Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 11 Julai 2019

SERIKALI YASHUSHA NEEMA KWA WANANJOMBE

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka wakiongea na Wazee waliofika kupata huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe wakati alipofanya uzinduzi wa huduma  za Afya katika Hospitali hiyo.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa maelekezo kwa uongozi wa Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe  wakati alipotenbelea kukagua chumba cha kuhifadhia Dawa katika Hospitali hiyo, wakatikati (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikagua kadi inayoonesha kiasi cha dawa kilichopo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe pindi alipofanya ziara ya kuzindua Huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akieleza juu ya umuhimu wa kuwepo kwa mabango yanayohamasisha haki ya mgonjwa kupata  huduma  za Afya zilozo Bora wakati wa  uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, kushoto kwake (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimjulia hali moja kati ya wagonjwa waliofika kupata matibabu kwa mara ya kwanza katika Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, ni baada ya kufanya  uzinduzi wa  huduma za Afya katika Hospitali hiyo, Kulia kwake (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka wakati wa uzinduzi wa Huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akipanda mti wa matunda (mpalachichi) ikiwa ni ishara ya kuhifadhi mazingira, shughuli iliyofanyika baada ya uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka akipanda mti wa matunda (mpalachichi) ikiwa ni ishara ya kuhifadhi mazingira, shughuli iliyofanyika baada ya uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ulioongozwa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikabidhi ramani ya ujenzi wa majengo mengine mapya saba  kwa Mkandarasi, shughuli iliyofuata baada ya uzinduzi  wa huduma katika Hospitali hiyo ya Rufaa  ya Mkoa wa Njombe.

Moja kati ya vyumba vya Wagonjwa kilicho na vitanda pamoja na mashine zakutambua hali ya Mgonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, iliyoanza kutoa huduma rasmi Julai 10, baada ya Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kufanya uzinduzi huo

Wananchi waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ulioongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka (Hawapo kwenye picha)

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka baada ya uzinduzi  wa huduma katika Hospitali hiyo ya Rufaa  ya Mkoa wa Njombe.



Na WAMJW-NJOMBE

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeshusha neema kwa Wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kutoa kiasi cha shilingi Bilion 7.6 kwaajili ya ujenzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ili kuboresha huduma kwa Wananchi.

Hayo yamejiri leo wakati wa zoezi la Uzinduzi wa huduma za Afya na lililoongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe iliyofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Katika uzinduzi huo, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma za Afya katika Mkoa wa Njombe ikiwemo kujenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, jengo la maabara, jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji gorofa mbili, wodi za wagonjwa gorofa tatu, nyumba za Watumishi tano, pamoja na kichomea taka.

" Tunajenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, tunajenga jengo la jengo la maabara, tunajenga jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji gorofa mbili, tunajenga wodi za wagonjwa gorofa tatu, tunajenga jengo la kufulia, tunajenga kichomea taka na tunajenga nyumba za watumishi tano" alisema Waziri Ummy.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi wa Hospitali hiyo kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa majengo hayo hayo ndani ya miezi kumi ili wananchi wa Mkoa wa Njombe waanze kufaidika na huduma za Afya katika Hospitali hiyo, huku akiwatoa hofu wananchi kuwa pesa zote zipo tayari.

Mbali na hayo, Waziri Ummy mewaasa Wananchi kupambana dhidi ya magonjwa yasiyo yakuambukiza kama Kisukari, shinikizo la damu, Saratani na magonjwa ya Moyo kwa kubadilisha mtindo wa maisha ikiwamo ulaji mlo sahihi , kuacha uvutaji wa sigara na tumbaku, kuacha unywaji wa pombe kupita kiasi pamoja na kutofanya mazoezi mara kwa mara.

Aidha, Waziri Ummy ametoa with kwa vijana kujiepusha na mambo ambayo yatapelekea kipata maambukizi ya VVU, huku akiweka wazi kuwa maambukizi mapya ya VVU ni 82,000 kila mwaka nchini Tanzania, huku katika kila watu 100, watu 40 ni vijana wenye umri kati ya 15 hadi 24 umri ambao ni nguvu kazi ya taifa.

"Tunatambua kwamba kuna maambukizi makubwa ya virusi vya Ukimwi Mkoani Njombe,lazima tuzingatie kanuni za kujikinga na maambukizi ya VVU, kujizuia kufanya mapenzi kwa vijana hasa kwa wasichana ambao muda wao haijafika, pili kuwa mwaminifu kwa mwenza wako au mpenzi wako na tatu kutumia kinga" alisema Waziri Ummy

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka amewatoa hofu wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kuweka wazi kuwa huduma za Afya katika Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe haitoathiri utoaji huduma katika Hospitali ya Kibena iliyokuwa Hospitali ya Mkoa, ambayo kwa sasa imerudishwa chini ya Halmashauri ya Mji wa Njombe.

"Na mimi ntahakikisha wale Watumishi ambao tilikubaliana waje kwenye Hospitali hii, waje na nguo zao , vifaa vyote waviache Kibena na huduma ya Kibena iendelee, na kazi ya Hospitali hii Mhe. Ummy Mwalimu na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wataweka vifaa vyote vitakavyohitajika na huduma zitaendelea" alisema Mhe. Olesendeka

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Mhe. Edwirn Mwanzinga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kupitia Wizara ya Afya kwa kuongeza bajeti ya dawa na vifaa tiba jambo linalosaidia kuokoa kwa kiasi kikubwa maisha ya Wananjombe.

Mwisho.

0 on: "SERIKALI YASHUSHA NEEMA KWA WANANJOMBE"