Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 28 Julai 2019

4% YA WANANCHI WAAMBUKIZWA VIRUSI VYA HOMA YA INI

Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika akitembelea moja ya banda la kufanyia uchunguzi  wakati wa maadhimisho ya siku ya homa ya ini yaliyofanyika leo  katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma, kushoto  kwake ni Mkurugenzi wa Epidemiolojia kutoka Wizara ya Afya Dkt. Janneth Mghamba.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika akiwajulia hali baadhi ya watu waliojitokeza kufanya  uchunguzi homa ya ini, katika  maadhimisho ya siku ya homa ya ini yaliyofanyika leo  katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma, Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Epidemiolojia kutoka Wizara ya Afya Dkt. Janneth Mghamba.

Wadau mbali mbali wa Afya wakifuatilia kwa makini taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika wakati wa maadhimisho ya siku ya homa ya ini yaliyofanyika leo  katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika akiteta jambo na mwakilishi wa WHO Dkt. Christine Chakanyuka Musanhu  wakati wa maadhimisho ya siku ya homa ya ini yaliyofanyika leo  katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika akisisitiza jambo wakati wa maadhimisho ya siku ya homa ya ini yaliyofanyika leo  katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma, kushoto ni Mkurugenzi wa Epidemiolojia kutoka Wizara ya Afya Dkt. Janneth Mghamba, na Kulia ni mwakilishi wa WHO anaitwa Dr. Christine Chakanyuka Musanhu

Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Alphonce Chandika katika picha ya pamoja na Wadau pamoja na Watumishi wa Sekta ya Afya, wakati wa maadhimisho ya siku ya homa ya ini yaliyofanyika leo  katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma.


4% YA WANANCHI WAAMBUKIZWA VIRUSI VYA HOMA YA INI

Na WAMJW-DOM

Mkurugenzi wa Hospitali ya Benjamini Mkapa Dkt. Alphonce Chandika amesema kuwa miongoni mwa Watanzania wenye umri kati ya miaka 15-49 wameabukizwa Virusi vya Homa ya Ini aina ya B, hii ni kutokana na Takwimu za Ofisi ya Taifa wa Takwimu 206-2017.

Dkt. Alphonce Chandika amesema hayo leo wakati wa Siku ya Homa ya Ini Duniani ambayo, yenye kauli mbiu ya “Wekeza katika mapambano ya Homa ya Ini “ maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika Jijini Dodoma katika Hospitali ya Benjamini Mkapa.

“kati ya wachangiaji damu 307,835 takribani watu 13,613 sawa na asilimia 4.4 walikuwa na maambukizi ya homa ya ini kwa mujibu wa takwimu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS)” alisema Dkt. Alphonce Chandika.

Dkt. Alphonce Chandika  aliendelea kusema kuwa Mwaka 2017, kati ya wachangiaji damu 233,953 takribani watu 11,417 sawa na asilimia 4.9 walikuwa na maambukizi, aidha asilimia 0.5 ya wachangiaji damu walikuwa na maambukizi ya homa ya ini aina ya C kwa mwaka 2017 na asilimia 0.3 kwa mwaka 2018.

Aidha, Dkt. Alphonce Chandika alisisitiza juu ya kutoa elimu ya kutosha kwa Wananchi juu ya athari za ugonjwa wa  Homa ya Ini katika jamii na kwa nchi kwa ujumla, huku akisisitiza kuwa Serikali itaokoa kiasi kikubwa  cha fedha kama  itawekeza nguvu kwenye kinga, ambacho kinachotumika kwenye matibabu dhidi ya ugonjwa huu wa homa ya ini.

Nae, Mkurugenzi msaidizi wa Epidemiolojia kutoka Wizara ya Afya Dkt. Janneth Mghamba amesema kuwa huduma  hii ya chanjo ya homa ya Ini imeanza kutolewa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa za Sokoture Mwanza,Hospitali ya Rufaa ya Mawenzi Kilimanjaro, Hospitali ya Rufaa ya Geita, Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Hospitali ya Temeke, Hospitali ya Mwananyamala, Hospitali ya Rufaa ya Morogoro, Hospitali ya Rufaa ya Iringa, Hospitali ya Muimbili, Moi, Ocean Road  na vituo vyote vya mipakani.

Mwisho.

0 on: "4% YA WANANCHI WAAMBUKIZWA VIRUSI VYA HOMA YA INI"