Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 16 Mei 2018

WATUMISHI WA AFYA NCHINI WANATAKIWA KUCHUNGUZA WATOTO SARATANI YA MACHO KILA WANAPOHUDHURIA KLINIKI.

Mganga Mkuu wa Serikali ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Mohammed Bakari Kambi akitoa tamko la Saratani ya Macho kwa watoto mbele ya waandishi wa Habari hawapo pichani leo katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es salaam.

 Mkurugenzi wa Ubora wa Huduma za Afya Dkt. Mohammed Ali Mohammed kushoto na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi wote kutoka wizara ya Afya wakifuatilia kwa makini maelezo ya Mganga Mkuu wa Serikali ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Mohammed Bakari Kambi alipotoa tamko la Saratani ya Macho kwa watoto.

Kaimu Mkurugenzi  wa mpango wa Macho wizara ya Afya Dkt. Benadertha Shilio akizumza na waandishi wa Habari hawapo pichani kuhusu wiki ya elimu ya Saratani ya Macho kwa watoto leo katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es salaam.

NA WAMJW-DAR ES SALAAM 

WATUMISHI wa Afya wa ngazi ya Jamii,Zahanati , Vituo vya afya vya na Hospitali za Kliniki za Mama na Mtoto za Wilaya zinatakiwa kuchunguza Uakisi wa mwanga kwenye mboni za watoto kila wanapoenda kucheki ukuaji wa watoto hao ili kupunguza uwepo wa saratani ya macho kwa watoto.
Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Mohammed Bakari Kambi wakati akitoa tamko la saratani ya macho kwa watoto kwa niaba ya Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es salaam.
“Iwapo mtoa huduma za afya unahisi kuwa mtoto ana tatizo kwenye jicho usimrudishe nyumbani hadi uhakikishe mtoto huyo ameonwa na mtaalamu wa macho ili kugundua kama ana tatizo kwenye macho yake” alisema Prof. Kambi.
Aidha Prof. Kambi amesema kuwa katika kuboresha huduma hizo Wizara imeandaa mwongozo ambao utasaidia kuinua uelewa wa wataalamu wa afya ili waweze kuwatambua watoto wenye tatizo hilo na kuwapa rufaa mapema.
Kwa Mujibu wa Prof. Kambi amesema kuwa takwimu za hapa nchini zinaonesha kuwa watoto137 wenye saratani hii walionwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa mwaka 2017 na watoto 80 hadi 100 hupewa rufaa na kufika kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na wengine hutibiwa KCMC Moshi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi  wa mpango wa Macho wizara ya Afya Dkt. Benadertha Shilio amesema kuwa anawashukuru wadau wote wa macho ambao wamekuwa bega kwa began a Serikali ya Tanzania katika kufanikisha kuboresha huduma za Macho kwa watoto.
“Tunawashukuru Rotary Club ya Dar es salaam Oysterbay wakishirikiana na Rotary Club ya Chelsea nchini Uingereza ambao wametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya kutibu Saratani ya macho vinavyogharimu kiasi cha Dola za Kimarekani 65,000 na Kampuni ya Pricewaterhouse ya Tanzania ambayo imetoa vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 25 ambavyo vimesambazwa Muhimbili na Mloganzila” alisema Dkt. Shilio.
Maadhimisho ya Wiki ya sarani ya Macho kwa watoto kwa mawaka 2018 imebeba kauli mbiu isemayo “MBONI NYEUPE KWENYE JICHO LA MTOTO INAWEZA KUWA SARATANI YA MACHO”.
 

0 on: "WATUMISHI WA AFYA NCHINI WANATAKIWA KUCHUNGUZA WATOTO SARATANI YA MACHO KILA WANAPOHUDHURIA KLINIKI."