Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 8 Agosti 2019

TEKNOLOJIA YA NANO FILTER YAWAVUTIA VIONGOZI WA WIZARA JIJINI ARUSHA


Dkt. Askwar Hilonga akiwakaribisha Viongozi wa Wizara wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi na wengineo wakati walipotembelea Chuo Kikuu cha Nelson Mandela Jijini Arusha.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela Prof. Emmanuel Luoga akiangalia tuzo ya ubunifu wa teknolojia ya maji aliyopewa Dkt. Askwar Hilonga kwenye kikao cha dunia cha masuala ya afya (World Health Assembly) kilichofanyika Jijini Geneva, Uswisi mwezi Mei mwaka huu.

Picha ya pamoja katika ofisi ya Kaimu Mkuu wa chuo cha Nelsona Mandela Jijini Arusha.


Mbunifu wa Teknolojia ya Nano Filter Dkt. Askwar Hilonga akiwaonesha viongozi sehemu ambayo ubunifu huo ulipoanzia katika chuo cha Nelson Mandela.

Mifupa ya wanyama inayotumika katika Teknolojia ya Nano Filter kuchuja na kutibu maji kwa ajili ya matumizi.

Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi akiangalia chengachenga za mifupa inayotumika na teknolojia ya Nano Filter katika kuchuja na kutibu maji ya kunywa.

Dkt. Hilonga akitoa maelezo kwa viongozi wa Wizara wakati walipotembelea maonesho ya Sabasaba kwenye banda la Nano Filter.

Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi akiwa na Dkt. Khalid Massa, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Wedson Sichalwe, mbunifu wa Teknolojia ya Nano Filter Dkt. Askwar Hilonga na wajumbe wengine wakiwa katika picha ya pamoja nje ya banda la Nano Filter katika maonesho ya Nanenane Jijini Arusha.


Teknolojia ya Nano Filter iliyofungwa katika moja ya Shule Jijini Arusha.

Baadhi ya Wananchi waliofika katika ofisi hiyo kwa ajili ya kujaziwa maji.

Picha ya pamoja ya viongozi wa Wizara wakiwa na Baadhi ya Wafanyakazi wa Nano Filter nje ya ofisi zao.
Teknolojia ya Nano Filter ikiwa imefungwa katika Maonesho ya Nanenane Jijini Arusha.
Na Emmanuel Malegi-Arusha


Viongozi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi wamemtembelea mbunifu wa teknolojia ya kusafisha maji ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Nelson Mandela kilichoko Arusha Dkt. Askwar Hilonga.

Katika ziara hiyo Dkt. Hilonga amewaonesha viongozi hao Teknolojia iitwayo Nano Filter yenye uwezo wa kusafisha maji, kuondoa bacteria na virusi, huondoa fluoride na madini yote ambayo hayatakiwi kwa binadamu na kuyafanya maji kuwa safi na salama kwa watumiaji na kwa gharama nafuu zaidi.

Dkt. Hilonga ana tuzo 17 kutoka taasisi na mashirika mbalimbali kutokana na ubunifu huo huku tuzo yake kubwa ikiwa ni ile aliyoipata kwenye kikao cha dunia cha masuala ya afya (World Health Assembly) kilichofanyika Jijini Geneva, Uswisi mwezi Mei mwaka huu.

0 on: "TEKNOLOJIA YA NANO FILTER YAWAVUTIA VIONGOZI WA WIZARA JIJINI ARUSHA"