Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 18 Desemba 2018

WAZIRI UMMY AGAWA BIMA ZA MATIBABU KWA WATOTO 900 NCHINI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Watoto wanaoishi katika Mazingira magumu na Walezi wao (hawapo kwenye picha) wakati wa kukabidhi Bima za Matibabu kwa Watoto hao wanaoishi katika Mazingira magumu Mkoani Dar es salaam

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dkt. Grace Magembe wakati wa kukabidhi Bima za Matibabu kwa Watoto wanaoishi katika Mazingira magumu Mkoani Dar es salaam

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akimkabidhi Bima ya Matibabu mmoja kati ya watoto wanaoishi katika Mazingira magumu wakati wa sherehe za kukabidhi Bima za Matibabu kwa Watoto wanaoishi katika Mazingira magumu jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na Watoto wanaoishi katika Mazingira magumu wakati wa saherehe za kukabidhi Bima za Matibabu kwa Watoto hao leo katika makao ya Watoto UMRA, Magomeni Mikumi jijini Dar es salaam.




Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na wafanyakazi wa Benki ya  Stanbinc, wakati wa sherehe za kukabidhi Bima za Matibabu kwa Watoto wanaoishi katika Mazingira magumu jijini Dar es salaam.


Na WAMJW - DSM
 
HOTUBA MGENI RASMI WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, MHESHIMIWA UMMY ALLY MWALIMU (MB) KATIKA SHEREHE YA KUKABIDHI BIMA ZA MATIBABU KWA WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU MKOANI DAR ES SALAAM: MAKAO YA WATOTO UMRA, MAGOMENI 

TAREHE 17/12/2018

Ndugu Dkt. John Jingu  Katibu Mkuu, WAMJW, Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii;
Ndugu Ken Cockkerill - Afisa Mtendaji Mkuu wa Stanbic Bank; 
Mganga Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam;
Ndugu Bernard Konga  Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya; 
Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Dar es Salaam;
Ndugu Francisca Makoye Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu  Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam;
Viongozi  wa Siasa na Watendaji Wakuu wa Serikali;
Ndugu Rahma Juma Kishumba  Kiongozi Mlezi wa Makoa ya Watoto UMRA;
Ndugu Viongozi na Waratibu wa Huduma za Ustawi wa Jamii kutoka Manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam;
Ndugu Viongozi wa Makao na Taasisi za Malezi ya Watoto Wanaishi katika Mazingira Magumu;
Ndugu Wanahabari na Wasanii;
Ndugu Wageni Waalikwa;
Ndugu Wananchi.

Asalaam Aleykum, 
Watotoooooo  (Wataitikia  Kwanzaaaaa!!)

Ndugu Wananchi; 
Awali ya yote, naomba tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana hapa Makao ya Watoto UMRA Magomeni. Leo ni siku kubwa na muhimu kwa watoto wote nchini na hususan kwa Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Magumu. Hivyo basi inatupasa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa dhati kwa kutupatia Fursa hii ambapo LEO kwa Msaada wa Benki ya STANBIC tunawapatia Bima za Matibabu Jumla ya Watoto 900 nchini. Kati yao, Mkoa wa Dar es Salaam tunawapatia Bima za Matibabu Jumla ya Watoto 500.

Ndugu Wananchi; 
Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru kwa dhati Benki ya Stanbic kwa moyo wao wa kizalendo wa kuamua kuwalipia Bima za Afya Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Hatarishi. Msaada huu ni muhi sana kwao katika kuhakikisha kuwa wanapata malezi na makuzi bora, hivyo kujiwekea hazina yenye afya bora kwa taifa letu miaka inayokuja.

Vile vile ninawashukuru kwa dhati wenzetu wa Mfuko wa Bima ya Afya kwa kuchukua hatua za haraka katika kupokea, kuchambua na kuhakiki na kupitisha orodha ya majina ya watoto ambayo Wizara yangu iliyapendekeza kupatiwa vitambulisho vya Bima ya Afya. Kasi na umakini mlio onyesha katika kukamilisha zoezi hili inaakisi sawa sawa kauli Mbiu ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya Hapa ni Kazi Tu!

Ndugu Wananchi;
Leo ni siku maalumu kwa watoto wetu wapendwa. Kwa msingi huu sijanuia kutoa hotuba ndefu za kitaalamu kama ambavyo huwa ninafanya katika hadhira nyingine za watu wazima. Hata hivyo ngoja nieleze mambo machache ya msingi hapa chini.

Ndugu Wananchi;
Kupitia Sera ya Afya 2007, Serikali imeendelea kutoa kipaumbele katika huduma za afya zenye ubora na zinazowafikia wananchi wote ili kuboresha afya zao. Serikali inatambua umuhimu wa afya bora kwa wananchi wake kwani afya bora ni raslimali muhimu kwa maendeleo. Kitendo cha kuwapatia Bima ya Afya Watoto wetu leo hii, ni mojawapo ya jitihada za Serikali kwa kukushirikiana na Wadau kama STANBIC BANK katika kuhakikisha kuwa wananchi wote iwemo wale wa makundi maalumu ya uhitaji wanapata Huduma Bora za Afya.

Ndugu Wananchi;
Napenda kuchukua fursa kusisitiza kuwa Maendeleo ya Taifa letu la Tanzania yataletwa na wananchi wenye afya na wenye uwezo wa kuzalisha mali. Katika kuhakikisha kuwa wananchi wana afya bora, Serikali imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutoa huduma za afya kwa kuzingatia sera na miongozo iliyopo. 

Ndugu Wananchi;
Hivyo basi naomba nitoe Wito kwa wengine wa Maendeleo and Sekta Binafsi hapa nchini kuiga mfano wa moyo wa kujitolea kwa kuwasaidia Watanzania wenzetu wasiojiweza kupata mahitaji yao ya msingi ikiwemo uhakika wa kupata huduma bora za afya.

Ndugu Wananchi;
Kama Waziri mwenye dhamana wa kusimamia uendeshaji wa Makao ya Kulelea Watoto Wenye Shida, nachukua fursa hii pia kuueleza Umma wa Watanzania na Wamiliki wa Makao haya juu umuhimu wa kuzingatia Sheria na Kanuni husika. Hili likifanyika vyema, litasaidia kuwa na Makao yanayotoa huduma bora za malezi na makuzi kwa watoto ambao wametoka kwenye shida nyingi maishani mwao. 

Ndugu Wananchi;
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inalojukumu la uratibu wa uanzishwaji na uendeshaji wa Vituo vya Kulelea Watoto Wadogo Mchana na Makao ya Watoto walio katika mazingira hatarishi kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto Na. 21 ya mwaka 2009. Lakini, Pamoja na uwepo wa sheria hii kumekuwepo na changamoto ya uanzishaji na uendeshaji wa Vituo na Makao usiozingatia  sheria na kanuni za uanzishaji wa huduma hizi.

Ndugu Wananchi; 
Katika kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa na Makao Bora ya watoto wenye shida, yenye uwezo wa kuwapatia mahitaji yao ya msingi kama vile Afya Bora ninatoa maelekezo yafuatayo;
Natoa tamko kuwa mamlaka husika katika kila Halmashauri kwa uratibu wa Maafisa Ustawi wa Jamii, wavifunge mara moja Vituo vyote, Makao yote yanayoendeshwa kinyume na sheria. 
Wamiliki wa Vituo na Makao haya watii matakwa ya sheria ya kuwasilisha taarifa za utekekezaji za Mwezi, Robo Mwaka na Mwaka kama ilivyoanishwa katika Kanuni;
Kuanzia sasa ni marufuku kwa mtu yoyote au Shirika kuanzisha Vituo vya Kulelea Watoto Wachanga Mchana na  Makao ya Watoto bila kibali cha Mamlaka husika; 
Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa na Halamashauri za Wilaya kupitia kwa Maafisa Ustawi wa Jamii kufanya Ukaguzi wa Vituo hivi na kuwasilisha taarifa za ukaguzi kila mwezi kwa Msajili ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa, ikiwemo kufunga Vituo visivyokidhi vigezo.
Wamiliki wa Vituo hivi kuzingatia Sheria na Kanuni katika utoaji wa huduma na kujiepusha kutumia huduma hii kwa manufaa binafsi;
Jamii inapaswa kuelewa kuwa familia ndiyo mahala salama kwa malezi ya watoto. Hivyo baba, mama na walezi wa watoto hawana budi kuwajibika ipasavyo kulea watoto wao.

Ndugu Wananchi; 
Kama nilivyotangulia kusema awali leo ni siku muhimu wa Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Magumu, na watoto wote kwa ujumla katika nchi yetu. Maelekezo ya kuzingatia sheria na taratibu husika niliyotoa hapo juu yanatosha kuwafungua masikio wakorofi wachache wasiopenda kufuata taratibu. 

MWISHO

Ndugu Wananchi;
Narudia tena kuwashukuru kwa dhati Benki ya STANBIC KUWAPATIA ZAWADI BORA YA KRISTMASI WATOTO WETU KWA KUWAPATIA BIMA ZA AFYA.

ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA SASA NIPO TAYARI KUWAKABIDHI KADI ZA BIMA YA AFYA WATOTO WETU WAPENDWA.

0 on: "WAZIRI UMMY AGAWA BIMA ZA MATIBABU KWA WATOTO 900 NCHINI"