Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 2 Agosti 2019

WAKAZI WA TANGA KUPATA HUDUMA ZA DHARURA NA MAHUTUTI KATIKA HOSPITALI YA BOMBO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiteta na Makamu wa Rais wa Taasisi ya ABBOTT Bw. Andy Wilson wakati wa uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tanga.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea jambo wakati wa uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga mapema leo.
Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya ambaye alimuwakilisha Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Leonard Subi akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi kartika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizindua huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Tanga Bw. Thobias Mwilapa.




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Kushoto) akioneshwa kifaa cha kusaidia mapigo ya moyo na Daktari bingwa wa huduma za dharura Dkt. Juma Ramadhan wakati Waziri alipozindua huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Bombo mkoani Tanga.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisikiliza maelezo kutoka kwa mtaalamu wa chumba cha wagonjwa mahututi wakati alipotembelea chumba hicho baada ya uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga.


Chumba cha wagonjwa mahututi (ICU)
Baadhi ya Wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Tanga wakifuatilia Hotuba za uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi Hospitalini hapo.
Na Emmanuel Malegi-WAJMW-Tanga

Wakazi wa Jiji la Tanga sasa wataanza kupata huduma za uhakika za dharura pamoja na huduma za wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga (Bombo).

Huduma hizo zimefunguliwa rasmi leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati ziara yake ya siku mbili mkoani humo huku akiwahakikishia wananchi wa Tanga kutolazimika kupewa rufaa kwa ajili ya kufuata huduma hizo Muhimbili na KCMC.

“Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli inaendelea kuboresha huduma za afya katika Hospitali za mikoa kwa kujenga jengo la huduma za dharura lililogharimu Tsh. Milioni 211.6 na jingo la kuwahudumia wagonjwa mahututi Tsh. Milioni 350 katika kipindi cha mwaka 2018/19”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy ameongeza kuwa kuanzishwa kwa huduma hizo za dharura na mahututi zitatatua changamoto zilizokuwepo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga na kuongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2018/19 Serikali iliipatia Hospitali hiyo ya Mkoa Tsh. Milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Oksijeni (Oxygen Implantation).

Aidha, Waziri Ummy amesema kuanzishwa kwa huduma za dharura na mahututi zinategemewa kupunguza vifo vitokanavyo na dharura kwa asilimia 50, huku akiongeza kuwa Serikali inatarajia kuhakikisha kuwa dawa zinapatikana kwa asilimia 100 Hospitalini hapo, kutengeneza lifti katika wodi ya Galanos, kujenga kituo cha uchunguzi na vipimo pamoja na kujenga jengo la tiba shufaa kwa wateja walioathirika na matumizi ya madawa ya kulevya.

Pamoja na hayo Waziri Ummy ameishukuru taasisi ya ABBOTT chini ya makamu wake wa Rais Bw. Andy Wilson kwa kusaidia ukarabati wa jengo la huduma za dharura kwa wagonjwa pia Waziri amewashukuru Wafanyabiashara wa Mkoa wa Tanga kwa kuchangia kuboresha huduma za afya katika Hospitali hiyo.

Kwa upande Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Serikali  ambaue ni Mkurugenzi huduma za Kinga a Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Leonard Subi amesema uzinduzi huo wa huduma za dharura na chumba cha wagonjwa mahututi ni katika utekelezaji wa mkakati wa Wizara ya Afya kuhakikisha huduma hizo zinapatikana katika Hospitali zote za rufaa nchini.

MWISHO

11 on: "WAKAZI WA TANGA KUPATA HUDUMA ZA DHARURA NA MAHUTUTI KATIKA HOSPITALI YA BOMBO"
  1. Thanks for sharing your thoughts. I truly appreciate your efforts and I will be waiting for your next post thank you once again. 바카라사이트인포

    JibuFuta
  2. Terrific work! That is the type of information that are meant to be shared across the net. 바둑이사이트

    JibuFuta
  3. The kind and easy-to-understand explanation made it easy to understand difficult topics. Your writing skills are great. 온라인카지노

    JibuFuta
  4. I’m very pleased to discover this web site. I need to to thank you for ones time just for this fantastic read!! I definitely loved every bit of it and I have you book-marked to see new stuff in your site.

    my website : https://www.casinoholic.info 마마카지노

    JibuFuta
  5. I have joined your feed and look forward to seeking more of your great post.
    바카라사이트

    JibuFuta
  6. Thanks for sharing this marvelous post.
    카지노

    JibuFuta
  7. I'd like more info relating to this, simply because it's very good. Abogado Transito Hopewell VA

    JibuFuta
  8. thanks for taking time to share this information ,must read Proceso de Divorcio Estado de Nueva York

    JibuFuta