Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 6 Machi 2019

KAMATI YA BUNGE MASUALA YA UKIMWI YATAKA MFUKO WA TAIFA WA UKIMWI KUJITEGEMEA.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akisema jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia Masuala ya UKIMWI na Madawa ya Kulevya mapema jana.

Mama Salma Kikwete, Mjumbe wa Kamati ya Bunge inajishughulishana Masuala ya UKIMWI na Madawa ya Kulevya akisoma nyaraka wakati wa ziara ya kamati walipotembelea Shule ya Sekondari Makoka.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia Masuala ya UKIMWI na Madwa ya Kulevya, Mhe. Oscar Mukasa akisema jambo kwa wajumbe wa kamati hiyo (hawapo pichani) katika ziara ya wajumbe wa kamati hiyo walipotembelea Mkoa wa Dar Es Salaam kujionea hali ya utoaji wa huduma za afya kwenye matibau ya Virusi vya Ukimwi.

Mjumbe wa Kamati ya Bunge inajishughulishana Masuala ya UKIMWI na Madawa ya Kulevya Mama Salma Kikwete (kulia) akisalimiana na Suzana Paul mwanafunzi katika Shule ya Sekondari Makoka.

Mjumbe wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia Masuala ya UKIMWI na Madawa ya Kulevya Mhe. Zainab Vullu akichangia mada katika ziara ya wajumbe wa kamati hiyo walipotembea Mkoa wa Dar Es Salaam kujione ahali ya utoaji wa huduma

Wajumbe wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia Masuala ya UKIMWI na Madawa (waliosimama) wakimsikiliza mtoa huduma za afya katika Kituo cha kutolea dawa za kufubaza Virusi vyta Ukimwi (CTC) katika Hospitali ya Sinza





Wajumbe wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia Masuala ya UKIMWI na Madawa wakimsikiliza mtoa huduma za afya katika Kituo cha kutolea dawa za kufubaza Virusi vyta Ukimwi (CTC) katika Hospitali ya Sinza.


KAMATI YA BUNGE  YATAKA MFUKO WA TAIFA WA UKIMWI KUJITEGEMEA

Na WAMJW - Dar Es Salaam.

Serikali imetakiwa kutenga bajeti ya kutosheleza ili kuuwezesha Mfuko wa Taifa wa Ukimwi kujitegemea na kuepukana na utegemezi wa fedha za wafadhili katika mapambano ya Virusi vya Ukimwi.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia masuala ya UKIMWI na Madawa ya kulevya  Oscar Mukasa wakati wa kamati hiyo ilipofanya ziara  katika Kitengo cha kutolea dawa za kufubaza Virusi vya UKIMWI (CTC) katika Hospitali ya Wilaya ya Ubungo kujionea hali ya utoaji huduma.

Mhe. Oscar Mukasa (MB) amesema suala la upatikanaji wa dawa za kufubaza virusi vya ukimwi ni jambo la kitaifa na kamati yake ina mkakati wa kuhakikisha inaongeza nguvu kwenye Mfuko wa Taifa wa Ukimwi (ATF) na nchi kuweza kujitegemea kuhusu masuala ya  UKIMWI.

“Tuna haja ya kujipanga wenyewe kuhakikisha kwamba tunajitegemea, ule utegemezi wa fedha za wadau za mapambano ya Ukimwi unaweza kupungua”. amesema Mhe. Mukasa.

Mhe. Mukasa amesema Serikali imekuwa ikitegemea fedha za wafadhili kutoka nje ya nchi na sasa ni vizuri tukajipanga wenyewe na kuacha utegemezi wa wafadhili hao kutoa fedha muda wote.

Hata hivyo Mhe. Mukasa amesema kamati yake itaendelea kusimamia Serikali hasa Wizara ya fedha na Ofisi ya Waziri Mkuu kuhakikisha  wanapata chanzo mahsusi cha kodi kwa ajili ya ATF.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo na pia Waziri mwenye dhamana ya Afya, Maendeleo ye Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu amefurahishwa kuona Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imeanza kutekeleza agizo alilolitoa la kutoa ushauri, kupima pamoja na matibabu ya kufubaza virusi vya ukimwi.

Aidha, Waziri Ummy ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kutekeleza agizo la Serikali kwa kutoa dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi kwa muda kwa kipindi cha miezi mitatu kwa wagonjwa ambao wameshachunguzwa na kubainika virusi kufubaa.

“Mpango wetu Serikali kwa wagonjwa ambao watakao kidhi vigezo basi watazipate dawa hizo kwa miezi sita”.  Alisema Waziri Ummy na kuendelea kuwa wanalenga kuwaondolea usumbufu wa kuja mara kwa mara.

Mwisho

0 on: "KAMATI YA BUNGE MASUALA YA UKIMWI YATAKA MFUKO WA TAIFA WA UKIMWI KUJITEGEMEA."