Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 3 Mei 2018

MAABARA YA AFYA YA JAMII YA TAIFA KUKAMILIKA JULAI 2018

Naibu wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati akipata maelekezo kuhusu ujenzi wa Maabara ya afya ya jamii ya Taifa  kutoka kwa Mkandarasi Alex Musumi wa kwanza kulia  kutoka kampuni ya Ukandarasi WCEC wakati alipotembelea kuangalia ujenzi huo leo jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile katikati akikagua michoro ya jengo la Maabara ya Taifa  ya Afya ya Jamii wakati alipotembelea ujenzi wa maabara hiyo unaoendelea jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kulia akikagua jengo la Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii wakati aliootembelea kukagua ujenzi huo leo jijini Dar es salaam , kushoto ni Mkurugenzi wa Ugavi na Manunuzi Wizara ya Afya Bw. Castro Simba.

 Ukaguzi wa jengo hilo ukiendelea.





Muonekano wa jengo la Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii liliopo jijini Dar es salaam likiwa bado linaendelea na ujenzi.

Sambamba na hilo Dkt. Ndugulile ametembelea Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua kitabu cha usajili wa dawa wakati alipotembelea Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA leo jijini Dar es salaam, kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi.  Agness Kijo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia mitambo iliyo katika maabara ya chakula, wakati alipofanya ziara katika mamlaka hiyo jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati akipata maelezo kutoka kwa Mchunguzi wa Dawa na vipodozi Gerald Sambu kulia wakati alipitembelea TFDA leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi TFDA Bi. Agness Kijo

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA wakati alipotembelea mamlaka hiyo leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi.  Agness Kijo.



Na WAMJW- DAR ES SALAAM. 

UJENZI wa Maabara ya  Afya ya Jamii ya Taifa inayohusiana na magonjwa ya mlipuko unatarajia kukamilika ifikapo Julai mwaka huu. 

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa ziara yake ya kuangalia hali  ya ujenzi wa maabara hiyo jijini Dar es salaam. 

"Mpaka hivi sasa asilimia 60 ya ujenzi imekamilika hivyo namsisitiza  Mkandarasi kwamba Serikali haitaongeza muda wa ziada mpaka kufikia Julali 9 mwaka huu tuwe tumeshakabidhiwa jengo hili" alisema Dkt. Ndugulile 

Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa Maabara hiyo ya Afya ya Jamii ya Taifa ni kwa ajili ya kupima sampuli ya magonjwa ya mlipuko na itakuwa ni maabara kubwa Afrika yenye kiwango cha ubora wa  BS3 ambayo imegharimu kiasi cha shilingi Bilioni 7. 6. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya ukandarasi ya WCEC Injinia Edwins Shittindi amesema kuwa ujenzi huo ulitakiwa uwe umekamilika Oktoba mwaka jana badala ya Julai 2018.

"Tulitakiwa kukabidhi hiki jengo Oktoba 2017 lakini kutokana na vifaa ya kazi  tulivyoviagiza kuchelewa kuwasili tutajitahidi mpaka kufikia Julai 9 mwaka huu tuwe tumekabidhi jengo" alisema Eng. Shittindi.

Sambamba na hilo Dkt. Ndugulile ametembelea Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA na kuwataka waangalie sana watu wanaotangaza vipodozi vyao kwenye mitandao ya jamii na kuandaa utaratibu husika kuhusu bidhaa hizo. 

"Kila kukicha kuna matangazo mengi sana kwenye mitandao ya jamii yanayohusiana na vipodozi hivyo mnatakiwa kuchukua tahadhari na kufuatilia kwa ukaribu kuhusu ubora wa bidhaa zao" alisema Dkt.  Ndugulile. 

Dkt. Ndugulile amesema kuwa TFDA wanatakiwa kuhakikisha ubora wa dawa ,  chakula pamoja na vipodozi unastahili ili watanzania waweze kutumia bidhaa zenye usalama zaidi. 

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile leo ametembelea maeneo mbalimbali ya TFDA ikiwemo sehemu ya usajili wa Dawa, maabara na kuweza kuongea na Uongozi wa Mamlaka hiyo. 

0 on: " MAABARA YA AFYA YA JAMII YA TAIFA KUKAMILIKA JULAI 2018"