Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 4 Mei 2018

TAARIFA KWA UMMA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA,MAENDELEO YA JAMII,JINSIA WAZEE NA WATOTO


TANGAZO LA WATUMISHI WALIOPATA UFADHILI KWA AWAMU YA PILI KWA MASOMO YA UZAMILI KWA MWAKA 2017/2018
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, anawatangazia watumishi walioomba ufadhili wa masomo ya Uzamili kwa mwaka wa masomo 2017/2018 kuwa zoezi la uchambuzi wa maombi ya ufadhili kwa awamu ya pili umekamilika. Jumla ya watumishi 17 wamechaguliwa kwa awamu hii ya pili hivyo kukamilisha idadi ya watumishi 90 ambao wamepata ufadhili kwa mwaka wa masomo 2017/2018, ufadhili huu unahusisha kulipiwa gharama za ada kwa kipindi chote cha masomo pamoja na posho ya utafiti.
Watumishi hawa waliochaguliwa wanatakiwa kuandika barua ya kukubali ufadhili huu pamoja na kujaza mkataba wa makubaliano ya ufadhili (Bonding Agreement) na Wizara. Wizara inasisitiza kuwa haitahusika kugharamia mafunzo ya mtumishi yeyote ambaye hayuko kwenye orodha hii au ambaye yuko kwenye orodha hii lakini hatojaza mkataba wa  makubaliano ya ufadhili.
Kila mtumishi aliyepata ufadhili atalazimika kuingia kwenye tovuti ya Wizara ya afya ili kupata nakala ya mkataba ambao atatakiwa kujaza nakala tatu katika sehemu zinazomhusu na sehemu ya “First guarantor” atajaza mwajiri wake au yeyote mwenye mamlaka ya kusaini kwa niaba ya mwajiri wake kisha agonge muhuri wa mwajiri na “guarantor” wa pili anapaswa kuwa mtu yeyote mwenye sifa za kuingia mkataba kwa mujibu sheria za nchi. Mikataba hiyo (nakala tatu) ikikamilika kujazwa itawasilishwa wizarani kwa kuambatishwa na picha 3 (passport size) ili Wizara iweze kukamilisha kusaini mikataba hiyo. Kwa watumishi waliopo Dar es Salaam wawasilishe mikataba hiyo ofisi ndogo ya Wizara iliyopo Dar es Salaam, na wengine wawasilishe Makao Makuu ya Wizara yaliyopo Dodoma
Mwisho wa kuwasilisha mikataba hiyo ni tarehe 25/05/2018. Mkataba wa makubaliano ya Ufadhili (Bonding Agreement) unapatikana kwenye tovuti ya Wizara www.moh.go.tz.

Imetolewa na;

Katibu Mkuu (Afya),
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Maendeleoya Jamii,
Jengo 11,
S.L.P 743.
40478 DODOMA
04/05/2018.

0 on: "TAARIFA KWA UMMA"