Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 20 Agosti 2018

WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII WANAHITAJIKA NCHINI

Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na wadau wa sekta ya afya wakati akifungua kikao cha wahudumu wa afya ngazi ya jamii hii leo jijini Dodoma

Mkurugenzi wa huduma za Kinga Wizara ya Afya, Dkt. Leonard Subi akifuatilia kwa makini Maelekezo ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya hayupo pichani katika kikao kilichoshirikisha wadau wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini Dodoma.

Wadau wa afya kutoka mikoa mbalimbali nchini wakisikiliza kwa makini mjadala unaoendelea katika kikao kilichoshirikisha wadau wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini Dodoma.

Katibu mkuu wizara ya afya, Maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa afya katika ufunguzi wa kikao kinachoshirikisha wadau wa afya nchini na wahudumu wa afya ngazi ya jamii.


Wadau wa afya kutoka mikoa mbalimbali nchini wakijadili kwa makundi mada mbalimbali  katika kikao kilichoshirikisha wadau wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini Dodoma.

NA WAMJW-DODOMA 

Wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanahitajika nchini ili waweze kusaidia kutoa elimu kwa wananchi ili kuweza waweze kutafuta huduma za afya kwenye vituo vya kutolea huduma za afya mahali popote.
Hayo yamesemwa leo na katibu Mkuu Wiraya ya Afya,maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Mpoki Ulisubisya wakati kikao cha wadau cha kujadili taarifa ya uchambuzi yakinifu  kwa ajili ya kuhuisha mtaala wa watoa huduma  ya afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini hapa.
Dkt.Mpoki alisema Serikali inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya sekta ya afya yenye lengo la kuboresha huduma za afya na kuimarifa afya za wananchi.
Aidha,alisema wahudumu wa afya ngazi ya jamii  wana nguvu  kwani wana mchango mkubwa mkubwa kwani ni makomandoo ambao wanaweza kutoa elimu kwa jamii na hivyo kusaidia kuzuia magonjwa yanayosababisha vifo vitokanavyo na uzazi.
Alisema takwimu zinaonesha kuwa vifo vitokanavyo na uzazi kati ya akina mama 100,000  ni vifo 556 hutokea  hivyo kuwapo wa hudumu wa afya gazi ya jamii wanaweza kupunguza hali hiyo.
“ Katika kufikia malengo ya Tanzania ya uchumi wa kati na  viwanda, wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanatakiwa kutumika kuwaibua akina mama ambao hawapeleki watoto wao kupata chanjo, na matumizi sahihi ya matumizi ya vyandarua ili kuepuka ugonjwa wa Malaria nah ii imeonekana  pia katika nchi za afrika kam Ethiophia,Rwanda na zingine
Hata hivyo Dkt.Mpoki aliwataka wadau  kuunga mkono  jitihada hizi za serikali na hivyo kubainisha maeneo ambayo watasaidia
Naye Mkurugenzi wa Mafunzo na Wataalam wa Rasiliamali watu Dkt.Otilia Gowele alisema kwa sasa wanapitia upya  mtaala wa mafunzo kwa wa hudumu wa afya ngazi  ili kuendana na hali halisi ya sasa na mahiaji katika sekta ya afya.
“tuekutana ili kupokea na kujadili maoni ya wadau kwa kuzingatia tathimini ya kina iliyofanywa katika kuuhisha mtaala wa mafunzo ya wahudumu wa afya ngazi ya jamii na kuangalia changamoto ili kuendana na mahitaji halisi na kukidhi soko la ajira katika hopsitali za umma na binafsi,” alisema.
Alisema tangu kuanza kutumika kwa mataala wa mafunzo ya watoa huduma wa afya ngazi ya jamii mwaka 2015 na kutumika kwenye vyuo 78 hapa nchini, tayari wataoa huduma wapatao 9,000 wamehitimu.
.
 


0 on: "WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII WANAHITAJIKA NCHINI "