Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 20 Julai 2018

SERIKALI YAIPATIA MKOA WA MARA BILION 5.9 KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akitoa maelekezo kwa mhandisi wa Majengo wakati alipofanya ziara ya kutembelea ujenzi wa hospitali ya Mkoa wa Mara.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akisikiliza kero kutoka kwa mgonjwa aliyefika kupata huduma za afya katika kituo chá Afya Nyasho Mkoani Mara.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akisikiliza maoni ya mama alipofanya ziara katika wodi ya kujifungulia katika kituo chá Afya chá Nyasho Mkoani Mara.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akimjulia hali Mtoto aliyefika na mama yake katika kituo chá Áfya chá Nyasho

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akimsalimia moja kati ya wazee aliyefika kupata huduma za afya katika kituo chá Áfya chá Nyasho Mkoani Mara huku akimsisitiza kuwa matibabu ni bure kwa wazee wote wasio na uwezo wakuchangia.

Dkt. Faustine Ndugulile (wakatikati) akiendelea na ziara yake ya kutembelea ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Serengeti.


SERIKALI YAIPATIA MKOA WA MARA BILION 5.9 KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

Na WAMJW-MARA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto imeupatia Mkoa wa Mara kiasi cha shilingi Bilion 5.9 ikiwaq ni moja ya jitihada za kuboresha hali ya utoaji huduma za Afya kwa wananchi katika mkoa huo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile mapema leo wakati akiwa katika ziara yake ya Kukagua hali ya utoaji huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara.

“Mkoa wa Mara umepokea Bilion 5.9 kwaajili ya kuboresha vituo vya kutolea huduma za Afya 13, ikiwa ni jitihada za Serikali katika kuboresha hali nya utoaji huduma kwa wananchi wake “ alisema Dkt Ndugulile.

Pia Dkt. Ndugulile aliagiza kamati ya ulinzi ya Wilaya ya Tarime ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya Mhe. Vicent Naano kusimamia vizuri manunuzi ya Dawa, huku akiagizi Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Mwanisi kuhakikisha  dawa zote zinunuliwe kutoka Bohari ya Dawa (MSD).

“Hutaratibu wa kuagiza Dawa kwa  mawakala sitaki kuusikia, MSD tuna dawa karibia zote za msingi,  utaratibu wa mawakala tuliuweka kama mbadala endapo MSD watakosa aina Fulani ya dawa” Alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa  mimba na ndoa za utotoni bado ni tatizo kubwa ambapo mkoa wa Mara ni wa tano kitaifa kwa kuwa na asilimia 37.

“Serikali imeandaa Mpango wa kazi wa Kitaifa wa Kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto wa mwaka 2017/18-2021/22 na moja kati ya msisitizo katika mpango huu ni kutokomeza ukatili wa kijinsia shuleni” alisisitiza Dkt. Ndugulile

Aidha Dkt. Ndugulile amekemea mahusiano ya kingono yaliyopo baina ya walimu na wanafunzi na kuwataka wanafunzi kuacha kufanyiana vitendo vya ukatili na kutoa taarifa ya vitendo vya ukatili.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Mwanisi alisema kuwa Idara ya Afya ina upungufu mkubwa wa watumishi mkoani hapo ambao ni 3477 sawa na Asilimia 60.9 ikilinganishwa na watumishi 2237 sawa na Asilimia 39.1 waliopo sasa kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya hadi kufikia mwezi Juni 2018.

Dkt. Mwanisi aliendelea kusema kuwa hali ya maambukizi ya VVU yamepungua kutoka Asilimia 4.5 mwaka 2011 hadi Asilimia 3.6 mwaka 2016/2017 kulingana na utafiti wa kitaifa uliofanyika mwaka  2011-2012 na 2016-2017 huku akisema kuwa wanaendelea kufanya juhudi mbali mbali za kupambana na UKIMWI ili kuhakikisha maambukiz mapya yanaendelea kupungua.

Kwa upande mwingine Mganga Mkuu wa Mkoa alisema hali ya chanjo hadi kufikia Disemba 2017 kwa watoto chini ya mwaka mmoja waliomaliza chanjo zote kimkoa ilikuwa Asilimia 143 ambayo ipo juu ya lengo la kitaifa ambalo ni Asilimia 90.

0 on: "SERIKALI YAIPATIA MKOA WA MARA BILION 5.9 KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO."