Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 21 Machi 2019

HOSPITALI ZA MIKOA ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU ILI KUWEZA KUJIENDESHA

Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati kamati hiyo ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akijibu hbaadhi ya hoja za Wabunge wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii wakati kamati hiyo ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe akisisitiza jambo wakati wa kikao cha kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akijibu hoja mbele ya Wabunge wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi kamati hiyo hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa (Watatu kushoto) akiongozana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (wapili kushoto) pamoja na Wabunge wengine kutoka kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi kamati hiyo hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akieleza kuhusiana na unyanyasaji wa kijinsia, pindi alipotembelea wodi ya wagonjwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala wakati kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi ilipotembelea hospitali hiyo kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula na Wabunge wengine kutoka kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi kamati hiyo hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.


HOSPITALI ZA MIKOA ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU ILI KUWEZA KUJIENDESHA

Na WAMJW - DSM

Matumizi ya fedha za ndani katika Hospitali za umma yanaweza  kutumika katika kutatua uhaba wa watumishi katika ngazi zote na kuacha tabia ya kuisubiri Serikali kufanya kila kitu.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa wakati kamati hiyo ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Aidha,Mhe.Mukasa ameziasa Hospitali hizo kuwa wabunifu ili ziweze  kujiendesha katika kutoa huduma bora  kwa wananchi. 

"Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya ni moja ya maeneo ambayo nimewahi kushuhudia matumizi bora ya fedha za ndani katika kutatua ikama ya watumishi hata ngazi ya Madaktari na Wauguzi " alisema Mhe. Oscar Mukasa.

Akijibu hoja za baadhi ya Wabunge Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha vituo vya Afya na kujenga Hospitali za Wilaya ili kupunguza msongamano katika Hospitali za Rufaa za mikoa.

"Serikali kwa kushirikiana na mamlaka nyingine tumeamua kuboresha vituo vya Afya ili kupunguza mzigo mkubwa kwa Hospitali za Rufaa, na katika Wilaya ya Kinondoni kuna vituo vya afya viwili vinavyojengwa" alisema Dkt Ndugulile 

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa Serikali inatambua kuwa zaidi ya 60% ya watu wanaoenda kupata huduma za Afya ni watu wa misamaha, hivyo kupoteza zaidi ya Bilioni mbili kwa mwezi na hiyo ni kutoka Julai 2018 mpaka mwezi Februari 2019, hali inayorudisha nyuma shughuli za utoaji huduma bora za Afya. 

Aidha,  Dkt Ndugulile amesema kuwa Serikali ipo katika hatua ya  kuhakikisha kila mwananchi anakuwa na Bima ya Afya, ikiwa ni moja ya njia ya kuondokana na tatizo la misamaha kwa matibabu kwa wananchi. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula ameahidi kuendelea kuboresha Sera na miongozo ya Sekta ya Afya ili hali ya utoaji wa huduma bora kwa wananchi iwe ya kuridhisha na stahili kwa wananchi. 

Mwisho.

0 on: "HOSPITALI ZA MIKOA ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU ILI KUWEZA KUJIENDESHA"