Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 23 Machi 2019

KAMATI YA BUNGE YAKUDUMU YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII YAFANYA ZIARA HOSPITALI YA TUMBI-PWANI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akijibu hoja za baadhi ya Wabunge ambao ni wanakamati ya Bunge ya kudumu ya huduma na Maendeleo ya Jamii wakati wa ziara yao ya ukaguzi wa ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Peter Selukamba akihoji jambo lililokwenye taarifa ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje wakati Kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii ilipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongozana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula baada ya kumaliza ziara Kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii ilipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiteta jambo  na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula wakati wa kujibu hoja Wabunge wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii walipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Peter Selukamba akipitia kwa kina taarifa ya ujenzi wa jengo la uchunguzi na jengo la vyumba vya upasuaji ambalo limekamilika kwa 100%,  jengo la wagonjwa wa nje, wakati Kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii ilipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Wabunge na Wajumbe wa kamati ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa za ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje, jengo la uchunguzi na jengo la vyumba vya upasuaji.


Na WAMJW-PWANI

Kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii imefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi ikiwa ni mwendelezo wa ziara yao ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya.

Kwa kiasi kikubwa kamati hiyo imeridhishwa na ujenzi wa jengo la uchunguzi, jengo la vyumba vya upasuaji ambalo limekamilika kwa 100%, huku ikionekana kutoridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje,

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Peter Selukamba amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula kupitia mkataba wa ujenzi wa jengo hilo ili kurekebisha baadhi ya mapungufu ili ujenzi umalizike mapema na huduma zianze kutolewa.

Nae Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amekiri uwepo wa mapungufu na kuahidi kutatua mara moja na huduma zitaanza kutolewa.

0 on: "KAMATI YA BUNGE YAKUDUMU YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII YAFANYA ZIARA HOSPITALI YA TUMBI-PWANI"