Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 2 Agosti 2018

WAZIRI UMMY AWAAGIZA WAGANGA WAKUU WA MIKOA KUTIMIZA WAJIBU WAO KATIKA KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na Wadau wa masuala ya Afya katika kikao cha tathimini  yakuokoa maisha ya mama na mtoto iliyofanywa mapema leo jijini Dar es salaam na shirika la Thamini Uhai.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Mstaafu Emmanuel Maganga akisisitiza jambo wakati wa kikao cha tathimini yakuokoa maisha ya mama na mtoto iliyofanywa mapema leo jijini Dar es salaam na shirika la Thamini Uhai.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi wakati wa kikao cha tathimini yakuokoa maisha ya mama na mtoto iliyofanywa mapema leo jijini Dar es salaam na shirika la Thamini Uhai.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu baada ya kikao cha tathimini  yakuokoa maisha ya mama na mtoto iliyofanywa mapema leo jijini Dar es salaam na shirika la Thamini Uhai.

 
WAZIRI UMMY AWAAGIZA WAGANGA WAKUU WA MIKOA KUTIMIZA WAJIBU WAO KATIKA KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI.

Na WAMJW-DSM

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa yote nchini kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kikamilifu katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

Amesema hayo mapema leo jijini Dar es salaam katika kikao cha tathmini ya miaka kumi (10) ya kuokoa maisha ya mama na mtoto katika maeneo ambayo ni magumu kufikika, iliyofanywa na Shirika la Thamini Uhai katika Mkoa wa Kigoma.

“Nawataka Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutimiza wajibu wao katika kuondokana na tatizo la  vifo vitokanavyo na uzazi, kwa kuhakikisha vipaumbele vyao viwe na lengo moja kwa moja la kupunguza vifo vya watoto wachanga na mama wajawazito” alisema Mhe. Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy alisema kuwa kama kila mtu atatimiza wajibu wake, inawezekana kabisa ifikapo 2020 vifo vitokanavyo na uzazi vikapungua kwa zaidi ya Asilimia 50%, hivyo kuwaagiza Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha vifaa muhimu vya huduma za uzazi vinakuwepo ili kumsaidia mama mjamzito .

Aidha,Waziri Ummy amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa kufanyia uchunguzi juu ya Vifo vyote vya akina mama wajawazito  vinavyotokea katika vituo  vya kutolea huduma za Afya jambo litaloweza saidia kubaini tatizo lilipo.

“Tumetoa maelekezo  kwa Waganga Wakuu wa Mikoa, kuhakikisha vifo vyote vya akina mama wajawazito vinavyotokea katika vituo vya kutolea huduma na katika jamii, vitolewe taarifa” alisema Mhe. Ummy Mwalimu.

Sambamba na hayo Waziri Ummy alisema kuwa Serikali katika kuhakikisha inapunguza vifo  vya uzazi  kwa kuboresha vituo vya Afya ili kuviwezesha kutoa huduma za wa Dharura ikiwemo upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni,

Aliendelea kusema kuwa Wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani kati ya vituo vya Afya vya Serikali takribani 473, ni vituo vya Afya 117 sawa na Asilimia 21% vilikuwa na uwezo wa kutoa Huduma za upasuaji wa Dharura, hivyo kuwashukuru Wadau kwa kushirikiana na Serikali kuboresha vituo vya Afya 208.

Hata hivyo, Waziri Ummy alisema kuwa katika kuimarisha Afya ya Mama, Uzazi na Mtoto, Serikali imeweka malengo kuwa  ifikapo mwaka  2020 angalau Asilimia 50% ya Vituo vya Afya nchini viweze kutoa huduma hizi kwa ubora unaotakiwa.

“Tunataka itapofika mwaka 2020, tunataka angalau Asilimia 50 ya Vituo vya Afya nchini viweze kutoa huduma hizi, hivyo nikiwa kama msimamizi wa Sera za Afya mpango wangu wa sasa ni kutaka kuhakikisha Ubora wa huduma hizi” alisema Mhe. Ummy Mwalimu

Nae Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Emmanuel Maganga  alisema kuwa Mkoa wa Kigoma umepiga hatua kubwa katika kusogeza huduma za dharura kwa wananchi na kufikia Asilimia 53 ya vituo vya Afya vyote vilivyopo huku wakitarajia kufikia Asilimia 83 ifikapo Desemba mwaka huu baada ya uboreshaji wa vituo vya Afya vingine 10 unaoendelea sasa.

 “Hadi sasa idadi ya vituo vya afya vinavyotoa huduma za Dharura za upasuaji ni Asilimia 53 ya vituo vya Afya vyote vilivyopo huku matarajio ni kufikia asilimia 83 ifikapo Desemba mwaka huu (2018) baada ya uboreshaji wa vituo vya Afya vingine 10 unaoendelea sasa” alisema Mhe. Maganga.

Aliendelea kusema kuwa Idadi ya akina mama wanaojifungulia katika vituo vya kutolea Huduma za Afya imeendelea  kuongezeka kwa kasi sana , mwaka 2015 wakina mama waliojifungua katika vituo vya kutolea huduma za Afya ilikuwa Asilimia 58 ya matarajio, Mwaka 2016 ilikuwa Asilimia 65 na Mwaka 2017 ni Asilimia 78, huku Idadi ya wanaohudhuria kliniki iliongezeka na kufikia Asilimia 113 ya matarajio.

0 on: "WAZIRI UMMY AWAAGIZA WAGANGA WAKUU WA MIKOA KUTIMIZA WAJIBU WAO KATIKA KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI."