Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 7 Desemba 2020

"WATUMISHI WA AFYA MSHIKIRI KATIKA KUCHANGIA MAENDELEO YA SEKTA YA AFYA" - MGANGA MKUU WA SERIKALI

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi

 


Na WAMJW – Mwanza.

 Mganga mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi amewata watumishi wa afya kushiriki kikamilifu katika kuchangia Maendeleo ya sekta ya afya na si kuiachia Serikali na Jamii pekee.

 

Amesema hayo akiwa kwenye kikao kazi na timu ya uongozi wa afya ndani ya Mkoa wa Mwanza kilichofanyika Wilayani Misungwi kujadali mikakati ya uboreshaji wa huduma za afya mkoani humo.

 

“Kwanini tushindwe kuchangia uboreshaji wa huduma za afya, lazima tuwe na moyo wa kujitoa kuchangia, hizi ni mali zetu sote sisi pamoja na watoto wetu sote tutatibiwa huko” Ni lazima sasa Hospitali zetu zianze kuwa na jicho la kutoa huduma huku zilijenga uwezo wa kifedha na kupunguza utegemezi toka serikali, bila kuathiri huduma kwa wananchi wasio na uwezo wa kulipia.. amesema Prof. Makubi.

 

Amesema hatuwezi kuitegemea Serikali na wafadhili pekee kutuletea Maendeleo ya huduma za afya katika maeneo yetu hivyo na watumishi wanapaswa kushiriki katika kuboresha huduma hizo katika maeneo waliyopo.

 

Aidha Prof. Abel Makubi alitumia nafasi hiyo pia kuendesha shughuli ya michango kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za afya ndani ya Mkoa huo ambapo juma ya Tsh 6,850,000/= fedha ambayo itaenda kutumika katika ujenzi wa jengo kwa ajili ya huduma kwa watoto waliolazwa mahututi (NICU)

 

Prof. Makubi amesema kuwa Mkoa wa Mwanza una uhitaji mkubwa wa huduma hiyo hivyo ufinyu wa eneo katika Hospitali ya Bugando unasababisha watoto walio wagonjwa kukosa huduma kwa wakati.

 

“Hospitali ya Budango inaendelea kupata wingi wa watoto ambao hawajafikia umri wa kuzaliwa na wengi wakiletwa bugando kunakuwa na shida ya kupata eneo la kuwahudumia, kwa michango hiyo itasaidia kuboresha huduma hizo kwa kuongeza eneo” amesema Prof. Makubi

 

Hata hivyo Prof. Makubi amesisitiza suala la uongozi imara kwa viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia taasisi za afya na kuwasisitiza  kuwajibika ipasavyo katika utumishi wao kwa kuhakikisha watumishi walio chini yao wanatoa huduma bora kwa wananchi.

 

Mwisho

0 on: ""WATUMISHI WA AFYA MSHIKIRI KATIKA KUCHANGIA MAENDELEO YA SEKTA YA AFYA" - MGANGA MKUU WA SERIKALI"