika kupambana na magonjwa yasiyo yakuambukiza ili kulilinda kundi kubwa la jamii ya Watanzania.

Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa katika ziara yake Mkoani Mbeya ya kukagua shughuli za utoaji wa huduma za Afya na kutathimini shughuli za maendeleo ikiwemo upanuzi wa miundombinu kama vile Vituo vya Afya na Shule.

Dkt. Ndugulile alisema kuwa magonjwa yakuambukiza yamekuwa yakiongezeka kwa kasi sana kutokana na mabadiliko ya mtindo ya Maisha, kutofanya mazoezi na hali ya ulaji usiofaa wa wananchi wengi katika jamii.

“Serikali imezidi kuboresha upatikanaji wa Huduma za magonjwa ya Saratani, mfano kupitia Hospitali ya Ocean Road tulioipatia vifaa vya kisasa sana, sambamba na hilo tumeanza kufanya upandikizaji wa Figo ndani ya Hospitali ya Benjamini Mkapa,” Alisema Dkt. Ndugulile

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kwamba, Serikali imewapeleka madaktari katika nchi za China na India ili kuanza kufanya mafunzo ya upandikizaji wa Ini, hali itakayosaidia kupunguza gharama kubwa kwa wananchi kwenda kutibiwa nje ya nchi. 

Aidha, Dkt. Ndugulile aliupongeza uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Jijini Mbeya kwa kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za Afya kwa jamii katika  Hospitali hiyo ikiwemo  upatikanaji wa Dawa ambayo ni zaidi ya Asilimia 90, kuwatambua Wazee na kuwapatia vitambulisha.

“Taarifa niliyoipata katika Mkoa wa Mbeya upatikanaji wa Dawa zote muhimu na za Wazee ni zaidi ya Asilimia 90, na katika Mkoa huu wa Mbeya wamepiga hatua kubwa sana kwa kuweza kuwatambua wazee wengi na kuwapa vitambulisho”, Alisema Dkt. Ndugulile

0 on: "SERIKALI YAENDELEA KUJIZATITI KATIKA KUPAMBANA NA MAGOJWA YASIYO YAKUAMBUKIZA."