Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 28 Februari 2018

SERIKALI YATARAJIA KUWA NA WATOA HUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII ZAIDI YA 30,000

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akielezea jambo mbele ya Wadau wa Afya, mashirika yasiyo Yakiserikali, na Serikali katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.

Afisa kutoka kitengo cha Elimu ya Afya kwa umma Wizara wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Amalbega Kasangala akiwasilisha taarifa mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu(hayupo kwenye picha).

Wadau wa Afya, mashirika yasiyo Yakiserikali, Watumishi wa Serikali na Waandishi wa Habari wakifuatilia taarifa kutoka kwa mgeni rasmi Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu(hayupo kwenye picha), katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.



Na WAMJW. Dar es salaam.
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inatarajia kuwa na watoa huduma wa Afya ngazi ya jamii (CHWz) Zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka 2020 katika vijiji Zaidi ya 15,000 nchini.
Hayo yamesemwa leo na  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu  katika Mkutano wa Wadau wa Afya, mashirika yasiyo Yakiserikali, na Serikali katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.
“Tunataka itakapofika mwaka 2020, tuwe na angalau Wahudumu wa Afya zaidi ya 30,000 katika vijiji Zaidi ya 15,000 tulivyonavyo Tanzania, Eneo hili tumeliona ni eneo muhimu kwasababu tutapata matokeo ya haraka, ni bora kutumia Bilioni 40 kwa ajili ya kinga ya magonjwa kwa Watanzania .” Alisema Mhe. Ummy Mwalimu.
Mhe. Ummy alisema kuwa lengo la Mkutano huo ni kujadiliana na Wadau wa Maendeleo na Mashirika yasiyo Yakiserikali juu ya kuimarisha huduma ya Afya ya msingi hasa katika kuwakinga wananchi dhidi ya maradhi kupitia mikakati ambayo inakubalika kimataifa ya kuwa na watoa huduma katika ngazi ya jamii.
“Kisera tumesema kuwa tunataka kuwa na watu wawili ambao watakuwa wanafanya kazi kama watoa huduma za Afya na kazi yao kubwa haitakuwa kutibu bali itakuwa ni kusisitiza masuala ya lishe, masuala ya uzazi wa mpango, kuhimiza watu kujua hali zao hasa katika maambukizi ya VVU na kuwaelekeza waende maeneo gani ili kupata huduma za Afya” alisema Mhe. Ummy
Kwa upande mwingine Mhe. Ummy Mwalimu aliwashukuru wadau wa maendeleo na Mashirika yasiyo Yakiserikali kwa kuwa tayari kushirikiana na Serikali katika kufanikisha kuwa na watoa huduma za Afya ngazi ya jamii kwa idadi yakuridhisha ifikapo 2020.
Hata hivyo Waziri Ummy alisema kuwa rasilimali watu katika Sekta ya Afya nchini ni Asilimia 51, huku kukiwa na upungufu wa watoa huduma za Afya kwa Asilimia 49, ambao ni pamoja na Madaktari, Wauguzi, Wataalamu wa Maabara, huku mikoa ambayo inaupungufu Zaidi ni Katavi, Rukwa, Tabora, Kigoma na Kagera.
Naye, Afisa kutoka kitengo cha Elimu ya Afya kwa umma Wizara wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Amalbega Kasangala alisema Serikali kuwa Serikali imejipanga katika kukinga ugonjwa kuliko kutibu jambo ambalo litasaidia katika kupunguza gharama kwa wananchi.

0 on: "SERIKALI YATARAJIA KUWA NA WATOA HUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII ZAIDI YA 30,000 "