Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 7 Desemba 2020

HOSPITALI ZENYE WATAALAM BINGWA ZATAKIWA KUTOA HUDUMA ZA MKOBA KWA WANANCHI WALIO MBALI NA HUDUMA

 

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Makubi akisema jambo kwenye kikao na kamati tendaji ya Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando



Dkt. Caroline Damian Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Tiba anayesimamia Hospitali za Rufaa za Mikoa akisema jambo kwenye kikao na kamati tendaji ya Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Hosptali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa Dkt. Fabian Massaga (aliyesimam) akisema jambo katika kikao kazi cha kamati tendaji ya Hospitali hiyo na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi 


Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi akimpima mapigo ya moyo mgonjwa kwa kutumia kipimo cha Echo-Cadiogram katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando

Na Englibert Kayombo, WAMJW - Mwanza

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi ametoa wito kwa Hospitali zenye wataalam wanaotoa huduma za kibingwa kuwa na huduma za mkoa “Outreach Services” endelevu ili wananchi walio mbali na huduma hizo nao waweze kuhudumiwa karibu na maeneo waliyopo.

Prof. Makubi ametoa amesema hayo akiwa katika ziara ya kikazi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando ambapo alikwenda kujionea hali ya utoaji wa huduma na kuzungumza na viongozi na kamati tendaji ya hospitali hiyo.

“Nitoe wito kwa Hospitali zote za Kanda, Maalum na ya Taifa ambazo tunazo nchini, zianze ama kama wameashaanza waendele kushuka chini kwenda kutoa huduma za mkoba kwenye hospitali zetu” amesema Prof. Makubi

Prof. Abel Makubi amesema kuwa Hospitali hizo zina wajibu wa kuwajengea uwezo wataalam waliopo kwenye Hospitali ngazi ya chini yao kuanzia Hospitali za Rufaa za Mikoa, Wilaya hadi ngazi ya chini ili waweze kutoa huduma kwenye maeneo yao na kuwapunguzia gharama wananchi kwenda umbali mrefu kwa ajili ya kupata huduma za matibabu.

Amesema kuwa wananchi wengi hawapati huduma za kibingwa katika maeneo yao kutokana na kukosokana kwa wataalam hao na pamoja na miundombinu ya vifaa wezeshi vya huduma hizo katika Hospitali za Wilaya hivyo ni vyema wakawa na mipango ya huduma hizo kwenye maeneo ya karibu na wananchi.

Prof. Makubi amesema kuwa huduma za mkoa zinawasaidia pia wataalam waliopo kwenye Hospitali za Wilaya kuongeza ujuzi wa kazi hasa kwenye kuwahudumia wananchi wenye uhitaji wa huduma za kibingwa ambazo hazipatikani kwenye maeneo yao.

Aidha Prof. Makubi ameipongeza Hospitali ya Kanda ya Bugando kwa kuwa na program endelevu ya huduma za mkoa na kuwahimiza wasiache kutoa huduma hizo kwa wananchi huku akizitaka Hospitali nyingine kuiga kutoka hospitali hiyo.

“Watu wanaona umuhimu wa Bugando kwamba ipo pamoja na wao, kwa hiyo ni vizuri na nyie mkatimiza huo wajibu wa kuendelea kushikamana na viongozi kuanzia ngazi ya Mikoa, Wilaya, Vituo vya afya mpaka kwenye zahanati”Amesema Prof. Makubi

Amemtaka Mkurugenzi pamoja na kamati tendaji ya hospitali hiyo na hospitali nyingine za Kanda na Taifa kukaa pamoja kwa muda wa miezi 3 ijayo kuona ni jinsi gani kuziendeleza huduma hizo za mkoba katika Mikoa 8” Amesisitiza Prof. Makubi

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Dkt. Fabian Massaga amesema hospitali hiyo inaendela kutoa na kuboresha huduma zaidi ili wananchi wengi waweze kupata huduma bora katika kanda ya ziwa.

Amesema Hospitali hiyo imekuwa ikitoa huduma za mkoba pamoja na ‘camp’ za huduma za kibingwa kwa wananchi hivyo kuwapunguzia gharama ya kwenda umbali mrefu kufuata matibabu bugando.

Amebainisha kuwa hospitali hiyo katika mwezi huu wa desemba kuazia tarehe 18 itaendesha ‘camp’ ya huduma za upasuaji wa moyo pamoja na upasuaji kwa watoto ambapo wataalam bigwa wa huduma hizo kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Bugando na Daktari kutoka nchi ya Uganda.

0 on: "HOSPITALI ZENYE WATAALAM BINGWA ZATAKIWA KUTOA HUDUMA ZA MKOBA KWA WANANCHI WALIO MBALI NA HUDUMA"