Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 23 Februari 2018

SERIKALI YAPANGA KUSITISHA UTOAJI HUDUMA YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA KWA WAGANGA WASIOJISAJILI

Kaimu Mkurugenzi msaidizi wa tiba asili na tiba mbadala kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Poul Mhame akiongea na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya leo jijini Dar es salaam.




Na WAMJW. Dar es salaam.
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepanga kusitisha shughuli za utoaji wa huduma zinazofanywa na waganga wa tiba asili na tiba mbadala pindi muda wa kujisajili utakapokuwa umwekwisha.
Amebainisha hayo Kaimu Mkurugenzi msaidizi wa tiba asili na tiba mbadala kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Poul Mhame mapema leo pindi alipoongea na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.
“Waganga wa Tiba asili na Tiba mbadala na vituo vyao watalazimika kusitisha utoaji huduma wanazotoa pindi muda wa usajili cha itafika mwisho” Alisema Dkt. Mhame
Dkt. Mhame aliendelea kusema kuwa Serikali ilianza usajili wa Waganga wa Tiba asili takribani miaka saba ilopita na mpaka sasa ni waganga 16,300 tu ndio waliofanikiwa kujisajili huku mchakato huo ukiendelea mpaka sasa.
Dkt. Mhame alielezea kusikitishwa sana na idadi ndogo ya Waganga wa tiba asilia kujisajili inayoendelea kwa maeneo ya mjini hususania katika Manispaa, Miji, na Halmashauri, ikilinganishwa na maeneo ya vijijini ambao wanaonekana kwenda kwa kasi sana,
“Ni Dhahiri kuwa taarifa hizi, hazijawafikia wengi hususani waliopo vijijini kutokana na vyombo vya habari vilivyopo kule, lakini wengi waliopo mijini hawana sababu zakusema hawajui” Alisema Dkt. Mhame.
Aidha, Dkt, Mhame amewashauri Wanganga wa Tiba asili kutumia fursa hii kwa muda uliobaki kwa kwenda ofisi za Waganga wa Halmashauri zao kujaza fomu na kuziwasilisha ili waweze kujisajili na kuondokana na usumbufu huo.
“Itakuwa si busara kwa mganga alipo Dar es salaam akakutwa hajajisajili kwa kipindi chote cha miaka saba, asilalamike kwamba hana taarifa” Alisema Dkt Mhame.
Kwa upande mwingine Dkt. Mhame aliwataka wanaojihusisha na uzalishaji wa Dawa kusajili dawa hizo huku akiwahasa wataalamu mbali mbali kama vile Madaktari, Wafamasia, Wakemia, Maafisa lishe kushirikiana kwa ukaribu katika kuboresha huduma za tiba Asili kwa kutumia taalama zao kwa kushirikiana na Waganga wa Tiba Asilia ili kuweza kupata soko linalostahili na lenye usalama na ufanisi wakutosha.

0 on: "SERIKALI YAPANGA KUSITISHA UTOAJI HUDUMA YA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA KWA WAGANGA WASIOJISAJILI"