Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 27 Machi 2019

SERIKALI YAZINDUA MFUMO WA MATIBABU KWA MTANDAO

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akibofya batani, ikiwa ni ishara ya kuzindua Mfumo mpya wa utoaji huduma za afya kwa njia ya mtandao,  katika Mkutano wa 27 wa masuala ya Sayansi na Afya uliowakutanisha mawaziri wa afya kutoka nchi za Afrika Mashariki katika Kituo cha mikutano ya Kimataifa cha J.K Nyerere Jijini Dar es salaam.

Wadau wa masuala ya Afya, kutoka nchi mbali mbali wakifuatilia ufunguzi wa wa mkutano wa 7 wa masuala ya sayansi na Afya uliowakutanisha mawaziri wa Afya kutoka nchi za Afrika Mashariki, mkutano huo ulifunguliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (Hayupo kwenye picha).

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, akinyanyua juu kitabu cha Mwongozo wa Mfumo mpya wa utoaji huduma za afya kwa njia ya mtandao utaosaidia kurahisisha utoaji wa huduma za Afya kwa wananchi. Wakwanza kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje, Palamagamba Kabudi na Watatu kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.
 

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Wakulia) akipata maelekezo, wakati alipita katika mabanda ya maonesho baada ya kumaliza Mkutano wa Kimataifa wa 7 wa masuala ya Sayansi na Afya uliowakutanisha mawaziri wa afya kutoka nchi za Afrika Mashariki, mkutano huo umefanyika katika Kituo cha mikutano cha Kimataifa cha J.K Nyerere Jijini Dar es salaam.




SERIKALI YAZINDUA MFUMO WA MATIBABU KWA MTANDAO

Na WAMJW - DOM

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo imezindua Mfumo mpya wa utoaji huduma za afya kwa njia ya mtandao utakaosaidia kurahisisha utoaji  huduma za Afya ikiwemo  matibabu ya kibingwa kwa wananchi.

Uzinduzi huo umefanyika  na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 7 wa masuala ya Sayansi na Afya uliowakutanisha mawaziri wa afya kutoka nchi za Afrika Mashariki kujadili kwa pamoja juu ya njia ya kufanikisha malengo ya Afya ya Umoja wa Mataifa.

Mhe. Samia amesema kuwa nchi za Afrika Mashariki zikijikita katika utoaji huduma kwa mfumo huo kwa ushirikiano wa pamoja, itakuwa ni njia sahihi kwa nchi hizo kufikia malengo ya milenia na huduma za afya kwa wote.

“Tunapaswa kufikia malengo tuliyojiwekea kama bara la Afrika na nchi za Afrika mashariki, mkutano huu si tu wa watafiti kutoka Afrika Mashariki bali ni muhimu kwa wadau wote katika sekta ya afya tufanye kazi kwa pamoja kukamilisha malengo haya,” alisema Mhe. Samia.

Mhe. Samia aliendelea kusema kuwa tiba mtandao itawezesha na kuongeza ufanisi katika kufanya uchunguzi, utoaji wa tiba na dawa kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na magonjwa mbalimbali, hivyo kurahisisha utoaji huduma za Afya kwa Wananchi.

Aidha, Mhe. Samia aliongeza kuwa tiba mtandao itapunguza gharama za wagonjwa na wanaowahudumia kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za matibabu katika Vituo vya kutolea huduma na Hospitali.

Naye,Waziri wa Afya na mapambano dhidi ya VVU kutoka Burundi Dkt. Thaddee Ndikumana alisema programu hiyo itakuwa ikitumika kwa nchi za Afrika Mashariki itakuwa chachu katika kuleta Mapinduzi ya utoaji huduma za Afya kwa Wananchi wa Afrika Mashariki.

 “Wananchi wa Burundi watakuwa wanaweza kupatiwa matibabu na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili wakiwa nchini kwao bila kuja Dar es Salaam hiyo ni kitu muhimu tutakuwa tunabadilishana uzoefu raia wa Burundi walikuwa wanakuja kila siku sasa safari zitapungua, watabaki Bunjumbura na huduma watapata.” Amesema Dkt. Thaddee Ndikumana

Kwa upande wake, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa daktari atakuwa na uwezo wa kuwasiliana na madaktari wenzake katika mtandao na madaktari bingwa wa nchi nzima wanaona lile tatizo jambo litalosaidia katika kutoa huduma bora kwa Wananchi wa nchi za Afrika Mashariki.

Waziri Ummy Mwalimu, aliendelea kusema kuwa tayari Tanzania ilishaingia katika mfumo wa matumizi ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwenye maeneo mengi, na umekuwa na msaada mkubwa sana katika Sekta ya Afya.

“Nchini Tanzania miezi mitatu iliyopita madaktari walianzisha mfumo mawasiliano kupitia dijitali ambao unawawezesha madaktari bingwa kuwasiliana moja kwa moja na madaktari waliopo pembezoni na umeweza kuokoa maisha ya kinamama sita ambao walikuwa wanajifungua,” amesema Ummy.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Nimr Profesa Yunus Mgaya alisema kuwa mfumo huo utapunguza gharama za utoaji wa huduma za afya na itaongeza ufanisi katika utendaji wa kazi wa wahudumu wa afya.

“Italeta utaalamu wa hali ya juu wa kibingwa katika maeneo ambayo hauwezi kufikika kwa mfano wataalamu wanaweza kuwepo Muhimbili na mgonjwa akawa mbali ambako hapafikiki kirahisi na hiyo ni msaada mkubwa sana kwa kuwa hizi huduma kama ingetakiwa wataalamu wawepo kule gharama yake ingekuwa kubwa sana,” alisema Prof. Mgaya.

Wakati huohuo, Waziri wa Mambo ya Nje na afrika Mashariki, Palamagamba Kabudi amesema kuwa nchi ya Tanzania itanufaika zaidi katika mfumo huo katika kulifikia lengo namba tatu la malengo ya milenia, pia itasaidia kufanikisha lengo la afya kwa wote ifikapo 2030.

MWISHO

0 on: " SERIKALI YAZINDUA MFUMO WA MATIBABU KWA MTANDAO"