Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 26 Februari 2018

TANZANIA YAPOKEA TUZO YA KUPAMBANA NA UGONJWA WA MALARIA KUTOKA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO)

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammed Bakari Kambi akipokea cheti cha kutambua mchango mkubwa uliofanywa na Serikali katika kupambana na ugonjwa wa Malaria kutoka mwakilishi wa WHO Dkt. Ritha Njau tukio lililofanyika mapema leo Serena jijini Dar es salaam.
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammed Bakari Kambi akiongea na wadau wa Afya na waandishi wa habari katika kikao cha kupokea cheti cha kutambua mchango mkubwa uliofanywa na Serikali katika kupambana na ugonjwa wa Malaria.

Meneja wa Mpango wa Kupambana na Kudhibiti Malaria nchini Dkt. Ally Mohamed akiwasilisha taarifa mbele ya wadau na waandishi wa Habari katika kikao cha kupokea cheti cha kutambua mchango mkubwa uliofanywa na Serikali katika kupambana na ugonjwa wa Malaria kutoka mwakilishi wa WHO Dkt. Ritha Njau tukio lililofanyika mapema leo Serena jijini Dar es salaam.

Mwakilishi wa WHO Dkt. Ritha Njau akijiandaa kumkabidhi cheti Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammed Bakari Kambi

Wadau wa Afya wakifuatilia kwa umakini taarifa ilokuwa ikiwasilishwa na Meneja wa Mpango wa Kupambana na Kudhibiti Malaria nchini Dkt.  Ally Mohamed (hayupo kwenye picha)wakati wa kikao cha kupokea cheti cha kutambua mchango mkubwa uliofanywa na Serikali katika kupambana na ugonjwa wa Malaria.


Na WAMJW-Dar es salaam.
SERIKALI ya Jamhuri wa Muungano Tanzania imepata tuzo kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa kutambua mchango mkubwa uliofanywa katika jitihada ya kudhibiti Ugonjwa wa Malaria nchini.
Akikabidhiwa Tuzo hiyo wakati wa mkutano wa siku mbili ulioanza leo wa kujadili mafanikio na changamoto katika kudhibiti Malaria,Mganga Mkuu wa Serikali  Profesa Muhammad Bakari Kambi alisema tuzo hiyo imetolewa kwa Serikali na Watanzania kwa ujumla na Shirika hilo  kanda ya Tanzania
Prof.Kambi alisema tuzo hiyo imetolewa kwa kuanisha mchango mkubwa uliofanywa na  Serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuweka Mikakati,Rasilimali fedha na kufanya kazi kwa ukaribu na wahisani mbalimbali katika kupambana na Malaria
Prof. Kambi aliendelea kusema kuwa ushiriki wa Tanzania katika tafiti mbalimbali ambazo zimechangia katika udhibiti wa Malaria ikiwemo utafiti wa kutumia vyandarua vyene viuatirifu vya kuzuia mbu pamoja na  tafiti za awali za chanjo za kudhibiti Malaria.
“Mafanikio mengine ni  upungufu wa Ugonjwa wa Malaria kutoka wagonjwa milioni 18 kwa mwaka 2008 hadi wagonjwa milioni 5.5 kwa mwaka 2017.Pia Malaria imekua chanzo kikubwa cha vifo vya watoto wenye umri chini ya miaka mitano hivyo kumekua na upungufu kutoka vifo 112 kati ya watoto 1,000 mwaka 2005 hadi vifo  79 kati ya watoto 1,000 mwaka 2016”.Alisema
Aidha, kipengele kingine katika vita dhidi ya udhibiti wa ugonjwa wa Malaria ni kwamba, Tanzania ndio nchi pekee Barani Afrika kuwa na kiwanda kinachotengeneza vyandarua vyenye dawa ya kudhibiti mbu aenezaye Malaria.
Naye,Kaimu Mwakilishi Mkazi wa WHO, Dkt. Ritha Njau amesema tuzo hiyo imetolewa kwa Tanzania baada ya kufanikiwa kupunguza maambukizi ya Malaria kwa kipindi cha miaka 10, hivyo WHO imeona ni vema kutoa tuzo hiyo ikiwa ni katika kutambua mafanikio hayo.
Wakati huo huo,Meneja Mpango wa Kudhibiti Malaria Nchini Dkt. Ally Mohammed alisema hali ya maambukizi ya Malaria nchini hivi sasa imepungua na kufika asilimia 7.3 ambapo lengo ni kutokomeza malaria nchini.
Dkt. Ally Mohammed Alitaja mikoa ya Kigoma, Geita na Kagera hali ya malaria bado ipo juu, hivyo mkutano huo utaweza kujibu maswali kwanini mikoa hiyo maambukizi ya malaria bado juu na kitu gani kifanyike ili kuweza kutokomeza ugonjwa huo.

0 on: "TANZANIA YAPOKEA TUZO YA KUPAMBANA NA UGONJWA WA MALARIA KUTOKA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO)"