Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 23 Januari 2018

SERIKALI YASAINI MKATABA WA UJENZI WA KITENGO CHA DHARURA NA MIFUPA.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Otilia Gowelle kulia akisaini mkataba wa ujenzi wa kitengo cha huduma za Dharura na Mifupa katika Hospitali ya  Benjamin Mkapa uliofanyika kati ya Serikali ya Tanzania na Israel kupitia Wizara ya Afya leo jijini Dar es salaam, kushoto ni Naibu Balozi wa Israel nchini Kenya Bw. Michael Baror.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Otilia Gowelle kulia akibadilishana mkataba wa ujenzi wa kitengo cha huduma za Dharura na Mifupa katika Hospitali ya  Benjamin Mkapa uliofanyika kati ya Serikali ya Tanzania na Israel kupitia Wizara ya Afya leo jijini Dar es salaam na Naibu Balozi wa Israel nchini Kenya Bw. Michael Baror.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Otilia Gowelle akiongea na Waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kusaini mkataba wa ujenzi wa kitengo cha huduma za Dharura na Mifupa katika Hospitali ya  Benjamin Mkapa uliofanyika kati ya Serikali ya Tanzania na Israel kupitia Wizara ya Afya.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Otilia Gowelle kulia akimkabidhi zawadi  Naibu Balozi wa Israel nchini Kenya Bw. Michael Baror. Kushoto wakati wa wakati wa kusaini mkataba wa ujenzi wa kitengo cha huduma za Dharura na Mifupa katika Hospitali ya  Benjamin Mkapa uliofanyika kati ya Serikali ya Tanzania na Israel kupitia Wizara ya Afya.
 Na WAMJW-DAR ES SALAAM

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesaini mkatba wa makubaliano ya ujenzi wa jengo la huduma za dharura na mifupa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo mkoani Dodoma kutoka Serikali ya Israel .

Akizungumza baada ya makubliano  hayo eo jijini Dar es salaam Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Otilia Gowelle amesema kuwa mkataba huo umefanywa na Serikali ya Tanzania na Israel kupitia Wizara ya Afya ili kuboresha huduma za afya nchini. 

"Licha ya kusaini mkatba wa ujenzi wa vitengo hivyo vya huduma za dharura na Mifupa pia Serikali ya Israel imejitolea na kufundisha wataalam wetu katika vitengo hivyo pindi ujenzi utakavyokamilika" alisema Dkt. Gowelle.

Aidha Dkt. Gowelle amesema kuwa anaishukuru Serikali ya Israel kwa kuingia mkataba wa ujenzi huo kwani utasaidia Hospitali hiyo kutoa huduma za dharura kwa ubora na kiwango cha juu kulingana na mahitaj ya wananchi.

Kwa upande wake Naibu Balozi wa Israel nchini Kenya Bw.  Michael Baror amesema kuwa ujenzi huo utakamilika ndani ya  mwaka mmoja na miezi mitatu na kuanza kutoa huduma mara moja.
 

0 on: "SERIKALI YASAINI MKATABA WA UJENZI WA KITENGO CHA DHARURA NA MIFUPA."