Jumatano, 10 Oktoba 2018
DKT. NDUGULILE AAGIZA KUBORESHWA KWA MFUMO WA UKUSANYAJI TAKWIMU NCHINI
Jumatano, Oktoba 10, 2018
-
Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile akisisitiza jambo mbele ya Wadau mbali mbali wa
masuala ya Afya baada ya kufungua mkutano wa masuala mbali mbali ya Afya
uliofanyika jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile akifungua Mkutano wa Wadau mbali mbali wa
masuala ya Afya
uliofanyika jijini Dar es salaam.
Naibu Katibu Mkuu anaeshughulikia masuala ya Afya TAMISEMI Dkt. Zainabu
Chaula akiongea na Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya katika mkutano
uliofanyika jijini Dar es salaam.
Kiongozi Mkuu wa Mkutano wa Masuala ya Afya, hususani
katika mfumo wa upatikanaji na usambazaji wa Dawa, Vifaa tiba na
Vitendanishi Bw. Mavelle Tukai akiwakaribisha Wadau wa masuala ya Afya waliofika katika Mkutano huo uliofanyika jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile akiongea jambo na Mkurugenzi wa Bohari kuu ya Dawa
nchini Bw. Laurean Bwanakunu, katikati ni Afisa mfamasia kutoka Wizara
ya Afya Siana Mapunjo.
Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya wakifuatilia kwa makini mgeni rasmi
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk.
Faustine Ndugulile (hayupo kwenye picha)
DKT. NDUGULILE AAGIZA KUBORESHWA KWA MFUMO WA UKUSANYAJI TAKWIMU NCHINI.
Na WAMJW - Dar es salaam.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile ameagiza kuboreshwa kwa mfumo wa ukusanyaji wa
Takwimu nchini utaosaidia upatikanaji wa takwimu sahihi na zinazifanana
katika taasisi zote.
Ameyasema
hayo mapema wakati akifungua Mkutano wa masuala ya Afya, hususani
katika mfumo wa upatikanaji na usambazaji wa Dawa, Vifaa tiba na
Vitendanishi leo jijini Dar es salaam.
Dkt.
Ndugulile alisema kuwa Serikali inataka kuona mifumo yote ya ukisanyaji
Takwimu inaboreshwa mara moja huku akisisitiza kuwa mifumo hiyo ni
lazima iweze kuwasiliana jambo litalosaidia kupata Takwimu sahihi na
zinazofanana kwa mifumo yote.
"Tunataka
kuona mnaboresha mfumo wa ukusanyaji Takwimu, Takwimu bado ni
changamoto kubwa sana katika utoaji wa huduma za Afya na katika mfumo
mzima wa usambazaji, na ni lazima kuhakikisha kuwa mifumo hii
inawasiliana na inakuwa endelevu" Alisema Dkt. Ndugulile.
Kwa
upande mwingine Dkt. Ndugulile amewaonya watumishi wa Serikali hususani
kutoka Wizara ya Afya wanaokwamisha mawazo endelevu yanayopelekea
kupiga hatua kwa Sekta ya Afya, na kuahidi kuwachukulia hatua endapo
yeyote atabainika kufanya hivo.
"
Muda wowote, mtu yeyote mwenye Mawazo mazuri na Endelevu kwaajili ya
Maendeleo ya Sekta yetu ya Afya, njoo unione Mimi au Waziri wangu,
milango yetu ipo wazi, wengine sisi hatuna urasimu, Serikali hii ya
awamu ya tano haitaki ubabaishaji" Alisema Dkt Ndugulile.
Aidha,
amewaagiza Waganga Wafawidhi wote nchini kuhakikisha wanaandaa orodha
ya Dawa zilizopo kila mwanzo wa wiki ili kusaidia kufahamu orodha ya
Dawa zilizopo na zinazohitajika kwa kipindi hicho, huku akisisitiza
kumchukulia hatua yeyote ataebainika.
"Tumepata
taarifa baadhi ya makampuni ya Dawa yanapita katika Hospitali zetu,
hususani Hospitali kubwa na wanawarubuni Madaktari wetu kuandika kwa MSD orodha ya Dawa ambazo hazipo katika mwongozo wetu wa Serikali,
tutachukua hatua Kali" Alisema Dkt Ndugulile.
Mbali
na hayo Dkt Ndugulile amepiga marufuku Madaktari wote nchini kuandika
Dawa kwa kutumia majina ya bishara na kuwataka kutumia majina ya asili
ya Dawa hizo.
"Jukumu la
Serikali sio kufanya Bishara ya kumtangazia mtu, mfano Panaldo sio jina
lake kitaalamu, ukienda baadhi ya nchi unaweza usikute Panaldo jina lake
halisi ni Parasetamo na ndio linatakiwa litumike" Alisema Dkt
Ndugulile.
Jumanne, 9 Oktoba 2018

MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE YANALETA ULEMAVU
Jumanne, Oktoba 09, 2018
-
Hakuna maoni
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila akifungua semina ya uraghibishaji na uhamasishaji wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa viongozi wa Mkoa na Wilaya kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa Jijini Mbeya.Kulia ni Ofisa mpango toka Wizara ya Afya Osca Kaitaba na mwisho ni Mkuu wa Wilaya ya Kyela Bi.Claudia Kitta.
Ofisa Mpango toka Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Osca Kaitaba akifafanua jambo kwenye semina hiyo.
Wataalam mbalimbali kutoka Sekratariet ya Mkoa wa Mbeya wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa semina ya uraghibishaji na uhamasishaji wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa viongozi na wataalam wa Sekretariet na Mamlaka za Serikali wa Mkoa wa Mbeya.
Ofisa Mpango toka Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Osca Kaitaba akifafanua jambo kwenye semina hiyo.
Wataalam mbalimbali kutoka Sekratariet ya Mkoa wa Mbeya wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa semina ya uraghibishaji na uhamasishaji wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa viongozi na wataalam wa Sekretariet na Mamlaka za Serikali wa Mkoa wa Mbeya.
Na WAMJW - Mbeya
Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yamekuwa yakusumbua na kuleta athari kwa wananchi wa Mkoa wa mbeya hadi kusababisha ulemavu.
Hayo yamesemwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila katika ufunguzi wa semina ya uraghibishaji na uhamasishaji wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa iliyofanyika katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Oktoba 9, 2018.
Alisema Magonjwa hayo yamekuwa yakiathiri zaidi wananchi kwa kiasi kikubwa na kupunguza uwezo wa wananchi katika shughuli za uzalishaji na ujenzi wa taifa.
"Magonjwa haya, pamoja na kusababisha usumbufu mkubwa kwa waathirika pia yanaongeza matumizi ya rasilimali chache tulizonazo katika kuyakabili "alisema Mkuu huyo mkoa.
Aidha Chalamila alisema kwamba uwepo wa magonjwa hayo umefanya watoto kutokuwa na mahudhurio mazuri mashuleni kutokana na muda mwingi kutumika kwenye matibabu.
Hata hivyo alisema kuwa jambo la kutia moyo ni kwamba Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na wadau wamekuwa wakitoa kingatiba za kukinga magonjwa hayo katika mkoa wa Mbeya.
"Hii ni kutokana na lengo la Serikali ya awamu ya tano ambalo ni kudhibiti magonjwa haya na hivyo kupunguza gharama kwa wananchi kwa kugawa kingatiba hizo"Alisisitiza Chalamila
Akielezea zaidi Chalamila alisema Mkoa wa Mbeya walikuwa wanakabiliwa na magonjwa yote matano ambayo ni minyoo ya tumbo, kichocho, matende na mabusha katika Wilaya zote ila kutokana na usimamizi na uhamasishaji nzuri Mkoa wake hivi sasa wamepunguza magonjwa hayo na hivyo kuwataka viongozi wa mkoa na Wilaya zake kuzidi kuhamasisha na kuelimisha zaidi wananchi kujitokeza kumeze kingatiba ili kutokomeza magonjwa hayo.
Aliyataja magonjwa yanayoendelea kuwa changamoto kwa Wilaya za Mkoa wa Mbeya ukiwemo ugonjwa wa Trakoma kwa Wilaya za Kyela, Chunya na Mbarali pamoja na ugonjwa wa usubi kwa Wilaya za Rungwe, Kyela na Busokelo.
Kwa upande wake Ofisa Mipango kutoka Mpango wa Kudhibiti Magonjwa Yasiyopewa Kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bwana. Oscar Kaitaba alisema semina hiyo imejumuisha wajumbe kutoka Halmashauri tatu za Mkoa wa Mbeya ambazo ni Rungwe, Kyela, Busokelo.
Aidha Bw. Kaitaba alitaja wajumbe hao kuwa Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Waweka Hazina za Wilaya, Waganga Wakuu Waratibu pamoja na Maafisa Usalama wa Wilaya.
Mwisho.
Jumatatu, 8 Oktoba 2018
Jumapili, 7 Oktoba 2018
WATANZANIA WAASWA KUPIMA MACHO MARA KWA MARA.
Jumapili, Oktoba 07, 2018
-
Hakuna maoni
Washiriki kutoka taasisi
mbalimbali za serikali na sekta binafsi wakiwa katika maandamano kuadhimisha
wiki ya afya ya macho yaliyofanyika jijini Dodoma mapema leo
|
Mganga Mkuu Wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Charles Kiologwe akisisitiza jambo katika
uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya afya ya macho uliofanyika katika viwanja vya
Nyerere jijini Dodoma mapema leo.
|
Jumamosi, 6 Oktoba 2018

WATOA HUDUMA ZA AFYA WATAKIWA KUTOWASAHAU WATOTO KATIKA KUWAKINGA NA MAAMBUKIZI YA VVU.
Jumamosi, Oktoba 06, 2018
-
Hakuna maoni
Ijumaa, 5 Oktoba 2018
WAZIRI UMMY AUAGIZA UONGOZI WA HOSPITALI YA ST. FRANCIS KUSHUSHA BEI ZA MATIBABU MARA MOJA.
Ijumaa, Oktoba 05, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
amwalimu akikagua vifaa vya moja ya kati ya wagonjwa waliopata Rufaa ya
kwenda kutibiwa katika Hospitali ya St. Francis pindi alipofanya ziara
ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika kituo cha Afya cha
Kibaoni.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akimjulia hali mtoto aliefika na mama yake kupata huduma katika
kituo cha Kibaoni.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya viongozi wa Mkoa wa
Morogoro walioongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ifakara James Lihunyo (hayupo
kwenye picha)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikagua cheti cha mgonjwa katika kituo cha
Afya cha Kibaoni wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji
huduma kisha kuelekea Hospitali ya Rufaa ya St. Francis.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akimjulia hali mtoto aliefika na mama yake kupata huduma katika
kituo cha Kibaoni.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jisnsia, Wazee na
Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akieleza umuhimu wa Bima ya Afya kwa watoto kwa
mmoja kati ya wamama waliofika kupata huduma za Afya katika kituo cha
Afya cha Kibaoni.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa maelekezo kwa Baba Askofu wa jimbo la
Ifakara Salutaris Libenaambae baada ya kikao cha kuboresha hali ya
utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.
Upande wa mbele wa Hospitali ya Rufaa ya St. Francis.
WAZIRI UMMY AUAGIZA UONGOZI WA HOSPITALI YA ST FRANCIS KUSHUSHA BEI ZA MATIBABU MARA MOJA.
Na WAMJW - IFAKARA
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
ameuagiza uongozi wa Hospitali ya Dini ya St.Francis kupunguza gharama
za matibabu kwa wananchi ndani ya mwezi mmoja kabla hajarudi kufanya
ukaguzi wa mara ya pili.
Ameyasema
hayo wakati akiwa katika ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya
katika Hospitali ya St Francis iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Ifakara
Mkoa wa Morogoro kufuatia taarifa isiyoridhisha juu ya gharama za
matibabu iyoripotiwa siku ya Octoba 3 na Televisheni ya Taifa (TBC).
Waziri
Ummy alisema kwamba, Serikali inatoa Jumla ya Watumishi 243 sawa na
Asilimia 68% katika Hospitali hiyo, lengo ni kuwasaidia wananchi wa
kipato cha chini kupata huduma za bora za afya na zenye unafuu ikiwa ni
moja kati ya ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
John Pombe Magufuli wakati anaingia madarakani.
"Kati
ya Watumishi 352, watumishi 219 wanalipwa mshahara na Serikali Kuu,
ambapo kila mwezi tunalipa shilingi milioni 153.7, bila kuhesabu gharama
za watumishi 12 walioshikizwa kutoka Wizara ya Afya, Watumishi 12
kutoka Halmashauri ya Kilombero, Katibu tawala Morogoro ameleta
watumishi 2, jumla watumishi 243, ambao ni sawa na Asilimia 68%
wanalipwa mshahara kutoka Serikali kwa Asilimia 100%". Alisema Mhe. Ummy
Mwalimu.
Waziri Ummy
aliendelea kusema kuwa mwaka wa bajeti 2015/2016 Serikali ilipeleka dawa
zenye thamani ya shilingi Millioni 119.5, bajeti ya mwaka 2016/2017
shilingi milioni 177.9 huku kwa mwaka 2017/2018 dawa zenye thamani ya
shilingi milioni 118.7 zilinunuliwa hospitalini hapo.
Kwa
upande mwingine Waziri Ummy alisema kuwa mwongozo wa Wizara ya Afya,
unazitaka Hospitali zote kuhakikisha kuwa wanawake wajawazito, wazee
wasio na uwezo na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kupata
huduma za matibabu bila malipo.
Mbali
na hayo Waziri Ummy alitoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Morogoro
kujiunga na mifuko ya Bima ya Afya bila kuwasahau watoto walio chini ya
umri wa miaka 18 ambao hupata bima ya afya kwa shilingi 50,400/=
"Wakati
umefika wa Watanzania kujenga utamaduni wa kuwa na uhakika wa matibabu
kabla ya kuugua, na uhakika huo ni wa kupitia Bima ya Afya", alihimiza
Waziri Ummy kwa msisitizo.
Waziri
Ummy, aliendelea kusema kuwa, Serikali inaelekea kutunga sheria ambayo
itamlazimu kila Mtanzania kupata Bima ya Afya, ili aweze kupata huduma
za matibabu ya Afya bila kikwazo chochote cha fedha.
Naye
Mbunge wa Jimbo la Kilombero Mhe. Peter Ambrose Lijualikali amemuomba
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu kuikumbuka Halmashauri ya Wilaya ya
Kilombero kwa kujenga Hospitali ya Wilaya, jambo litaloimarisha hali ya
utoaji huduma za Afya kwa wananchi.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Hospitali ya St. Fransis, Baba Askofu Salutaris Libena
ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kufika hospitali hapo na
kuahidi kutekeleza maelekezo yote ambayo yametolewa na Serikali.
"
Tunaahidi kwamba tumeelewa na tutatekeleza maelekezo yote, katika lengo
la kuboresha huduma za Afya kwa wananchi ", alisema Baba Askofu Libena.

SERIKALI YANUNUA MA SHINE ZA MIONZI ZENYE THAMANI YA BILIONI 1.7
Ijumaa, Oktoba 05, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
akionesha baadhi ya mashine za mionzi 10 zilizonunuliwa na Serikali
zenye thamani ya shilingi bilioni 1.7 na kusambazwa kwenye Hospitali za
Rufaa za Mikoa.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt.Mashack
Shimwela,akiongea na waandishi wa habari baada ya kupokea mashine
hizo(picha zote na Wizara ya Afya
Waziri Ummy akiongea na vyombo vya habari wakati wa kupokea mashine hizo
za mionzi (digital X-ray) ambazo zitaboresha huduma za afya nchini
hususani za uchunguzi wa mionzi
SERIKALI YANUNUA MA SHINE ZA MIONZI ZENYE THAMANI YA BILIONI 1.7
Na.WAMJW, Dar es Salaam
Serikali
kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
imenunua mashine za Mionzi (digital X-ray) zipatazo kumi zenye thamani
ya shilingi bilioni 1.7.
Hayo yamesemwa leo na
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
wakati akipokea mashine hizo kwenye Bohari ya Dawa(MSD) jijini hapa.
Waziri
Ummy amesema kuwa Serikaki inaendelea kutoa kipaumbele katika kuboresha
huduma za afya nchini ikiwa ni lengo la kuhakikisha huduma za afya
zinawafikia watanzainia wote karibu na maeneo wanayoishi.
"Maendeleo
ya Taifa letu la Tanzania yataletwa na wananchi wenye afya na wenye
uwezo wa kuzalisha mali,hivyo tunaboresha na kuimarisha huduma za tiba
na uchunguzi wa magonjwa katika hospitali zetu kuwa na vifaa vya kisasa
zaidi na kuondokana na utaratibu wa kupeleka wagonjwa nje ya
nchi".Alisema,Waziri Ummy Mwalimu.
Alisema
mashine hizo zitapelekwa kwenye hospitali za rufaa za mikoa 10 ambazo
X-ray za zamani zimekwisha muda wake na zimekua zikiharibika mara kwa
mara.
Alizitaja hospitali hizo ni Amana, Bukoba, Katavi,Morogoro,Njombe,Ruvuma, Simiyu na Singida pamoja na hospitali za Wilaya ya Magu na Nzega.
Aidha,Waziri
Ummy alisema katika bajeti ya mwaka 2018/2019, Wizara yake imepanga
kununua mashine za mionzi nyingine zipatazo ishirini na nne(24) zenye
thamani ya shilingi bilioni 4.1 ambazo zitapelekwa kwenye hospitali za
rufaa za Mikoa na Wilaya ambazo hazina au zina X-ray za kizamani au
chakavu.
Akizungumza kwa niaba ya Waganga Wakuu
wa hospitali zinazopelekwa mashine hizo,Mganga Mkuu wa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Amana Dkt.Mashack Shimwela alisema ujio wa mashine hizo
za kisasa zitasaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa uchunguzi za
mionzi pia utunzaji wa mazingira tofauti na aina zilizokuwa zikitumika
mwanzo
Aidha,alisema mashine hizo zina ubora wa
picha pia ina mifumo ya Tehama ambayo ni rahisi kusomwa hata nje ya
hospitali husika endapo hakuna msoma picha
DKT. NDUGULILE AHIMIZA USHIRIKIANO WENYE MATOKEO YANAYOONEKANA BAINA SEKTA BINAFSI NA SEKTA ZA SERIKALI
Ijumaa, Oktoba 05, 2018
-
Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile akiongea na Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya,
kutoka Sekta Binafsi na Sekta za Serikali wakati wa ufunguzi wa mkutano
wa pili wa mwaka wa Sekta Binafsi na Sekta za Serikali.
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akimkaribisha Mgeni
rasmi katika Mkutano wa pili wa mwaka wa masuala ya Afya jlioshirikisha
Sekta Binafsi na Sekta za Serikali leo jijini Dar es salaam.
Mwakilishi Kutoka Sekta Binafsi Bw. akiongea na Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya,
kutoka Sekta Binafsi na Sekta za Serikali wakati wa ufunguzi wa mkutano
wa pili wa mwaka wa Sekta Binafsi na Sekta za Serikali.
Wadau mbali mbali kutoka Sekta Binafsi na Sekta za Serikali walioshiriki
katika Mkutano wa pili wa mwaka wa Masuala ya Afya uliofanyika katika
ukumbi wa Bank Kuu ya Tanzania (BoT) leo jijini Dar es salaam
Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile baada ya kufungua Mkutano wa pili wa mwaka wa masuala ya Afya jlioshirikisha
Sekta Binafsi na Sekta za Serikali leo jijini Dar es salaam.
DKT. NDUGULILE AHIMIZA USHIRIKIANO WENYE MATOKEO YANAYOONEKANA BAINA SEKTA BINAFSI NA SEKTA ZA SERIKALI.
Na WAMJW- Dar es salaam
NAIBU
WAZIRI Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile amehimiza ushirikiano wa karibu wenye tija na matokeo
yanayoonekana baina ya Sekta Binafsi na Sekta za Serikali katika kuleta
Maendeleo chanya kwa wananchi.
Amesema
hayo mapema leo wakati akifungua mkutano wa pili wa mwaka wa Sekta
binafsi na Sekta ya Serikali uliofanyika katika ukumbi wa Bank kuu ya
Tanzania (BoT) jijini Dar ea salaam.
Dkt.
Ndugulile alisema kuwa katika kuboresha Sekta ya Afya nchini, Serikali
inahitaji ushirikiano wa karibu na Sekta Binafsi ili kurahisisha utoaji
wa Huduma za Afya kwa wananchi, huku akisisitiza matokeo yanayoonekana
katika ushirikiano wa pande hizo .
"Kusudio
la Serikali ni jema kabisa, na ndomana tumeweka Sera na Sheria, sisi
kama Serikali hatuwezi kuyafanya yote, tunahitaji Sekta ya Binafsi
tushirikiane, Serikali iliyopo saivi madarakani inataka matokeo, hatupo
hapa kukutana kila mwaka wakati hatuna mradi ulioshirikisha pande zote"
alisema Dkt. ndugulile.
Kwa
upande mwingine Dkt. Ndugulile ameagiza watumishi wote wa Sekta ya Afya
nchini kuacha ubabaishaji pindi Sekta Binafsi zinapohitaji ushirikiano
katika kuleta Maendeleo kwa wananchi na kuagiza kumchukulia hatua yeyote
atakaebainika kutenda kosa hilo.
"Niwaombe
sana wafanyakazi wenzangu wa Sekta ya Serikali tuache urasimu,
tuangalie jinsi gani yakurahisisha ushirikiano ili mawazo mazuri yalete
Maendeleo, tunataka kuwekeza katika viwanda, bado tunahitaji Huduma
zakibingwa, watu wapo tayari, nataka tuache vikwazo", alisema Dkt
Ndugulile
Pia, Dkt
Ndugulile alitoa ushauri kwa Afisa Tabibu juu ya namna yakudhibiti
matumizi ya fedha nyingi ambayo yanatumika kununua vifaa vya matibabu na
mashine za maabara na thieta kwa kutoa fursa kwa Sekta Binafsi kununua
na kuendesha mashine hizo huku Serikali ikijikita katika kutoa Huduma
zilizo bora kwa wananchi.
"Sioni
sababu ya Serikali kuingia gharama za kununua vifaa vya kutibu, maabara
na thieta, kwanini tusiweke utaratibu wa watu wa Sekta Binafsi,
wawekeze kwenye vifaa, sisi kama Serikali tujikite katika kutoa Huduma,
itatusaidia sana sisi kutoa Huduma bora" alisema Dkt Ndugulile.
Dkt.
Ndugulile aliendelea kusisitiza kwamba , Sekta Binafsi si washindani
wala maadui wa Sekta za Serikali hivyo ni lazima kuhakikisha ushirikiano
unakuwa katika kutoa Huduma bora kwa wananchi, hivyo kutoa mwanya kwa
yoyote mwenye wazo zuri ikiwemo ujenzi wa viwanda vya dawa kuleta wazo
hilo ofisini kwake na kuahidi kulitekeleza Mara moja.
Sambamba
na hilo Dkt Ndugulile alisema kuwa Serikali imedhamiria kuja na Sera
ambayo itamtaka kila Mtanzania kuwa na Bima ya Afya ili aweze kupata
Huduma za Afya, hivyo kuwataka Sekta Binafsi kuja na mawazo jinsi gani
inaweza kushiriki katika kufanikisha wazo hili.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)







