Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 16 Machi 2020

FEDHA ZA MWENGE WA UHURU ZITUMIKE KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA - RAIS MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 



FEDHA ZA MWENGE WA UHURU ZITUMIKE KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA- RAIS MAGUFULI

Na Englibert Kayombo - WAMJW, Dar Es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesitisha mbio za Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka huu na kuagiza Fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya Mwenge zitumike kujiandaa kukabiliana na ugonjwa wa Corona.

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo alipokuwa akikagua hatua za ujenzi wa daraja, Ubungo Jijini Dar Es Salaama ambapo ametumia fursa hiyo kuwatahadharisha wananchi juu ya ugonjwa huo wa Corona.

“Tumesikia ugonjwa huu wa corona umeshafika nchi jirani, ugonjwa huu ni hatari na hakuna kinga iliyopatikana mpaka sasa” amesema Rais Magufuli.

“Mwenge wa Uhuru hatutouwasha wala kuukimbiza mpaka tutakapohakikisha tatizo la ugonjwa wa corona limeisha” Amesema Rais Magufuli na kuagiza fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya kukimbiza Mwenge kupelekwa Wizara ya Afya kuongeza nguvu ya kukabiliana na ugonjwa huo.

Rais Magufuli amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ni ishara ya amani na hawezi kuweka maisha ya Watanzania hatarini na ugonjwa huo hasa kwenye mikusanyoko ya watu wengi katika kipindi cha kukimbiza Mwenge wa Taifa.

0 on: "FEDHA ZA MWENGE WA UHURU ZITUMIKE KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA - RAIS MAGUFULI"