Alhamisi, 19 Julai 2018
Ijumaa, 13 Julai 2018

MARUFUKU KUAJIRI WATOA HUDUMA NGAZI YA JAMII NJE YA ENEO HUSIKA.
Ijumaa, Julai 13, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akiongea na
Wananchi wa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu wakati wa ufunguzi wa mradi
wa Tuwatumie ambao unawaajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii katika
vijiji vyote vya halmashauri hiyo chini ya ufadhili wa AMREF
Wadau mbalimbali wa sekta ya afya walifuatilia hotuba ya mgeni
rasmi(hayupo pichani) aliyekaa kushoto ni Niall Morris Mkuu wa Arish
Aid,Dar.Aisa Muya -Kaimu Mkurugenzi Mkazi Amref Tanzania(katikati) na
kulia ni Dkt.Helen Senkoro Mkurugenzi wa Benjamin Mkapa Foundation
Wananchi waliojitokeza kushuhudia ufunguzi wa mradi huo ambapo watoa
huduma hao watakua kiungo kati ya wananchi na vituo vya kutolea huduma.
Waziri Ummy Mwalimu akifungua mradi huo
MARUFUKU KUAJIRI WATOA HUDUMA NGAZI YA JAMII NJE YA ENEO HUSIKA.
NA WAMJW-SIMIYU.
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imepiga marufuku kuajiri watoa huduma wa afya ngazi za jamii kutoka nje ya Halmashauri husika.
Katazo
hilo limetolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa mradi wa TUWATUMIE
uliofanyika mkoani Simiyu wilaya ya Itilima.
"Nataka
kuwaambia viongozi wa Mkoa na Wilaya nchi nzima pamoja na taasisi
zisizo za kiserikali ni marufuku kuajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii
(CHW) kutoka nje ya makazi yao ili kusiwe na kutotofautiana
kimazingira,kwani wenyeji wanajua tamaduni na mila za wakazi wanapotoka"
alisema Waziri Ummy.
Waziri
Ummy amesema kuwa watoa huduma ngazi ya jamii wanatakiwa kuwa
kipaumbele katika kukinga kuliko kutoa tiba ili kupunguza idadi ya
wagonjwa na kuokoa fedha.
"Nataka
kuwaambia wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanatakiwa kuweka kipaumbele
kinga kuliko tiba kwani mimi ni Waziri wa Afya na sio Waziri wa
wagonjwa,siwezi kusubiri watu wale ,nitawatumia CHW kuwakinga ama
kuwazuia wanaoumwa kupata matibabu" alisema Waziri Ummy.
Alisema
nchi ipo kwenye mikakati ya kufikia malengo endelevu ya millennia ya
kumfikia kila mtanzania kwa wakati na popote,hivyo kwa kuanza CHW
wanaanza eneo la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania Dkt. Aisa Muya
amesema kuwa asilimia 50 ya miradi yao wanatumia watoa huduma za afya
ngazi ya jamii .
Aidha,
Dkt. Muya amesema kuwa wametoa mafunzo kwa watoa huduma 2,265 na mradi
huo utawaajiri watoa huduma 2,015 mbapo Wilaya ya Itilima watakuwa 102
na Misungwi 113 ambao wataenda kwenye vijiji vyote vya wilaya hizo.
Dkt.
Muya amesema kuwa matarajio ya mradi huo ni kuwatumia watoa huduma hao
kama kiungo kati ya jamii na vituo vya kutolea huduma za afya.

TAARIFA KWA UMMA
Ijumaa, Julai 13, 2018
-
Hakuna maoni
JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA
WIZARA YA AFYA,
MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
KUITWA KAZINI
Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda kuwataarifu wote
walioomba nafasi mbalimbali za Ajira za Kada ya Afya tarehe 11 Mei
hadi 26 Mei, 2018 kuwa walioorodheshwa katika tangazo hili wamechaguliwa na kupangiwa
vituo vya kazi kama jedwali linavyoonyesha kwenye Tovuti ya Wizara ya Afya www.moh.go.tz.
Waombaji
waliochaguliwa wanatakiwa kuzingatia kwa
ukamilifu maelekekezo yafuatayo:
1). Kuripoti Ofisi za Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto
Dodoma katika muda wa siku kumi na
nne (14) kuanzia tarehe ya tangazo hili,
kwa ajili ya kukamilisha taratibu za Ajira Serikalini. Ambao hawataripoti ndani ya siku kumi na nne
(14) nafasi zao zitajazwa na waombaji wengine wenye sifa. Aidha, wakati wa kuripoti kila aliyechaguliwa
atapaswa kuwasilisha vyeti halisi (Original Certificates) ambavyo nakala zake zilitumiwa
wakati wa kuomba ajira zao, ikiwa pamoja na:-
a)
Vyeti halisi vya Elimu
ya Sekondari, Vyeti vya Taaluma, Usajili wa Baraza/Bodi ya Kitaaluma na cheti
cha kuzaliwa.
b)
Nakala ya picha mbili
ndogo (passport size). Picha ziwe na muonekano kamili wa sura na ziwe zimepigwa
si zaidi ya miezi mitatu iliyopita.
2) Waombaji wote ambao
majina yao hayakuonekana
katika tangazo hili watambue
kuwa hawakupata nafasi hiyo, hivyo wanashauriwa wasisite kuomba mara
nafasi nyingine za
kazi zitakapotangazwa.
3) Waombaji
waliopangiwa Kada ya Uhudumu wa Afya
majina yao yatatangazwa baadae.
Imetolewana:
Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini - Afya
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, WAZEE NA WATOTO
13
Julai, 2018
Alhamisi, 12 Julai 2018

SERIKALI KUFUTA TOZO YA USAJILI,KUHUWISHA NA KUSHIKILIA USAJILI KWA WAWEKEZAJI WA NDANI.
Alhamisi, Julai 12, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee
na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akikagua shughuli za ujenzi wa jengo la
wodi ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure wakati
alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo hilo jijini Mwanza.
Waziri wa afya,Maendeleo ya
jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akipata maelezo kutoka
kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kushoto wakati
alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo la Mamlaka hiyo jijini
Mwanza. Kulia ni Mkurugenzi wa Ubora wa Huduma za Afya kutoka Wizara ya afya
Dkt. Mohammed Mohammed.
Waziri wa afya,Maendeleo ya
jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akipata maelezo juu ya
sukari zinazopimwa ubora wake kutoka kwa
Mkuu wa Maabara wa TFDA Kanda ya Ziwa
Bw. Salum Kindoli wakati alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo la
Mamlaka hiyo jijini Mwanza.
Waziri wa afya,Maendeleo ya
jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akipata baadhi ya maelezo kutoka kwa
Mkurugenzi wa Ubora wa Huduma za Afya kutoka Wizara ya afya Dkt. Mohammed
Mohammed kushoto wakati alipotembelea kukagua shughuli za ujenzi wa jengo la
Mamlaka hiyo jijini Mwanza.
Baadhi ya mafundi wakiendelea na
shughuli za ujenzi wa wa jengo la wodi
ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure
jijini Mwanza.
SERIKALI
KUFUTA TOZO YA USAJILI,KUHUWISHA NA KUSHIKILIA USAJILI KWA WAWEKEZAJI WA NDANI.
NA
WAMJW-MWANZA
SERIKALI kupitia wizara ya
afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imefuta tozo ya usajili ,
kuhuwisha pamoja na kushikilia usajili wa bidhaa zao kwa wawekezaji wa ndani
kupitia Mamlaka ya chakula na Dawa TFDA .
Hayo yamesemwa na Waziri wa
Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati
alipotembelea kuangalia ujenzi wa jengo la TFDA ambalo linajengwsa Jijini
Mwanza ili kusogeza huduma kwa wananchi wa mkoa huo.
“Ili kuunga mkono juhudi za Rais Dkt.
John Pombe Magufuli za kukuza nchi kupitia uchumi wa viwanda hivyo TFDA msiwe
kikwazo kwa wawekezaji hao hivyo kuanzia leo nafuta tozo za kusajili
bidhaa,kuhuwisha bidhaa na tozo ya kushikilia usajili wa bidhaa”, alisema
Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa kuendana
na juhudi hizo pia Serikali imefuta tozo
ya udhibiti ya thamani ya 0.25 za
dawa,vifaa na vifaa tiba zinazoingizwa kwenye hospitali za Umma kutoka kwa
wafadhili.
Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa
TFDA ina wajibu wa kusimamia Tanzania isiwe jalala la bidhaa zisizo na ubora
kwa watanzania hivyo wanatakiwa kuweka afya ya wananchi mbele kuliko manufaa
binafsi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa
TFDA Bi. Agness Kijo amesema kuwa ujenzi wa jengo hilo ukikamilika utasaidia
kuhudumia huduma za kimaabara kwa bidhaa zinazoingia nchini kwani itakuwa sio
lazima tena kwenda kupima bidhaa hizo jijini Dar es salaam.
“Maabara hizi zikikamilika zitasaidia
kufanya vipimo na udhibiti wa bidhaa katika mipaka mingi ya kanda ya ziwa
ikiwemo Silali,Lusumo na Mtukula ili kuweka usalama wa bidhaa zinazoingia na
kutoka nje ya nchi kwa usalama wa wananchi.
Sambamba na hilo Waziri Ummy alipata
nafasi ya kutembelea kukagua ujenzi wa jengo la wodi ya mama na mtoto katika
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure na kuhakikisha ujenzi
unakamilisha ili kuokoa vifo vya mama na mtoto vinavyotokana na uzazi.
“Kama watu wa mwanza wanaridhishwa na
huduma zinazotolewa katika hospitali hii basi ni lazima huduma za afya
ziboreshwe ikiwemo afya ya mama na mtoto hivyo ninaleta mashine ya CT Scan kwa
ajili ya kuboresha matibabu hapa” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy aliwataka watendaji wa
Hospitali kutoa taarifa za utendaji kwa
Waziri wa Afya na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo pamoja na kusimamiwa na Wakuu wa
Mikoa yao ili kuimarisha huduma za afya nchini.
Jumatatu, 9 Julai 2018
WILAYA 58 ZAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA TRAKOMA
Jumatatu, Julai 09, 2018
-
Hakuna maoni
Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Dkt. Leonard Subi akifungua Mkutano wa mafunzo wa nchi 21 ambazo
zina maambukizi ya Ugonjwa wa Trakoma (Vikope) uliofanyika katika jiji
la Arusha.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Timothy Wonanji akiongea na Wadau
kutoka nchi mbali mbali wa magonjwa ya Trakoma(Vikope) katika kikao
kilichofanyika jijini Arusha huku lengo likiwa kuhimarisha mkakati wa
namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi
katika nchi hizo 21.
Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele chini ya
Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazeee na watoto Dkt .
Upendo Mwingila akionga kwa kifupi juu ya hali ya ugonjwa wa Trakoma
nchini mbele ya Wadau wa ugonjwa wa Trakoma kutoka nchi 21.
Picha ya Wadau zaidi ya 100 kutoka nchi 21 ambao walihudhuria kikao
chenye lengo la kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa
Trakoma na jinsi yakuweka takwimu sahihi kilichofanyika jijini Arusha
Kundi namba 1 la Wataalamu likiongozwa na madaktari (Graders) wakijadili kuhusu ugonjwa wa Trakoma katika nchi zao.
Kundi namba 2 ni Wataalamu wa masuala ya Takwimu wakijadil namna ya uingizaji wa takwimu kwa usahihi.
Picha ya Pamoja ya Wadau kutoka nchi 21 wa ugonjwa ya Trakoma(Vikope)
walioshiriki katika kikao kilichofanyika jijini Arusha huku lengo likiwa
kuhimarisha mkakati wa namna ya kugundua ugonjwa wa Trakoma na jinsi
yakuweka takwimu sahihi katika nchi hizo 21.
WILAYA 58 ZAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA TRAKOMA
Na WAMJW - ARUSHA
Mkurugenzi
wa Kinga Wizara ya Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto
Dkt. Leonard Subi amethibitisha kuwa halmashauri 58 nchini zimefanikiwa
kutibu ugonjwa wa trakoma kutokana na jitihada mbali mbali zilizofanywa na Serikali kwa ushirikiano na Wadau.
Alisema
hayo wakati akifungua Mkutano wa Uzinduzi wa Mafunzo kwa wawakilishi wa
nchi 21 ambazo zinamaambukizi ya ugonjwa wa Trakoma/ vikope huku lengo
likiwa ni kuwajengea wataalamu hao uwezo ili waweze kupambana dhidi ya
ugonjwa huu.
"Mwanzoni tulikuwa na Wilaya
takribani 75 ambazo zilikuwa na ugonjwa huu, jitihada zimeweza
kufanyika tangu 2014 hadi leo Hii Karibu Wilaya 58 zimeweza kushinda
dhidi ya ugonjwa huu, tumebakiza Wilaya 13 na kama Serikali tutaendelea
kutoa dawa na Elimu kwa umma ili waweze kujikinga dhidi ugonjwa huu ",
Alisema Dkt. Subi
Dkt
Subi aliendelea kusema kuwa sifa mojawapo ya kudhibiti ugonjwa huu ni
kupitia mafunzo yanayomjengea uwezo mtaalamu kuweza kujua namna ya kujua
ugonjwa, na kuweza kudhibiti dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huu
Kwa
upande mwingine Dkt. Subi ametoa wito kwa wananchi wote hususani
waliokatika hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa huu wa trakoma kuwa
Safi wakati wote kwa kunawa uso, kujenga vyoo na kusafisha mazingira
yanayotuzunguka mara kwa mara.
"ugonjwa huu
unatokana na uchafu, kama huogi, kama hunawi uso, unaweza sababisha
macho yako yakahathirika, ni vizuri kutumia Fursa ya maji vizuri kwa
kufanya usafi vizuri mda wote" alisema Dkt. Subi
Pia
Dkt Subi aliwahasa wananchi kutumia dawa Kwani ni salama na nzuri
ndiomaana zimeponya watu katika halmashauri 58 kufanikiwa kupambana
dhidi ya ugonjwa huu wa trakoma.
Kwa
upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt Thimothy Wonanji alisema kuwa
bado Wilaya tatu jijini Arusha zinaendelea kusumbuliwa na tatizo hili lá
trakoma, Wilaya hizo ni Longido, ngorongoro pamoja na Monduli na
kusema kuwa tatizo kubwa limeonekana kuwa ni changamoto ya upatikaaji wa
maji katika maeneo hayo.
Aliendelea
kusema kuwa Serikali katika ngazi ya Mkoa kuna uratibu wa Magonjwa
yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ambao kwa kushirikiana na wadau wamekuwa
na mradi wa kwenda kijijini na kupita nyumba kwa nyumba kuwapima wakazi
wa maeneo hayo na kuwaanzishia dawa (zitromas) kwa wanaogundulika kuwa
na ugonjwa huu.
Nae
Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dkt Upendo
Mwingila alisema kuwa idadi ya wagonjwa wamepungua kutoka 160 Mpaka
mwaka huu wagonjwa elfu 25,000 hii inatoka na juhudi za Wizara ya Áfya
kupitia mpango wa taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi
kipaumbele na Wadau mbali mbali katika kupambana dhidi ya ugonjwa huu wa
trakoma jambo lililosaidia kufanikisha kufanya upasuaji wa vikope
takribani 12,000 kwa mwaka.
Jumamosi, 7 Julai 2018
DMO SIHA ASEMA KUWA UTOAJI WA DAWA ZA MINYOO MASHULENI YAFIKIA 97% KATIKA WILAYA YA SIHA.
Jumamosi, Julai 07, 2018
-
Hakuna maoni
Mtabibu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto katika Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi
kipaumbele Bw. Wilfred Mandala akiwaelekeza Wawakilishi kutoka Taasisi
ya Bill and Melinda Gate na The End Fund namna ya kusafisha mguu wa Bw.
Juma ambae ni mwasilika wa ugonjwa wa Matende
Afisa kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
katika Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi
kipaumbele Hope Rusibamayila akishirikiana na wanafunzi kutoka Shule ya
Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro
kutoa maelekezo kwa wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate
na The End Fund namna ya Kibuyu Chirizi kikifanya kazi ya kuosha mikono
kwa sabuni baada yakutoka Chooni.
Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund
wakiendelea na ziara yao yakukagua baadhi ya miundombinu waliyoisaidia
katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa
wa Kilimanjaro.
Wawakilishi kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund
wakigawa kalamu za kuandikia kwa wanafunzi wanafunzi kutoka Shule ya
Msingi ya Kilari iliyo katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Endrew Method akiongea na Wanafunzi
pamoja na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund
wakati walipotembelea katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyopo katika
Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro
Afisa Elimu Wilaya ya Siha Rose Sandi akifanya utambulisho kwa Wanafunzi
pamoja na Wageni waliofika katika Shule ya Msingi ya Kilari iliyo
katika Wilaya ya Siha katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa ni kutembelea na
kujionea maendeleo ya mchango waliotoa katika shule hiyo.
Mwanafunzi Kutoka Shule ya Msingi ya Kilari Vaileth Wilfred akimkabidhi
ujumbe Afisa Elimu Wilaya ya Siha Rose Sandi baada ya kumaliza Shairi
lao, kulia kwake ni Mganga Mkuu wa Wilaya ya Siha Dkt. Endrew Method na
wa mwisho ni Afisa Mipango wa kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi
kipaumbele kutoka Wizara ya Afya Bw. Oscar Kaitaba.
Picha yapamoja ya Watumishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto na Wageni kutoka Taasisi ya Bill and Melinda
Gate na The End Fund baada ya kumaliza shughuli ya kutembelea na kukagua
miundombinu katika Shule ya Msingi Kilari wilaya ya Siha Mkoa wa
Kilimanjaro.
Picha ya Pamoja ya Wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Kilari wakionesha
kalamu zao juu kuonesha furaha zao baada ya kupokea kutoka katika
Taasisi ya Bill and Melinda Gate na The End Fund
DMO SIHA ASEMA KUWA UTOAJI WA DAWA ZA MINYOO MASHULENI YAFIKIA 97% KATIKA WILAYA YA SIHA.
Na WAMJW - SIHA KILMANJARO
Mganga
Mkuu wa Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Endrew Method amesema
kuwa Wilaya ya Siha imepiga hatua kubwa katika kukabiliana na changamoto
ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, huku akidai kuwa 97% ya
watoto tayari wameshapata dawa hizo za minyoo.
Ameyasema
hayo alipowapokea wageni kutoka Bill and Melinda Gate na THE END FUND
waliokuja kuangalia utekelezaji wa miradi waliyoifadhili na kufuatilia
namna ya wanufaika wanavyofaidika na miradi hiyo katika Wilaya ya Siha.
“Ukiangalia
utoaji wa Dawa za minyoo mashuleni kwa Wilaya tulifikia 97% jambo
ambalo linasaidia watoto kutopata changamoto za ugonjwa wa minyoo, hata
hivyo kwa wagonjwa wa n je tu matatizo ya minyoo yanafikia hadi nafasi
ya tatu hivyo kuna umuhimu mkubwa wa wa kuufanya uwe mkakati endelevu”
Alisema Dkt. Method
Dkt. Method aliendelea kusema
kuwa Taasisi ya Bill and Melinda Gate na THE END FUND wamekuja kuangalia
ni jinsi gani miradi hiyo imekuwa ikitekelezwa na namna ambavyo
matumizi ya fedha wanazotoa yamekuwa yakiwanufaisha wahusika.
“Wamekuja
kuangalia, ni jinsi gani yale mambo waliyokuwa wakititusaidia
tunatekeleza, na miongoni mwa mambo hayo ni unyweshaji wa watoto dawa
za minyoo kwaajili ya kukabiliana na minyoo mashuleni, usafi wa vyoo na
ujenzi wa vyoo bora katika mashule yetu ambayo tumefanya kwa zaidi ya
miaka Sita, pia wamekuja kuangalia namna ya kukabiliana na ugonjwa wa
trakoma”. Alisema Dkt. Method
Aidha, Dkt. Method
amewashukuru wafadhili hao kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gate na
THE END FUND kwa msaada mkubwa ambao wamekuwa wakitoa katika kuisaidia
Serikali ya Tanzania na jamii kwa ujumla kwaajili ya kupambana na
magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.
Kwa upande
wake Afisa Mipango kudhibiti Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele
kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Oscar
Kaitaba akieleza namna Taasisi ya THE FUND na Bill and Melinda Gate
ilivyosaidia Wizara amesema kuwa ;-
“THE END FUND
imekuwa ikishirikiana na Wizara ya Afya katika kudhibiti ugonjwa wa
Vikope (Trakoma) na ugonjwa wa Matende na Mabusha kwa kuwafanyia
upasuaji katika Mikoa ya Tanga, Pwani na sehem chache Mkoa wa Dar es
salaam”,Alisema Oscar Kaitaba
Oscar Kaitaba
aliendelea kuwa Kwa ugonjwa wa Trakoma wamesaidia kufanya upasuaji wa
Kope katika Mikoa ya Kilimanjaro katika Wilaya ya SIHA na Arusha katika
maeneo ya watu waliohathirika zaidi na ugonjwa huu.
Ijumaa, 6 Julai 2018

UBALOZI WA JAPAN YAMUUNGA MKONO MHE. UMMY KUJENGA MADARASA MKOANI TANGA
Ijumaa, Julai 06, 2018
-
Hakuna maoni
PICHA ZINAZOONYESHA TUKIO LA UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA UJENZI WA MADARASA 6 KATIKA SHULE YA MSINGI MWAKIDILA MKOANI TANGA KATI YA UBALOZI WA JAPAN NA TAASISI YA MAENDELEO YA WANAWAKE TANGA ( TAWODE).
NA WAMJW-DAR ES SALAAM.
Serikali ya Japan kupitia ubalozi wa Japan nchini Tanzania
imetoa kiasi cha shilingi miliioni 188 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 6 ya
shule ya msingi Mwakidila kata ya Tangasisi iliyopo Jijini Tanga
Fedha hizo zimetolewa leo jijini hapa kupitia Shirika la Maendeleo ya Wanawake wa Mkoa wa
Tanga (TAWODE) chini ya Mwenyekiti wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu .
Ubalozi wa Japan nchini imetoa fedha hizo ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya elimu ya Msingi na Sekondari
katika jiji la Tanga.
Akiongea wakati wa hafla ya kutia saini mkataba wa ujenzi
wa madarasa hayo Balozi wa Japan Nchini Tanzania Mhe. Masaharu Yoshida alisema Serikali ya japan imetoa fedha
hizo ili kusaidia maendeleo ya elimu kwa
Jiji la Tanza ili kutatua tatizo la
mrundikano wa wanafunzi madarsani
Aidha, Balozi Yoshida
ameitaka TAWODE kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kikamilifu na kukamilisha ujenzi huo wa madarasa kwa
wakati.
Akiongea wakati wa kutiana saini mkataba huo Mwenyekiti wa
TAWODE, Waziri Ummy Mwalimu ameushukuru Ubalozi wa Japan nchini kwa kukubali
ombi la kufadhili ujenzi wa madarasa ya
shule hiyo ya Msingi Mwakidila ambayo
ina wanafunzi zaidi ya 1,400 kulinganisha na madarasa yaliyopo.
“Sisi kama sehemu ya wanajamii wa Jiji la Tanga tuliona
tuna wajibu wa kuunga mkono Serikali kwa kutafuta vyanzo vingine vya fedha ili
kuwezesha elimu ya Msingi na ile ya sekondari hususan changamoto ya madarasa
itatuliwe hivyo fedha hizi ni za jamii ya Wana Tanga hivyo TAWODE tutahakikisha
zinatumika ipasavyo”.Alisema Waziri Ummy.
Hata hivyo alisema hivi sasa kumekuwa na changamoto ya
madarasa kwenye halmashauri mbalimbali nchini kutokana na ongezeko la wanafunzi kutokana na
Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt.John Magufuli ya kutoa elimu
bure .
Kwa upande wake Meya wa Jiji la Tanga Mhe.Selebosi Mhina
ameushukuru Ubalozi wa japan pamoja na kumpongeza Mhe.Ummy mwalimu kwa kuwa
bega kwa bega katika kusukuma mbele
maendeleo ya wananchi wa Tanga katika sekta ya Elimu na Afya.
Jumatano, 4 Julai 2018

GLOBAL FUND YARIDHISHWA NA UTENDAJI WA WIZARA YA AFYA NCHINI.
Jumatano, Julai 04, 2018
-
Hakuna maoni
Na WAMJW-DSM
Mfuko wa pamoja wa Dunia wa kupambana
na magonjwa ya UKIMWI,Malaria na Kifua Kikuu (GLOBAL FUND) umeridhishwa
kwa kiasi kikubwa na Jinsi Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya
katika kupambana na magonjwa hayo.
Pamoja
na hayo Wawakilishi wa Mfuko huo hapa Nchini wamesema kuwa kutokana na
mwenendo mzuri wa Tanzania katika kutumia vizuri Mfuko huo sasa wanaweza
kuanzisha kitu kingine kizuri kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya na
kupeleka mapendekezo na kukubaliwa.
Malengo ya kikao hiko kati ya Global Fund na Wizara ya Afya ilikuwa ni kujadili ,kupanga na kuboresha Sekta ya Afya nchini.
Jumanne, 3 Julai 2018
KIWANDA CHA DAWA KIKUBWA KUJENGWA NCHINI.
Jumanne, Julai 03, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Wadau wa Masuala ya Uwekezaji na
masuala ya Afya wakati akiwa katika Kikao cha kujadili Uwekezaji wa
Kiwanda cha kutengenezea Dawa nchini na Kampuni ya Fosun Pharma kutoka
nchini China.
Picha ya Wadau wa Masuala ya Uwekezaji na Masuala ya Afya, ikiongozwa na
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage
katika Kikao cha kujadili Uwekezaji wa Kiwanda cha kutengenezea Dawa
nchini na Kampuni ya Fosun Pharma kutoka nchini China.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akijadili jambo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe.
Charles Mwijage katika Kikao cha kujadili Uwekezaji wa Kiwanda cha
kutengenezea Dawa nchini na Kampuni ya Fosun Pharma kutoka nchini China.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimuaga Rais wa Kampuni ya Fosun Pharma inayotarajia kufungua kiwanda cha uzalishaji wa Dawa hapa nchini hivi karibuni baada ya majadiliano yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Kituo cha uwekezaji yaliyomuhusisha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage.
Picha ya Pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na Waziri wa Viwanda, Biashara
na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage baada ya kikao cha kujadili Uwekezaji
wa Kiwanda cha kutengenezea Dawa nchini na Kampuni ya Fosun Pharma
kutoka nchini China.
NA WAMJW-DAR ES SALAAM
KIWANDA
kikubwa cha kutengeneza dawa kinatarajiwa kujengwa nchini ili kupunguza
adha na gharama zinazoikumba nchi wakati wa kuagiza dawa nje ya
Tanzania.
Hayo yamesemwa
na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.
Ummy Mwalimu wakati wa kujadili uwekezaji wa kiwanda cha dawa hapa
nchini leo jijini Dar es salaam.
"Leo
tumekutana kujadili jinsi ya kuwekeza na kiwanda cha kutengeneza dawa
cha FOSUN PHARMA kutoka nchini ili kupunguza changamoto za kuagiza dawa
nje ya nchi na kutokomeza tatizo la upatikanaji wa dawa nchini", alisema
Waziri Ummy .
Aidha
Waziri Ummy amesema kuwa kutokana na kujengwa kwa kiwanda hiko
kitapunguza asilimia kubwa ya fedha inayokwenda nje kwa ajili ya
manunuzi ya dawa kwani mpaka sasa asilimia 94 ya fedha zinakwenda
kununua dawa nje na asilimia 6 ndiyo inannua dawa nchini.
Waziri
Ummy amesema kuwa kutokana na uwekezaji huo kutapelekea kupunguza muda
wa kuagiza dawa kwani muda mwingine kunachukua miezi 9 mpaka miezi 11
kupata dawa kutoka nje ya nchi hivyo kuifanya Serikali kuagiza mzigo
mkubwa zaidi ili kukimbizana na mahitaji ya Watanzania.
"Tunatumia
mda mrefu sana kupata dawa tangu tunapoagiza na wakati mwingine
tunaweza kupata dawa zisizo na ubora kutokana na dawa hizo zinakaguliwa
na mdhibiti wa nje hivyo zinaweza zikaruhusiwa tu na zikija kukaguliwa
na mdhibiti wa ndani unaweza kukuta hazina ubora" alisema Waziri Ummy.
Mbali
na hayo Waziri Ummy amesema kuwa kampuni hiyo inayotengeza sindano za
kutibu Maralia kali ya ATESUNAT itaweza kutengeneza sindano nyingi zaidi
na kuweza kuwahudumia nchi jirani ikiwemo Kenya, Uganda na Burundi.
Kwa
upande wake Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles
Mwijage amesema kuwa hakuna kikwazo kwa Kampuni hiyo kuanzisha ujenzi wa
kiwanda cha dawa hapa nchini kwani kitasaidia upatikanaji wa dawa kwa
urahisi na kukua kwa uchumi kupitia viwanda.
"Tumejadili
na kuwakubalia bila ya kuweka kikwazo kwani tumeridhishwa na ubora wao
katika utengenezaji wa dawa na mafuta nchini kwao hivyo tunawakaribisha
kuja kufanya uwekezaji huo" alisema Waziri Mwijage.
Naye
Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji Nchini Bw. Geofrey Mwambe amesema
kuwa wameupokea uwekezaji huo na wanaufanyia kazi haraka iwezekanavyo
ili kuipeleka Tanzania kuelekea uchumi wa Viwanda.
"Kutokana
na ahadi ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kuipeleka nchi kwenye
uchumi wa viwanda na kutokomeza kabisa tatizo la uhaba wa dawa hatuna
budi kushirikiana na wawekezaji hao kutimiza lengo hilo" alisema Bw.
Mwambe.
Kika hiko cha
kujadili uwekezaji wa kiwanda hiko cha kutengeneza dawa kimeudhuriwa na
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage,
Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA, Bohari kuu ya Dawa MSD, Kituo cha
Uwekezaji nchini TIC na wadau mbalimbali.
Jumatatu, 2 Julai 2018
WIZARA YA AFYA YATANGAZA RASMI KUPOKEA HOSPITALI ZA RUFA ZA MIKOA.
Jumatatu, Julai 02, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akitoa maelekezo juu ya matangazo yaliyo kwenye mbao mapema leo
wakati alipofanya ziara ya kukagua huduma za Afya zinazotolewa katika
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akimsikiliza moja kati ya wagonjwa waliofika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala wakati
alipofanya ziara mapema leo katika Hospitali hiyo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akimsikiliza kwa makini Bi Halima Said aliyefika kupata huduma
za matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala pindi
alipofanya ziara mapema leo katika Hospitali hiyo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akiongea na Bi. Angelina Erasto juu ya umuhimu wa kukata Bima ya
Afya ya TOTO AFYA KADI itakayomsaidia kupunguza gharama za matibabu kwa
mtoto wake,
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
akishangaa idadi kubwa ya wakina mama iliyozidi kiasi katika wodi ya
kupumzikia wakina mama baada ya kujifungua, akiwa katika ziara yake ya
kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala kukagua ubora wa
Huduma zitolewazo katika Hospitali hiyo.
NA
WAMJJW-DAR ES SALAAM
WIZARA ya afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imetangaza
rasmi kuanzia Juali 1 2018 imepokea
Hospitali 28 za Rufaa za Mikoa ambazo zilikuwa chini ya usimamizi wa
OR-TAMISEMI .
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Afya,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara katika
Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala.
“Hospitali ambazo tumezipokea zina jumla
ya vitanda 7,474 na jumla ya watumishi 8,671 ambao, kati yao Wauguzi ni
3,960, Madaktari 536, Madaktari Bingwa wa fani mbalimbali ni 182, na waliobakia
ni watumishi wa kada zingine mbalimbali za Afya” alisema Waziri Ummy.
Waziri Ummy amesema kuwa Hospitali ambazo Wizara imezipokea ni Hospitali
ya Rufaa ya Mkoa ya Mount Meru (Arusha), Dodoma General (Dodoma), Kitete
(Tabora), Shinyanga, Geita, Singida, Mpanda (Katavi), Mawenzi (Kilimanjaro),
Bombo (Tanga), Morogoro, Ligula (Mtwara), Sokoine (Lindi), Maweni (Kigoma),
Sekou Toure (Mwanza), Mwananyamala, Amana, Temeke (Dar es Salaam), Songwe,
Kibena (Njombe), Iringa, Tumbi (Pwani), Sumbawanga (Rukwa), Bariadi (Simiyu),
Musoma (Mara), Songea (Ruvuma), Mbeya, Babati (Manyara) na Bukoba (Kagera).
Waziri Ummy alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2018/19, Wizara imetenga
shilingi Bilioni 30 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya kipaumbele katika
Hospitali za Rufaa za Mikoa ambako tayari huduma zinatolewa ikiwemo Matibabu
kwa wagonjwa wa dharura ,Huduma za upasuaji wa dharura hususan wakati wa
ujauzito na uzazi pamoja na Huduma za tiba kwa wagonjwa mahututi zikiwemo za
watoto wachanga .
Mbali na hayo Waziri Ummy
amesikitishwa na upungufu wa wodi pamoja na vitanda kwa ajili ya wanawake wanaofika kujifungua katika
hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala na kuahidi kulifanyia kazi mara moja
iwezekanavo.
“Kama Mama,na nimeumia sana na lazima tulifanyie ufumbuzi mara moja
kwahiyo namuagiza katibu mkuu alete mtaalamu wa majengo na tupandishe fedha za
kujenga ghorofa mbili mara moja kwakweli halii hii haikubaliki” alisema Waziri
Ummy.
Mnamo Novemba 25, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizindua Hospitali ya Taaluma na
Tiba (MAMC) ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)
aliagiza kuwa Hospitali za Rufaa za Mikoa zihamishiwe kwenye usimamizi wa
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (WAMJW) kutoka
Ofisi ya Rais TAMISEMI.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)














