Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 2 Mei 2018

MAJI YANAYOTIRIRIKA MITAANI KUTOKA VIWANDANI YAPIMWE KEMIKALI.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndegulile akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu ambae alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Otilie Gowelle.kulia ni Mwenyekiti wa bodi hiyo Dkt Esther Jason.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndegulile akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi Dkt. Esther Jason mwongozo wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu ambae alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Otilie Gowelle.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndegulile akimkabidhi vitendea kazi Mkemia Mkuu wa Serikali Fidelice Mafumiko wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali leo jijini Dar es salaam. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Esther akiongea akitoa neno mbele ya viongozi wa Serikali na Waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndegulileakisisitiza jambo mbele ya Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mku na viongozi wengine wa Srikali wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu.


Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndegulile wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali leo jijini Dar es salaam. 

Na WAMJW-DAR ES SALAAM. 

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeitaka  Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kuchukua hatua ya kupima maji yanayotiririka mitaani kutoka viwandani kubaini kama yana kemikali ambazo zinaathiri wananchi au hazina madhara yoyote. 

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afy, Maendeleo ys Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali leo jijini Dar es salaam. 

"Bodi hii ninayoizindua leo inatakiwa kuhakikisha  majibu ya watu wanaokuja kuleta vipimo vyao yatoke mapema na haraka iwezekanavyo ili kupunguza msongamano wa wateja wenu" alisema Dkt. Ndugulile. 

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa Mamlaka hiyo inatakiwa kushirikiana na kufanya  mazungumzo na Taasisi ya Chakula na Dawa TFDA na TBS ili kutoingiliana katika majukumu kwani kuna kuna kipengele cha majukumu yao kinafanana katika kusimamia ubora wa chakula. 

Aidha Dkt. Ndugulile ameitaka Mamlaka hiyo kuisimamia kikamilifu sheria ya uchafuzi wa Mazingira ili kuepusha wananchi na magonjwa ya kuambukiza na yasioambukiza. 

Kwa upande wake Mkemia Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu wa Bodi hiyo Dkt. Fidelis Mafumiko amesema kuwa wanaiomba Serikali kutatua changamoto ya upungufu wa mitambo ya kufanyia kazi katika mamlaka hiyo. 

Aidha Dkt. Mafumiko amesema kuwa Bodi hiyo iliyozinduliwa leo ipo tayari kufanya kazi kwa manufaa ya  Watanzania japo mamlka hiyo ina upungufu wa Watumishi kutoka watumishi 400 mpaka kufikia watumishi 220. 

Bodi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imezinduliwa leo ikiwa na Wajumbe saba ambao ni Mwenyrkiti wa bodi hiyo Prof. Esther Hellen, Katibu Dkt. Fidelis Mafumiko,  Dkt. Eliud Eliakimu,  Dkt. Samwel Gwamaka, Dcp. Hussein Laiser, Bi. Irene Leisure na Bw. Pius Mponzi. 

0 on: "MAJI YANAYOTIRIRIKA MITAANI KUTOKA VIWANDANI YAPIMWE KEMIKALI. "