Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 14 Februari 2018

SERIKALI YAENDELEA KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI KWA KUONGEZA VITUO VYA AFYA NCHINI.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiweka jiwe la Msingi katika ufunguzi wa jengo la mama na mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, mapema leo jijini Dar es salaam, katikati ni Naibu waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akimjulia hali moja ya mama aliyekuwa akiuguliwa na mtoto wake, akifanya hivyo baada ya kuzindua jengo la mama na mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Poul Makonda.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakisalimiana na Mbunge wa Ilala Mhe. Azan Zungu wakati wa Uzinduzi wa jengo la mama na mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, wa pili ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Poul Makonda na wa mwisho ni Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa mama aliyekuwa akiuguliwa na mtoto wake, akifanya hivyo baada ya kuzindua jengo la mama na mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, kulia kwake ni Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, kulia kwake ni Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile na kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Poul Makonda.

Na WAMJW. DSM
SERIKALI yaendelea kuongeza vituo vya Afya nchini ikiwa ni moja ya jitihada za Serikali za kuboresha Huduma za afya nchini jambo litakalo saidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali za Wilaya na Mkoa kwa kuwa huduma zote zitakuwa zimeishia kwenye ngazi ya Kata.
Hayo yamebainishwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa ufunguzi wa jengo la mama na mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, mapema leo jijini Dar es salaam.
“Kumekuwa na ongezeko kubwa la vituo vya Afya nchini kutoka vituo vya Afya 6321 kwa mwaka 2010 hadi vituo vya Afya 7680 kwa mwaka 2016, na kazi ya nyongeza inaendelea, kwaiyo tunaamini  vituo hivi vitaweza kupunguza msongamano katika hospitali za Wilaya, pamoja na Hospitali za Mkoa”, alisema Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Mhe. Waziri Mkuu alisema kwamba Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametenga kiasi cha Zaidi ya Bilioni 100 ikiwa ni fedha za kuboresha Vituo vya Afya nchini ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi katika maeneo yote nchini.
“Tumeanza kuboresha Vituo vya Afya kwa kujenga Wodi yakinamama wanaojifungua, thieta, wodi za magonjwa yakawaida, maabara, tunaongeza na nyumba za watumishi, ili kila kituo cha Afya kiwe na miundombinu hiyo ili utoaji huduma uwe rahisi” alisema Mh. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Mhe. Waziri Mkuu aliendele kusema kwamba Serikali imetumia Zaidi ya Bilioni 161 katika kuendelea kuboresha Huduma za Mama na Mtoto kwa lengo la kuokoa Maisha ya mama na mtoto jambo ambalo ni moja kati ya changamoto kubwa nchini.
Aidha Mhe. Waziri Mkuu alisema kwamba Serikali imeendelea kuboresha Huduma za Afya kwa kutenga kiasi cha shilingi Bilioni 129 kwaajili ya vifaa vya kuwezesha kundesha shughuli za upasuaji katika kila kituo cha Afya ambacho kinaboreshwa.
Wakati akitoa taarifa ya Afya ya Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Poul Makonda alisema kwamba wakina mama 126,164 walipata nafasi ya kujifungua katika vituo vya Afya, huku wakinamama 202 ambao ni sawa na Asilimia 0.5 walilazimika kujifungua kwa wakunga, na Asilimia 1.5 zaidi ya akinamama 1976 walijifungua njiani wakielekea kupata huduma, idadi inayoonekana kuwa kubwa sana katika Mkoa wa Dar Es salaam.
Idadi ya 2016 inaonesha Zaidi ya akina mama 85 walikuwa wanapoteza Maisha kati ya kina mama 100,000 waliokuwa wanajifungua lakini kwa sasa tangu maboresho yafanyike ni akina mama 57 kati ya akina mama 100,000 wanaojifungua ndio hupoteza Maisha, huku mikakati thabiti yakupunguza vifo hivyo ikiendelea kuwekwa.
Mhe. Makonda aliendelea kusema kwamba zaidi ya watoto ambao wanafanikiwa kuwa hai na kuwa salamakatika kujifungua ni Zaidi ya watoto 126,712, na watoto 131 huzaliwa wakiwa tayari wameshakufa, idadi hii ikilinganishwa .
Pia Mhe. Makonda alimshukuru AMSONS GROUP ambayo imetoa mchango mkubwa katika ujenzi wa Jengo hilo la Mama na Mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana huku akiwataka Wadau wengine kuiga mfano huo katika dhana ya kusukuma gurudumu la maendeleo katika jamii zetu.
Nae Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano tangu iingie madarakani imeongeza Bajeti ya Dawa kutoka Bilioni 30 mpaka sasa ni Bilioni 270 likiwa ni ongezeko la Zaidi ya mara 9, huku Wastani wa upatikanaji wa dawa ukiwa Zaidi ya asilimia 80.
“Serikali wakati inaingia madarakani Bajeti ya dawa ilikuwa ni Bilioni 30, mwaka unaofuata ikafikia Bilioni 200, na hivi tunavyoongea Bajeti ya Dawa ni Bilioni 270, likiwa ni ongezeko la mara 9, kama msaidizi wako nasimama kifua mbele na kusema ya kwamba hatuna uhaba wa Dawa muhimu”, alisema Dkt. Ndugulile.

0 on: "SERIKALI YAENDELEA KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI KWA KUONGEZA VITUO VYA AFYA NCHINI."